Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, April 13, 2010

Baba ashikiliwa kwa tuhuma za kumkanyaga mtoto wake kwa gari na kusababisha kifo

MKAZI wa Makumbusho, Gharibu Ayubu (35) anashikiliwa kituo cha polisi Kinondoni jijini hapa kwa kumkanyaga kichwani kwa gari lake hadi kufa, mtoto wake, Ayubu Gharibu aliyekuwa na mwaka mmoja na miezi mitano wakati alipokuwa akirudi nyuma ili kutoka katika nyumba yake wakati akitaka kuelekea Sinza. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Elius Kalinga aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 2.00 asubuhi katika nyumba ya Gharibu iliyopo barabara ya New Bagamoyo eneo la Makumbusho katika Wilaya ya Kinondoni. Kalinga alisema tukio hilo lilitokea baada ya mtoto huyo kutaka kwenda na baba yake asubuhi hiyo, lakini baba yake akamkabidhi kwa mkewe ambaye alirudi naye ndani, lakini baada ya muda mtoto huyo alitoka tena nje na kulifuata gari hilo bila mama yake kujua. Alisema mtoto huyo alipolifikia gari hilo aina ya Toyota Folona alikwenda kusimama nyuma yake na Gharibu alipokuwa akirudi nyuma ili aweze kupata mwelekeo wa kutoka katika nyumba yake kuelekea Sinza ghafla akamkanyaga mtoto huyo kichwani na kumsababishia kifo kwa kuwa aliumia sana kichwani. Kamanda Kalinga alisema Gharibu anashikiliwa na jeshi lake na atafikishwa mahakamani huku uchunguzi wa kesi yake ukiendelea kufanyika.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote