Kazi : Mwanamuziki
Mke : Danniella Atim
Chameleon ni mmoja wa wanamuziki maarufu na waliotokea kutamba na kupendwa katika ulimwengu wa Muziki kwenye nchi za Afrika mashariki, pia ameonyesha kipaji cha kuimba nyimbo kwa kutumia lugha za nchi mbalimbali ikiwemo nje ya Afrika Mashariki na hii imeonekana pale alipotoa singo yake ya Maokao & Maoko aliyoiimba ya lugha ya kizimbabwe. Binafsi anazungumza kuwa muziki ni vile wewe unavyoupenda na kuukubali haijalishi hata kama huelewi maana halisi ya nyimbo ( nafikiri anamaanisha midundo)
Chameleon akiwa na Asali wa Moyo wake Danniella Atim siku ya harusi yao.Inasemekana siku ya Harusi Chameleon aliwasili kanisani akitumia usafiri wa ndege ndogo huku bibi harusi Danniella akiwa na msafara wa magari 7 aina ya Benz. Harusi yao ilifanyika Kampala Serena Hotel na inakadiriwa kuwa moja ya harusi maarufu zilizowahi kufanyika nchini Uganda. Nyepesi nyepesi zetu zimetujulisha kuwa watu walikunywa, walikula na kusaza na inakadiriwa kulikuwa na Krate za bia zaidi ya 500 bila kuhesabu vinywaji laini, mivinyo na pombe kali.
No comments:
Post a Comment