
Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Friday, April 23, 2010
Waziri Mkuu wa Ubelgiji awasilisha barua ya kujiuzulu

Tuesday, April 20, 2010
Maimatha kudhamini shindano la uchezaji wa Kiduku!

'ChemChem' ya Pesa Mkoani Ruvuma Yavuta Wengi
WAKAZI wa wilaya ya Songea mkoani Ruvuma wamekuwa wakikesha wilayani humo usiku na mchana wakisubiria pesa zinazotoka chini ya mti mithili ya chemchem. Baadhi ya Wakazi wa mji huo inasemekana waligundua maajabu hayo kwenye mti huo na baada ya wakazi hao kuanza kujizolea pesa toka kwenye mti huo habari ghafla zilisambaa mkoani Ruvuma kuwa kuna mti una chemchem ya pesa.Ilidaiwa kuwa wakazi hao walipokuwa wakipita chini ya mti huo waliona pesa zikitoka chini ya mti na pamoja na kustaajabishwa na tukio hilo wakazi hao waliamua kuzichukua pesa hizo.Taarifa zaidi zilisema kwamba kwa muda wa siku mbili mfulululizo wakazi wa wilaya ya Songea waliendelea kuziokota pesa zilizokuwa zikitoka kwenye mti huo.Pesa hizo inadaiwa zilikuwa zikitoka mithili ya chemchem zikiwa ni noti tofauti tofauti zikiwemo na noti za shilingi elfu kumi, tano na kadhalika.Baadhi ya watoto waliowahi kuhojiwa na mwakilishi wetu wa nifahamishe kutoka eneo la tukio, watoto hao walidai kuwa walishajizolea pesa hizo na walizipeleka kwa wazazi wao nyumbani.Walidai kuwa pesa hizo zilikuwa zikitoka chini ya ardhi na mamia ya watu toka sehemu mbalimbali za mkoani Ruvuma walikuwa wakizigombania kila zilipoanza kuchomoza.Watu wazima waliohojiwa na Nifahamishe nao pia walithibitisha kujizolea noti hizo zilizodaiwa kutoka kwenye chemchem hiyo.Kwa kuwa pesa pesa hizo zilikuwa zinatumia muda mrefu kutoka kwenye chemchem hiyo, maelfu ya watu kutoka wilaya tofauti wamekuwa wakiweka kambi eneo hilo kusubiria pesa hizo.Tukio hilo limethibitishwa na polisi mkoani humo na walisema wanafanya uchunguzi wa kina kubaini kuwa pesa hizo zinakuwa zinatoka wapi.
Tuesday, April 13, 2010
Baba ashikiliwa kwa tuhuma za kumkanyaga mtoto wake kwa gari na kusababisha kifo
MKAZI wa Makumbusho, Gharibu Ayubu (35) anashikiliwa kituo cha polisi Kinondoni jijini hapa kwa kumkanyaga kichwani kwa gari lake hadi kufa, mtoto wake, Ayubu Gharibu aliyekuwa na mwaka mmoja na miezi mitano wakati alipokuwa akirudi nyuma ili kutoka katika nyumba yake wakati akitaka kuelekea Sinza. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Elius Kalinga aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 2.00 asubuhi katika nyumba ya Gharibu iliyopo barabara ya New Bagamoyo eneo la Makumbusho katika Wilaya ya Kinondoni. Kalinga alisema tukio hilo lilitokea baada ya mtoto huyo kutaka kwenda na baba yake asubuhi hiyo, lakini baba yake akamkabidhi kwa mkewe ambaye alirudi naye ndani, lakini baada ya muda mtoto huyo alitoka tena nje na kulifuata gari hilo bila mama yake kujua. Alisema mtoto huyo alipolifikia gari hilo aina ya Toyota Folona alikwenda kusimama nyuma yake na Gharibu alipokuwa akirudi nyuma ili aweze kupata mwelekeo wa kutoka katika nyumba yake kuelekea Sinza ghafla akamkanyaga mtoto huyo kichwani na kumsababishia kifo kwa kuwa aliumia sana kichwani. Kamanda Kalinga alisema Gharibu anashikiliwa na jeshi lake na atafikishwa mahakamani huku uchunguzi wa kesi yake ukiendelea kufanyika.
Ajuza wa miaka 102 aanza darasa la kwanza

Subscribe to:
Posts (Atom)
VJN Super Motors
Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote