Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, April 13, 2010

Ajuza wa miaka 102 aanza darasa la kwanza

Bibi mmoja nchini China amekuwa mwanafunzi mwenye umri mkubwa kuliko wote duniani baada ya kuamua kuanza darasa la kwanza akiwa na umri wa miaka 102. Ma Xiuxian, kutoka Jinan, katika jimbo la Shandong alifanikiwa kutimiza ndoto yake ya kuanza elimu ya msingi akiwa na umri wa miaka 102.Ma alianza kufanya kazi kwenye kiwanda cha nguo tangia alipokuwa na umri wa miaka 13 na kwa miaka yote aliendelea kufanya kazi huku akiwa na ndoto ya kuwa na angalau elimu ya shule ya msingi.Ma aliolewa akiwa na umri wa miaka 18 na alifanikiwa kupata watoto tisa, saba kati yao ni wahitimu wa shahada ya kwanza ya chuo kikuu.Ma alipewa nafasi ya kusoma kwenye shule hiyo baada ya kulieleza gazeti moja la mjini mwake kuwa alikuwa na ndoto ya muda mrefu sana ya kwenda shule."Nina furaha sana nimeweza kutimiza ndoto yangu ya kwenda shule ingawa katika umri huu", alisema Ma.Ma alienda shuleni akisindikizwa na mwanae wa mwisho wa kiume Yi Fengxin mwenye umri wa miaka 58.Katika somo lake la kwanza katika shule yake ya Weishan Road Primary School, Ma alisema "Nawashukuru walimu wangu, nawashukuru wanafunzi wenzangu nawaahidi nitajisomea kwa nguvu zote na nikimaliza shule nitasaidia kulijenga taifa".Ma anatumia kifaa cha kumsaidia kusikia vyema ili aweze kuwasikia walimuwa wake vizuri na huwatumia wanafunzi wenzake kumsaidia kusoma vitabu vya masomo yake.Ma ameingia kwenye rekodi za dunia kwa kuwa mwanafunzi mzee kuliko wanafunzi wote duniani.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote