Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, April 20, 2010

Maimatha kudhamini shindano la uchezaji wa Kiduku!

MAKUNDI matano kati ya nane yamefanikiwa kuingia fainali ya mashindano ya kutafuta bingwa wa kucheza kiduku kwa mwaka huu,baada ya kushinda katika nusu fainali iliyofanyika katika ukumbi wa Traventain uliopo magomeni. Mashindano hayo ambayo,yameandaliwa na Manywele Entertaiment,ambayo ipo chini ya Maimartha,yaliwakutanisha makundi nane kutoka sehemu mbalimbali katika jiji la Dar es Salaam. Katika shindano hilo ambalo wakazi wengi kutoka sehemu mbalimbali katika jiji la Dar es Salaam,walihudhuria na kuujaza ukumbi na kusababisha baadhi ya watu wakose viti vya kukalia na kukaa chin. Vikundi vilivyofanikiwa kuingia fainali ni Vidaleki kutoka Magomeni Makuti,ambao walikuwa wa kwanza kwa kujikusanyia kura 830 na kufutiwa na Stavanga kutoka Mwananyamala waliopata kura 790,washindi wa tatu walikuwa Mazombi kutoka kwa Alimaua A ambapo walipata kura 660,waliofanikiwa kushika nafasi ya nne na tano ni Vsquer kutoka Yombo waliopata kura 650 na Wanaume Fight kutoka Makumbusho waliojikusanyia kura 560. Katika shindano hilo la kumtafuta mkali wa kucheza kiduku,fainali yake inatarajiwa kufanyika Mei 2 mwaka huu,ambapo mshindi wa kwanza atajinyakulia kitita cha Dola 250 za Kimarekani. Hata hivyo Msimamizi wa Shindano hilo Maimartha,hakutaja ukumbi ambao utatumika siku hiyo ya fainali,na kuwatangazia mashabiki waliojitokeza katika shindano hilo,kuwa sehemu ambayo itafanyikia fainali itatangazwa siku zijazo,kabla ya fainali hiyo.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote