Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, April 23, 2010

Waziri Mkuu wa Ubelgiji awasilisha barua ya kujiuzulu

Ubelgiji inaonekana kuingia tena katika mzozo wa kisiasa, baada ya Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Yves Leterme kuwasilisha barua yake ya kujiuzulu kufuatia mgogoro wa lugha. Mgogoro huo ni kati ya jamii inayozungumza Kifaransa na ile inayozungumza Kiflemish. Chama cha kiliberali katika serikali ya Leterme, kimejiondoa katika serikali ya muungano kutokana na sheria za uchaguzi katika vitongoji vya mji mkuu wa nchi hiyo, Brussels. Kiasi jamii ya watu 1,000 wanaozungumza Kiflemish waliingia mitaani kudai mipaka ya wilaya za uchaguzi iwekwe kulingana na lugha. Mfalme Albert wa Pili kwa sasa amekataa hatua ya kujiuzulu Bwana Leterme, akisema kuwa hatua hiyo itatishia ustawi wa Wabelgiji na pia nafasi ya nchi hiyo barani Ulaya. Ubelgiji inajitayarisha kuchukua nafasi ya uenyekiti wa Umoja wa Ulaya mwezi Julai, mwaka huu.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote