Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, March 31, 2010

Mauaji Musoma mganga aongezwa

Kesi ya mauji ya kikatili ya watu 17 wa ukoo mmoja imechukua sura mpya baada ya mtu anayesadikiwa kuwa mganga wa kienyeji kuunganishwa kesi ya mauaji inayowakabili watuhumiwa wengine 18. Mganga huyo ambaye ni mwanamke pekee katika kesi hiyo, alitajwa kuwa ni Mariam Sivanus Masatu, anadaiwa kufanikisha mipango ya mauaji hayo. Masatu jana alipandisha kizimbani kwa mara ya kwanza na kusomewa shitaka la kushiriki katika mauaji hayo yaliotokea usiku wa Februari 16, mwaka huu katika eneo la Buhare, nje kidogo ya Manispaa ya Musoma. Mwendesha Mashitaka, Mrakibu wa Polisi, Gabriel Bonanza, alidai mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Husen Mushi, kuwa kufikishwa mahakamani kwa mtuhumiwa huyo kunaongeza idadi ya kutoka 19 hadi 20, ingawa alisema mtuhumiwa mmoja kati yao amefariki dunia hivyo kubakia watuhumiwa 19. Alimtaja mtuhumiwa aliyefariki kuwa ni Daudi Nyamagati Makika huku akiitaarifu mahakama kuwa mtuhumiwa mwingine, Bundara Ikaka, alishindwa kufika mahakamani jana kutokana na kuwa mgonjwa na kwamba amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mara. Wathumiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote dhidi ya mashitaka 17 ya mauaji na matatu ya kujaribu kuua ambayo yanawakabili. Walirejeshwa rumande hadi Aprili 14, mwaka huu. Polisi wengi walimwagwa kuimarisha ulinzi ili kuepusha uwezekano wa watuhumiwa hao kushambuliwa na watu wenye hasira. Wakazi wengi wa manispaa ya Musoma walijitokeza kuwashuhudia watuhumiwa wakiingia mahakamani. Hati ya mashitaka iliyosomewa watuhumiwa hao, ilidaiwa kuwa watuhumiwa hao waliwaua watu 17 kwa kukusudia wakati wakijua ni kosa. Watuhumiwa katika kesi hiyo ni Marwa Mau Mgaya (16), Matiko Mgasa, Juma Mgaya, Juma Kinonko, Daudi Nyamagati, ambaye ni marehemu, Aloyce Nyakumu, Bahati Simeo, Nyakangara Wambura na Nyakangara Masemere. Wengine ni Kumbata Alphonce, Alphonce Nyabugimbi, Sodaki Alphonce, Mikindo Mgendi, Mole Magesa, Vedastus Nyangeta na Sospiter Mbita, ambaye ni mwalimu wa Shule ya Nsingi Kukirango Usiku wa Februari 16 mwaka huu katika mtaa wa Bugaranjabho watu wasiofahamika walivamia familia tatu za ukoo mmoja na kuwaua kwa kuwachinja na kuwaatakata mapanga watu 17 wakiwemo watoto wachanga kwa kile kilichadaiwa ni ulipizaji wa visasi.

2 comments:

Anonymous said...

hermes replicaHermes Belts lbrz 2013 hermes bagshermes bags oacu

Anonymous said...

Wanting to, this particular could merely got suggests of shopping by using email.
Absolutely ideal males from all areas of life and is defined
as a safe and secure to be able to always be health boosting, slimmer, work with also are more
durable. The two and so on should be the add ons around the informative install related Breville Juice
machine JE95. When you've got any a cancerous tumor nurturing at home then you need to pick the greenstar juicer offers the system of the classic unhurried probably the most compound info or the power each anti-oxidant that an demands within just unsalted plant consist of. If it's not sufficiently strong
enough, you will get spacious bits connected fresh fruit
rather than creamy smoothies recipes.

Feel free to visit my site; turbo blender sinbo

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote