Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Saturday, January 2, 2010

Amuua mama yake kwa kukataza kuuza nyumba ya urithi

Mkazi wa Tabata Jijini Dar es Salaam, Cristabela Mtondo ,60, ameuawa kwa kuchinjwa shingo na mtu anayedaiwa kuwa ni mwanae. Imedaiwa mama huyo alifanyiwa ukatili huo baada ya kukataa kuuza nyumba ya urithi. Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Faustine Shilogile, aliongea na gazeti moja kuwa, mwili wa marehemu uligundulika juzi saa 9:00 alasiri ukiwa ndani ya nyumba aliyokuwa akiishi. Kwa mujibu wa Kamanda Shigolile, polisi wanamshikili kijana huyo aliyetajwa kwa jina la Amani Mtondo. “Polisi walipokwenda kwenye nyumba hiyo walimkuta mtuhumiwa ambaye inadaiwa mara kwa mara alikuwa akimlazimisha mama yake kuiuza nyumba hiyo,”amesema Kamanda. Hata hivyo amesema akasema marehemu (Cristabela), alikuwa akikataa kuiuza nyumba hiyo iliyoachwa na marehemu mumewe. Kamanda Shilogile amesema hadi sasa haijafahamika silaha iliyotumika kumchinja mwanamke huyo na kwamba upelelezi wa tukio unaendelea.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote