
Ashley Jo Beach, mwalimu mwanamke mwenye umri wa miaka 38 (pichani) ambaye ni mama wa watoto watatu, alikamatwa akifanya mapenzi kwenye kichaka na mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 13.Mwalimu huyo pia anatuhumiwa kula uroda na mtoto huyo ndani ya darasa lake huku milango yote ikiwa imefungwa.Wakati alipokuwa akifanya nae mapenzi, mtoto huyo wa kiume alikuwa na umri wa miaka 12."Alianza kutembea nae kimapenzi wakati alipokuwa darasa la sita na yeye akiwa ndio mwalimu wake", alisema mwendesha mashtaka Jean Fisher.Ili kufanikisha azma yake ya kumteka kimapenzi mwanafunzi wake, mwalimu huyo alikuwa akimnunulia zawadi mtoto huyo na wakati mwingine akimtaka awaangalie watoto wake.Mwalimu Beach alikiri makosa yake na kuongeza kuwa anatafuta tiba ya makosa aliyofanya."Imani ambayo nimeivunjia familia yangu na jamii yangu inanisumbua kila siku", mwalimu Beach aliiambia mahakama.Katika hali ya kushangaza zaidi, mume wa mwalimu huyo naye alikamatwa wakati wa uchunguzi wa kesi hiyo kwa kuwapiga picha wafungwa wanawake wakiwa uchi.Alikuwa na ruhusa ya kuingia kwenye jela ya wanawake kutokana na kazi yake aliyokuwa akifanya kwenye ofisi ya mkuu wa polisi.Mume wa mwalimu huyo alimtumia mkewe picha za wafungwa wanawake wakiwa uchi ili kumfanya aone wivu, mahakama iliambiwa.Naye amefunguliwa mashtaka kuhusiana na picha hizo na hivi sasa anasubiria hukumu yake.
No comments:
Post a Comment