Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Monday, November 30, 2009
Je wajua?
Unywaji wa glass nane (8) za maji kwa siku unasaidia kukufanya uwe na afya zaidi pamoja na kupunguza uzito mwilini.
Kwa sasa nipo busy na Muziki shule baadae

D Banj awapagawisha Wabongo

Mapenzi kizunguzungu - Afukua maiti ya Mkewe na kulala nayo kwa miaka 5 mfululizo

Huu ni Uungwana? Watanzania washushwa ndege ya Precision Air na kupakizwa wazungu!!!!!
ZAIDI ya abiria 15 raia wa Tanzania waliokuwa wakisafiri kwa ndege ya Shirika la Precision Air kutoka Arusha kuelekea Dar es Salaam wameshushwa na kupakizwa raia wa kigeni. Tukio hilo lilitokea jana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) na kusababisha mtafaruku uliodumu kwa zaidi ya dakika 30 kabla ya walinzi wa uwanja huo kuingilia kati, ili kutuliza hali hiyo kutokana na abiria hao kugoma kushuka. Wakizungumza na Tanzania Daima uwanjani hapo, abiria hao wamedai kuwa, kitendo cha kuteremshwa katika ndege waliyopanda na kupakizwa abiria wengine ambao ni raia wa kigeni (Wazungu) bila kuelezwa sababu za msingi ni cha ubaguzi wa hali ya juu. Akizungumza na gazeti moja, mmoja wa abiria aliyekumbwa na kadhia hiyo, Pamela Msuya, mkazi wa Dar es Salaam, alisema dakika chache kabla ya ndege kupaa hewani, rubani alizima injini ya ndege na wahudumu kuwaeleza kuwa kumetokea dharura, hivyo hawataweza kupaa. Alisema kutokana na hali hiyo, waliombwa kusubiri hadi saa 5:40 asubuhi. Awali walikuwa waondoke na ndege hiyo saa 1:00 asubuhi. Abiria huyo alieleza kuwa, ilipofika saa 5:40 waliingia katika ndege na rubani kuiwasha, lakini ilizimwa tena na kuamriwa kuteremka kwa maelezo ndege hiyo ilipaswa kupakia abiria wa Zanzibar ambao ni raia wa kigeni. Pamela aliendelea kudai kuwa, wakiwa wanashushwa katika ndege hiyo, baadhi ya abiria waligoma na kusababisha kutokea kwa mtafaruku mkubwa wa zaidi ya dakika 30 kabla ya walinzi wa uwanja huo kuitwa na wahudumu wa ndege hiyo na kwenda kuwashusha huku wakiwaita wazamiaji. “Si siri, tumedhalilishwa sana, yaani tunaitwa wazamiaji mbele ya wageni, watatuelewaje? Tuna booking ya muda mrefu tofauti na hao (raia wa kigeni),” alisema Pamela. Baada ya kushushwa abiria hao, wengine ambao wengi ni raia wa kigeni, walionekana wakipanda ndege hiyo kuelekea Zanzibar. Abiria mwingine ambaye hakupenda kutaja jina litajwe, alisema alishangazwa na kitendo hicho kutokana na abiria hao (wazungu) kutokuwa na taarifa za usafiri (booking) na kwamba walifika muda huohuo na kupatiwa usafiri. Aliongeza kuwa, baadaye waliambiwa kuwa wasubiri ndege ya saa 11:00 jioni ambayo itawapeleka jijini Dar es Salaam. “Tulishushwa tukaambiwa tusubiri ndege ya saa tano, tukavumilia na muda huo ulipofika tena wakatuambia tusubiri ya saa 11. Huu si uungwana hata kidogo,” alisema abiria huyo. Baada ya jitihada za kupata uongozi wa shirika hilo kugonga mwamba, mmoja wa wafanyakazi wa Precision Air mkoani Arusha ambaye alikataa kutaja jina wala cheo chake, alisema kwa kifupi tatizo hilo linashughulikiwa, na alipoulizwa zaidi aliwataka waandishi wa habari waende katika Uwanja wa KIA.
Adai kuiona sura ya YESU kwenye Pasi

Friday, November 27, 2009
Je ni haki Kampuni ya Famili ya Kingunge (Smart Holdings) kupewa Tenda ya kukusanya Mapato Machinga Complex baada ya kuharibu Ubungo Stand?
Vyama vya wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga) kwa kushirikiana na Muungano wa Masoko ya Mkoa wa Dar es Salaam (Mumada), vimeandaa mkutano mkubwa, kujadili pamoja na mambo mengine, uhalali wa kampuni inayomilikiwa na familia ya Mbunge wa Kuteuliwa, Kingunge Ngombale-Mwiru. Familia hiyo imepewa zabuni ya kukusanya mapato katika jengo la Machinga Complex, huku ikiwa imefanya vibaya katika kazi hiyo katika Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT). Vyama vilivyoandaa mkutano huo utakaofanyika wiki ijayo kwa kushirikiana na Mumada, ni pamoja na Asbo, Tamada, Vibindo pamoja na Umoja wa Wafanyabiashara Walemavu Mkoa wa Dar es Salaam (Uwawada). Katibu wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano huo, David Nyendo, alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa tayari wameshaunda kamati ya watu sita, ambayo ina mwakilishi kutoka katika kila chama kwa ajili ya kuratibu mkutano huo. Nyendo alisema mkutano huo utafanyika Desemba 5, mwaka huu, katika ukumbi wa Al-Muntazir (zamani Korea) na kwamba, wanatarajia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi, kuwa mgeni rasmi. “Barua ameshapelekewa. Tulifika Ofisini kwake (Mkuu wa Mkoa), tukamkabidhi Msaidizi wake. Hivyo tunatarajia atakuwa mgeni rasmi katika mkutano wetu,” alisema Nyendo alipozungumza na na chombo kimoja cha habari. Alisema mkutano huo unatarajia kujadili kuhusu maendeleo ya Machinga Complex na mikakati ya kusukuma mambo, ambayo wamachinga wanahisi kuwa yana maslahi nao katika uendeshaji wa jengo hilo lililoko Ilala. Ajenda nyingine ni zabuni ya kukusanya mapato katika jengo hilo, pamoja na uhalali wa kampuni ya Smart Holdings iliyopewa zabuni hiyo ya kukusanya mapato katika jengo hilo. “Tutahoji pia, kwa nini Jiji wameharakia kutangaza zabuni kabla hata jengo halijaisha,” alisema Nyendo. Wakati mkutano huo ukisubiriwa kwa hamu kubwa, habari tulizozipata jana kutoka kwa baadhi ya viongozi wa vyama hivyo, zinaeleza kuwa huenda mkutano huo ukapitisha azimio la kutotoa ushirikiano kwa kampuni hiyo, ikiwa ni pamoja na kugomea kuilipa chochote kwa lengo la kushinikiza zabuni waliyopewa Smart Holdings itangazwe upya. “Kama mtu kaharibu Ubungo hadi Waziri Mkuu akaagiza ukaguzi ufanyike, iweje apewe sehemu nyingine akaharibu?” alihoji kiongozi mmoja wa Asbo, ambaye hata hivyo, hakutaka jina lake liandikwe magazetini kwa maelezo kuwa si msemaji wa chama. Licha ya kampuni hiyo ya mwanasiasa mkongwe nchini kufanya vibaya katika kazi ya ukusanyaji mapato ya serikali katika Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT), kiongozi huyo alidai kuwa ushindi wa zabuni yake umegubikwa na utata. Alidai utata huo unatokana na moja ya makampuni yaliyoomba zabuni hiyo, kampuni ya Amma Consult Limited, kuibuka mshindi katika kinyang’anyiro cha kuwania zabuni hiyo, lakini ikanyang’anywa ushindi huo na zabuni hiyo kutolewa kwa Smart Holdings Limited katika mazingira ya kutatanisha. Kampuni nyingine iliyowania zabuni hiyo, lakini ikashindwa, ni Zing Company. “Aliyenyang’anywa ushindi ‘alitenda’ zaidi ya Sh. bilioni 1.2 na alionyesha uwezo wake na namna atakavyoweza kufanya kazi hiyo, lakini aliyepewa zabuni alitenda fedha kidogo,” alidai bila kufafanua. Aliongeza: “Kampuni ya Amma Consult Limited ndiyo iliyokuwa imeshinda mwanzo, lakini katika hali ya kushangaza afisa mmoja wa kitengo cha manunuzi cha Halmashauri ya Jiji akainyang’anya ushindi.” Alidai katika kutekeleza njama hizo, Bodi ya Usimamizi na Uendeshaji wa jengo hilo haikushirikishwa katika hatua yoyote ya mchakato wa kumpata mzabuni licha ya Mwenyekiti wake, ambaye pia ni Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan Zungu (CCM) kuagiza suala hilo. Badala yake, bodi iliishia tu kualikwa kwenye ufunguzi wa kinyang’anyiro cha zabuni.
Hongera Babu Sikare

Daznundaz kurudi tena?

Je wajua?
CHOKORAA apewa kadi ya Njano Twangapepeta

Tibaigana atengua hukumu ya kifungo cha maisha kwa OTHUMAN KAZI

Thursday, November 26, 2009
Wafanyakazi Watano wa Kampuni moja wafariki dunia kwa mpigo
WAFANYAKAZI watano wa Kampuni ya ujenzi ya SICU ya jijini Dar es Salaam, wamefariki dunia na wengine 12 kujeruhiwa, baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kupinduka. Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Leonard Paul, alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea jana, majira ya saa moja usiku katika Kijiji cha Inokanoka, wilayani Ngorongoro na kulihusisha gari T 372 AFC Mitsubishi Canter. Kamanda Paul aliwataja waliokufa katika ajali hiyo kuwa ni Letuyo Lembeu (38), Ngidadiya Paluny (38), Oleyumbayiguti Pasani (36), John Mgawa (50) na Mesikongi Silelian (25), wote wakazi wa Ngorongoro. Aidha, waliojeruhiwa na kulazwa katika hospitali ya wilaya ni pamoja na Ezekiel Habali (27), Brayson Bake (26) na Azizi Hassan (27). Alieleza kuwa chanzo cha ajali hiyo kilitokana na ubovu wa barabara, hatua ambayo ilisababisha dereva wa gari hilo kushindwa kulimudu na kuacha njia kabla ya kupinduka. Polisi wanamshikilia dereva wa gari hilo, Huchen Weni (28), ambaye ni raia wa China kwa uchunguzi zaidi. Kamanda Paulo alifafanua kuwa gari hilo ni mali ya Kampuni ya ujenzi ya SICU ya jijini Dar es Salaam na lilikuwa linatoka Campu likiwa limebeba wafanyakazi 17 wa kampuni hiyo kuelekea eneo la Sopa na lilipofika kwenye kona liliacha njia na kupinduka.
Hali ya Mjamzito aliyekataliwa Hospitali ya Mwananyamala bado ni tata
HALI ya mwanamke mjamzito ambaye kiumbe chake kimefia tumboni tangu wiki iliyopita, bado ni tete, huku ndugu zake wakijitahidi kutafuta tiba ili kunusuru maisha yake. Akizungumza na Tanzania Daima nyumbani kwao Mwananyamala A, dada mkubwa wa mgonjwa huyo ambaye hakuwa tayari kutaja jina lake kwa kuogopa kuendelea kukosa ushirikiano kutoka Hospitali ya Mwananyamala, alisema hali ya ndugu yao si nzuri. “Kusema kweli ndugu yetu bado hali yake si nzuri, maana hata hii (leo) jana tumerudi tena Hospitali ya Mwananyamala lakini hakuna tiba tuliyopata,” alieleza. Aliongeza kuwa hata jana walipokwenda na kumtafuta daktari wa wasaidia, aliwaeleza kuwa wasubiri muda wa wiki mbili waliopangiwa awali. Alisema kutokana na majibu hayo, waliamua kurudi nyumbani na mgonjwa huyo huku wakijaribu kuwasiliana na ndugu wengine, ili kutafuta fedha kwa ajili ya kumpeleka katika hospitali binafsi. “Kwa sasa hatuna njia nyingine, kwa muda huu tunajaribu kukusanyana na kufanya kikao ili tumpeleke katika hospitali binafsi, kwani hatuwezi kukaa kwa wiki mbili, kwani hali yake ni mbaya,” alisisitiza.
Wednesday, November 25, 2009
Liyumba aendelea Kusota lupango

Utata wa Makusanyo ya mapato Kituo cha Ubungo - Jiji yaiumbua familia ya Kingunge
Makusanyo ya mapato katika Kituo Kikuu cha Mabasi cha Ubungo (UBT), yameongezeka maradufu, ikiwa ni wiki chache tangu mkataba wa kampuni binafsi inayomilikiwa na familia ya Mbunge wa Kuteuliwa, Kingunge Ngombale-Mwiru, kumalizika na kazi hiyo kukabidhiwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ilianza rasmi kusanya mapato kituoni hapo Novemba Mosi, mwaka huu baada ya kampuni hiyo ya familia ya Kingunge ya Smart Holdings, iliyokuwa imepewa zabuni hiyo kwa zaidi ya miaka mitano kumaliza mkataba wake mwishoni mwa mwezi uliopita. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Bakari Kingobi, alisema jana kuwa tangu Halmashauri ianze kazi hiyo, imekuwa ikikusanya mapato ya wastani wa Shilingi milioni nne kwa siku. Kingobi aliyasema hayo jana alipokuwa akitoa taarifa katika kikao cha Madiwani wa Jiji la Dar es Salaam. Kwa hesabu hiyo, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, kwa mwezi itakuwa ikikusanya Sh. milioni 120. Awali, kampuni ya Smart Holdings ililalamikiwa kuwa ilikuwa ikikusanya mapato makubwa katika kituo hicho, lakini ikiishia kuilipa serikali fedha kidogo Sh. milioni 1.5 tu kwa siku. Katika makusanyo hayo, kampuni hiyo ilikuwa ikiilipa serikali sh. milioni 46.5 kwa mwezi. Kutokana na hali hiyo, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alimuagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, kufanya ukaguzi wa hesabu za mapato katika kituo hicho na katika Shirika la Masoko ya Kariakoo, jijini Dar es Salaam na kisha kuwasilisha ripoti ofisini kwake. Pinda alitoa agizo hilo wakati akizungumza katika kikao cha majumuisho, baada ya ziara yake ya siku tatu, jijini Dar es Salaam, Machi 15, mwaka huu. Katika agizo lake, Pinda alisema bila kujali mmiliki halali wa kampuni hiyo, ukaguzi wa hesabu hizo unapaswa kufanyika kwa maslahi ya umma, kabla ya kuchukua hatua kwa mujibu wa mapendekezo yatakayotolewa na CAG. Katika ziara hiyo, Pinda alishangazwa na kushtushwa na utendaji mbovu wa uongozi wa UBT, mkataba uliofikiwa kati ya kituo hicho na kampuni hiyo na namna ilivyopatikana. Pinda alifikia hali hiyo, baada ya kupewa taarifa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji, Kingobi, kuhusu hali ya utendaji wa uongozi wa UBT, ukusanyaji wa mapato, mkataba wa mkandarasi na maendeleo ya kituo hicho. Katika taarifa yake, Meneja wa Kituo hicho, Fadhili Izumbe, alisema kwa mujibu wa mkataba, mkandarasi huyo huipa Halmashauri ya Jiji, Sh. milioni 1.5 kwa siku, taarifa iliyomshangaza Pinda na kumfanya ahoji: “Hata kama anakusanya Shilingi bilioni moja anatoa Sh. milioni 1.5? Na kwa nini mkataba utamke shilingi badala ya asilimia?”. Kwa siku mabasi zaidi 400 husafirisha abiria, teksi 100 na watu zaidi ya 2,000 huingia UBT. Pia, kuna maduka ya vinywaji (baa na grosari), maduka ya kawaida, hoteli, ‘vioski’, gereji, ambavyo vyote hulipa ada za viwango mbalimbali. Siku moja baada ya ziara hiyo ya Pinda, mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Smart Holdings, Hassan Khan, alisema viongozi wa Halmashauri ya Jiji waliokuwapo kwenye ziara hiyo, hawajui lo lote na ndio maana walishindwa kumueleza Waziri Mkuu ukweli kuhusu mkataba huo. Khan alisema katika mkataba huo, walikubaliana na Halmashauri ya Jiji kuwa wangekuwa wakiilipa asilimia 75 na kushangazwa kusema asilimia hiyo ni sawa na Sh. milioni 1.5. Alisema katika mkataba huo, pia walikubaliana wawe wanalipa kiasi hicho cha fedha kwa kila siku bila kujali hali ya mapato itakayokuwa na bila kujali pia kuwa siku za mwishoni mwa juma (wikiendi) na wakati madaraja yanapokatika, kampuni yao hupata hasara. Utouh alikabidhi ripoti ya UBT mjini Dodoma, Julai mwaka huu, wakati wa Mkutano wa 16 wa Bunge. Akijibu maswali ya papo kwa papo mwishoni mwa mwezi uliopita bungeni, Pinda alisema ripoti hiyo inapitiwa na Katibu Mkuu wa Tamisemi na yule wa Ofisi ya Waziri Mkuu na kuahidi kuwa itatolewa hadharani baada ya maofisa hao wa serikali kumaliza kazi ya kuipitia. Hata hivyo, kabla Pinda hajatoa kauli hiyo, wiki kadhaa zilizopita, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi, alidokeza kuwa serikali ingechukua kituo cha Ubungo kupitia Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam mwisho wa mwezi uliopita.
Rihhana akanusha kuwa na mahusiano ya mapenzi ya Jay - Z

Tuesday, November 24, 2009
Yanga yamtosa Ambani
.jpg)
Apata Mimba baada ya kufunga kizazi

Walimu 22 wafukuzwa kwa Ulevi Singida
Walimu 22 katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida, wamesimamishwa kazi kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo ulevi na utoro kazini. Hayo yalibainishwa mwishoni mwa wiki na ofisa Elimu wa Wilaya ya Iramba, Leonard Ngaharo, kwenye mkutano wa viongozi uliofanyika katika kijiji cha Mwanga, Tarafa ya Nduguti. Mkutano huo uliitishwa na Mbunge wa Iramba Mashariki, Mgana Msindai. Ngaharo alisema walimu hao wamesimamishwa kazi katika kipindi cha miezi miwili iliyopita ikiwa ni mkakati wa wilaya hiyo kuhakikisha taaluma inayotolewa kwenye shule zake za msingi, inakuwa na ubora unaostahili. Alisema walimu hao wamesimamishwa kazi kutokana na makosa ya kukiuka mikataba ikiwemo ulevi na utoro kazini. Aidha, Ofisa Elimu huyo alisema ofisi yake itawahamisha walimu wote waliokaa kwenye kituo kimoja kwa muda mrefu ili kuleta ufanisi na upatikanaji elimu bora kwenye shule zake za msingi. Ngaharo alilazimika kutoa ufafanuzi huo kufuatia ombi la kiongozi wa serikali za mitaa kumwomba Msindai asaidie kuwahamisha walimu wa shule ya msingi waliotumika kwa miaka mingi kwenye Kata ya Mwanga. Kwa upande wake, Mbunge huyo aliwataka viongozi wa dini kufanya kazi kwa bidii na kujenga uhusiano mwema kati yao na waumini wanaowaongoza, huku akiiasa jamii kuheshimu mema yote wanayoelekezwa. “Naomba sana waongozeni waumini wenu kwa njia za haki, msikate tamaa na endeleeni kuwahimiza wafanye kazi zaidi, ikiwemo utoaji wa michango ya miradi mbalimbali ya maendeleo…ya Kaisari mpe Kaisari na ya Mungu mpe Mungu,” alifafanua Msindai. Mbunge huyo alikuwa kwenye ziara katika jimbo lake hususani Kata za Mwanga na Ilunda, ambapo aliwahimiza wananchi kushiriki kwenye miradi ya maendeleo na kutumia vizuri mvua zinazonyesha sasa ili washiriki fursa ya kilimo kwanza.
Busta Asifia Ukarimu wa watanzania

Monday, November 23, 2009
Mwanaume aliyepoteza fahamu kwa miaka 23 azinduka


Sisi mabingwa watarajiwa Chalenji atamba Maximo
.jpg)
Mtoto wa ajabu azaliwa - LINDI
Mkazi mmoja wa Mtaa wa Rupiani katika Halmashauri ya Mji wa Lindi na ambaye hufahamika kwa jina la Salima Ally, 38, amejifungua mtoto wa ajabu na kuzua gumzo la aina yake kwa madokta na wauguzi wa Hospitali ya Mkoa wa Lindi. Mtoto huyo ambaye ni wa kike, amekuwa gumzo kwani licha ya kuzaliwa na afya njema na uzito wake wa kilo 3.2, imebainika kuwa hana macho wala pua. Aidha, mtoto huyo ana mdomo wenye mpasuko mkubwa kiasi cha kumfanya ashindwe kunyonya mwenyewe, huku kwenye paji la uso akiwa na uvimbe usio wa kawaida. Mtoto huyo alizaliwa jana, mishale ya saa 11:30 asubuhi katika hospitali hiyo ya mkoa wa Lindi iitwayo Sokoine. Akizungumza na mwandishi wa habari hii hospitalini hapo, Afisa Muuguzi wa zamu katika wodi hiyo ya wazazi namba nne aitwaye Bi. Zuhura Namkovera, amesema mtoto huyo alizaliwa salama lakini kinachosikitisha ni kwamba hadi sasa, maumbile yake ya ajabu yamemfanya aishi kwa shida mno. “Tangu azaliwe, mtoto huyu tumekuwa tukimnywesha maji, tena huwa anakunywa kwa shida sana kutokana na maumbile ya mdomo wake, ” amesema muuguzi huyo. Akieleza zaidi, Muuguzi huyo akasema kuwa huo ni uzazi wa sita wa mama huyo kwa mume aliyenaye. "Maendeleo ya afya ya mama (Bi. Salma) yanaendelea vizuri… na mtoto wake pia anaendelea vizuri, licha ya kwamba hajaanza kunyonya mwenyewe maziwa ya mama yake,” akasema Bi. Zuhura . Naye mganga aliyekuwa zamu katika hospitali hiyo, Dokta Jumanne Shija, amesema kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha hali hiyo, ikiwa ni pamoja na mama kuwahi kuathiriwa na magonjwa mbalimbali. “Ila mambo mengine yanakuwa ni maumbile tu… ni baada ya baadhi ya vichocheo vya mwili kushindwa kufanya kazi yake,” akasema Dk. Shija.
Wananchi Newala wazuia Msafara wa Waziri Mkuu
.jpg)
Shoga aliyeleta Kizaazaa Italia Achomwa Moto na Kufa

Aliyemuua Mkewe akiwa Usingizini aachiwa huru

Mahujaji 4 wafariki kwa mafua ya Nguruwe

Mwanaume mmoja toka India, mwanamke mmoja toka Morocco na mwanaume mwingine toka Sudan wote wenye umri zaidi ya miaka 75 pamoja na msichana mwenye umri wa miaka 17 toka Nigeria wamefariki dunia kutokana na ugonjwa wa homa ya mafua ya nguruwe walioambukizwa wakati wa hija."Wote walikuwa na matatizo mbali mbali ya kiafya kabla ya kukumbwa na mafua ya nguruwe, msichana wa Kinigeria alikuwa na matatizo ya kifua", alisema msemaji wa wizara ya afya ya Saudia, Khaled al-Marghlani."Pia hakuna hata mmoja wao aliyepiga sindano ya chanjo ya ugonjwa wa mafua ya nguruwe", aliongeza msemaji huyo wa wizara ya afya.Takribani waislamu milioni 2.5 wanatarajiwa kuhudhuria hija ya mwaka huu, ukiwa ni mkusanyiko mkubwa kuliko wote wa watu tangia ugonjwa wa mafua ya nguruwe ulipogunduliwa nchini Mexico mwezi aprili mwaka huu.Watu 20 wamegundulika kuambukizwa mafua ya nguruwe tangia hija zilipoanza katika miji ya Makka na Madina na 12 kati yao walipatiwa matibabu na kutolewa hospitali wakati watu wanne bado wamelazwa hospitali.Wataalamu wa masuala ya afya wamesema kuwa maambukizi ya ugonjwa huo yamekuwa katika kiwango kidogo sana kuliko ilivyohofiwa kutokana na tahadhari zilizochukuliwa.Wataalamu wa afya 20,000 wamepelekwa kwenye miji ya Makka, Madina na Jeddah kuwa tayari tayari kupokea watu watakaoambukizwa ugonjwa huo huku hospitali zimewekwa mamia ya vitanda vya ziada.Mawe yatakayotumika kuipiga alama ya shetani wakati wa hija, nayo yamewekwa madawa kuzuia maambukizi ya ugonjwa huo.Watu wenye magonjwa sugu, wazee sana, watoto na wanawake wenye mimba wametakiwa kuahirisha safari zao za hija mwaka huu.
Thursday, November 19, 2009
Sina mpango wa kugombea urais 2010 - Dr. Slaa

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Dk Slaa ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Karatu, alisema "Ikulu si mahali pazuri kukimbilia na urais si mchezo wa kitoto." Alisema wakati alipojiundoa katika upadre na kujitumbukiza katika ulimwengu wa kawaida, aliahidi kuwatumikia wananchi wa Karatu na si kutafuta njia ya kuingia Ikulu, ambako alisema kuna matatizo mengi yanayoweza kumfanya mtu kukosa usingizi. Unajua Ikulu si lele mama, kunahitaji mtu mvumilivu hasa wananchi wake wanapohangaika na ugumu wa maisha ya kila siku, jambo ambalo linaweza kumfanya ashindwe kupata usingizi, kwa sababu ya mawazo,alisema Dk Slaa. Alisema kama mtu anataka kugombea nafasi hiyo anapaswa kukumbuka maneno ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kuwa mtu anayekimbilia Ikulu anapaswa kuogopwa kama ukoma. Alisema mtu wa aina hiyo mara nyingi anakusukumwa na maslahi binafsi kuliko maendeleo ya watu. Dk Slaa alisema maendeleo yanapatikana bila ya hata kuingia ikulu na kwamba la msingi ni viongozi kujipanga katika kupigania maendeleo ya wananchi. Alisema mkakati wake ni kuhakikisha kuwa wananchi wa Karatu wananufaika na uongozi wake kwa kuwatafutia maendeleo na kuwaondolea kero kama ya maji na kadhalika. Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na uvumi kwa Dk Slaa ana mpango wa kuwania kiti cha urais kupitia tiketi ya Chadema. Kwa mujibu wa habari hizo, Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, hana mpango wa kuwania tena nafasi hiyo na badala yake anakwenda kuwania ubunge katika Jimbo la Hai mkoani Kilimanjaro.
Baba wa kijana Aliyedai Amebakwa na Michael Jackson Ajiua

Dunia Imefika mwisho - Mchungaji Kortin Singida kwa kubaka
POLISI mkoani Singida linamshikilia Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) wa Usharika wa Igengu katika Dayosisi ya Kati, kwa tuhuma ya kumbaka msichana mwenye umri wa miaka 18 na kumtelekeza . Ilidaiwa msichana huyo (jina kapuni) alibakwa na mchungaji huyo na kusababishiwa maumivu makali katika sehemu zake za siri.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Celina Kaluba, alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Japhet Kidindima (37) mkazi wa wilayani Iramba mkoani humo.Kamanda Kaluba alisema kuwa tukio hilo lilitokea Jumatatu ya wiki hii, katika majira ya saa 9:45 alasiri, kwenye vichaka vilivyopo kati ya vijiji vya Igengu na Ibaga katika tarafa ya Kirumi, wilayani Iramba.Kamanda Kaluba alisema kuwa, mtuhumiwa huyo alifanikisha njama zake za ubakaji baada ya kumdanganya msichana huyo kuwa anataka kumtafutia kazi za ndani jijini Dar es Salaam.Kamanda alisema licha ya kumuahidi kumtafutia ajira, pia Mchungaji huyo alimuahidi msichana kuyo kumsafirisha hadi Dar es Salaam kwa ajili ya kwenda kufanya kazi hiyo.Alisema kuwa safari ya kwenda kijiji jirani cha Ibaga ilianza kwa miguu ambako ndipo ulipo usafiri wa basi, lakini walipofika katikati ya vijiji hivyo, Mchungaji Kidindima alimbaka msichana huyo kwenye vichaka.Alifafanua kuwa baada ya kumbaka, waliendelea na safari yao hadi kwenye kituo cha mabasi kilichopo kijiji cha Ibaga na hapo ndipo mtuhumiwa alifanikiwa kumtelekeza msichana huyo akiwa haelewi cha kufanya.Kamanda Kaluba alisema kuwa baadaye msichana huyo aliamua kuripoti tukio hilo katika kituo cha polisi kilichopo katika kijiji cha Ibaga kesho yake saa 7:30 mchana na jitihada za polisi kumsaka mtuhumiwa huyo zilianza.Alisema polisi walifanikiwa kumkamata Mchungaji Kidindima jana, majira ya saa tano asubuhi wakati akiwa masomoni kwenye chuo cha Biblia mjini Kiomboi.Hatua za awali zinachukuliwa ili mchungaji huyo aweze kufikishwa mahakamani kujibu tuhmu hizo za ubakaji na kutelekeza binti huyo vichakani.
Kuweni makini na Urembo wa Madukani

Monday, November 16, 2009
FIFA yamfungia Maradona Miezi miwili

Auwawa kikatili na Mumewe kisa kutakaa kuokota EMBE usiku
MSICHANA Khadija Daudi (22), mkazi wa Mbagala Charambe aliuawa kikatili na mumewe kwa kuchomwa na kisu mgongoni kwa kile kilichodaiwa kuwa ni baada ya kukataa kuamka usiku kwenda kuokota embe. Tukio hilo la kusikitisha lilitoka mwishoni mwa wiki huko Mbagala jijini Dar es Salaam.Ilidaiwa kuwa chanzo cha kifo hicho ni mume wa msichana huyo aliyetambulika kwa jina la Shariff Kondo alimuamsha marehemu kumtaka aende nje ya nyumba yao majira ya saa kumi kasoro usiku, aende akaokote embe lakini marehemu aligoma na kudai kwa kuwa ni usiku asingeweza kwenda nje kufanya kazi hiyo.Inadaiwa kuwa kutokana na majibu hayo mumewe alikasirika na ndipo alipochukua kisu na kumchoma nacho mgongoni.Baada ya kuchomwa kisu hicho alipiga kelele na majirani walijitokeza kumpa msaada wa kumkimbiza Hospitali ya Temeke huku akiwaambia kilichomtokea kwa mumewe huyo.Kwa bahati mbaya msichana huyo alipoteza fahamu na kufariki mara baada ya kufikishwa hospitalini hapo.Wakithibitisha tukio hilo baadhi ya majirani wa marehemu huyo, wamedai kuwa walisikia kelele za kuomba msaada katika chumba cha mpangaji mwenzao na mara baada ya kuingia ndani kwake kujua kilichotokea ndipo walipokuta kitanda chake kimelowa damu na huku akiugulia maumivu.Majirani hao wamesema kutokana na hali hiyo walikwenda kutoa taarifa kituo cha polisi na baadhi yao walijaribu kumtafuta mumewe lakini hakupatikana ndipo walipokwenda kumwamsha baba mzazi wa msichana huyo anayeishi Charambe na kumuelezea yaliyompata binti yake.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Liberatus Sabasi, amesema kuwa, tayari mtuhumiwa aliyehusika na tukio hilo tayari ameshakamatwa yuko katika kituo cha polisi cha Chan’gombe na anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo.
Friday, November 13, 2009
Mtandao wa wezi wa Magari wakamatwa Dar
MTANDAO mkubwa wa wezi wa magari uliokuwa ukiongozwa na mwanamke mwenye asili ya Mnyarwanda umekamatwa.Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Suleiman Kova, amesema, mtandao huo ulinaswa na polisi wanaoendesha msako mkali kuwasaka wahalifu hao kote nchini.Amesema mtandao huo ulikuwa ukiongozwa na mwanamke Meritha Mwanahawa (20), ambaye katika kumbukumbu zake imeonesha kuwa ni bingwa wa kuwalaghai wanaume kimapenzi ambapo huenda kufanya nao mapenzi kisha kuwanywesha dawa za kulevya na kuwaibia funguo na kutoweka na magari yao.Amesema kuwa kumbukumbu za magari mengi yaliyoibwa zimeonyesha kuwa msichana huyo alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na baadhi ya madereva hao ambaod wealikiri wenyewe.Wengine walionaswa katika mtandao huo ni pamoja na Hamis Fumu (37), Arafat Juma (34), Samwel Mwamba (19), Yasmin Chuchu (20), Antipasi Kilawe (28) na Elias Moses (35).Kamanda Kova amesema kuwa jeshi lake bado linaendelea na msako mkali na litawafikisha mahakamani watuhumiwa baada ya upelelezi kukamilika.
Tyson Matatani kwa kumpiga Mpiga Picha ngumi ya uso na kumpasua

Mbwa wahitajika zoezi la kutafuta Miili ya waliopoteza maisha Same
.jpg)
Wednesday, November 11, 2009
Hatimaje Elizabeth kutua Dar Leo
Msiba mzito Same

Ahudhuria mazishi yake

Akata nyeti za baba yake wa kambo na kuzichoma moto

Golikipa wa timu ya Taifa ya Ujerumani ajiua

Tuesday, November 10, 2009
Kuweni makini na Mapenzi ya kwenye Mtandao

Thursday, November 5, 2009
Mbatia aibuka na kusema "Takukuru, Wabunge wote ni WAFISADI"
.jpg)
Ahukumiwa kunyongwa na mwili wake Kuwekwa Msalabani
Mwanaume mmoja nchini Saudi Arabia ambaye aliwabaka watoto watano miongoni mwao akiwemo mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka mitatu ambaye alimtelekeza jangwani afariki, amehukumiwa kunyongwa na kisha mwili wake kuwekwa kwenye msalaba. Mahakama nchini Saudi Arabia imemhukumu mwanaume aliyewabaka watoto watano adhabu ya kunyongwa na kisha mwili wake kuwekwa kwenye msalaba na kisha kuwekwa hadharani watu waushuhudie.Mwanaume huyo mbali ya kuwabaka watoto hao watano, alimchukua mtoto mmoja wa kiume aliyembaka na kumtelekeza katikati ya jangwa ili afariki mwenyewe.Mahakama ya rufaa ya mjini Riyadh imethibitisha adhabu hiyo ambayo ilitolewa mwezi juni mwaka huu na mahakama moja ndogo ya mji wa Hail ambako mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 22 alifanya unyama wake huo,limeripoti gazeti la Okaz la Saudi Arabia.Baada ya kunyongwa mbele ya hadhara, mwili wake utawekwa kwenye msalaba na kuwekwa wazi kwenye hadhara watu waushuhudie.Mwanaume huyo ambaye hakutajwa jina lake, alikamatwa wiki chache zilizopita baada ya kujaribu kumlaghai mtoto mwingine kwa kumpa lifti ya baiskeli kutoka nyumbani kwao hadi shuleni kwao.
Watu 4 wakamatwa na Meno ya Tembo Dar
JESHI la polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata watu wanne wakiwa na meno ya Tembo vipande 33 kinyume na sheria za nchi. Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, ASP Suleimani Kova aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa, nyara hizo zilikamatwa maeneo ya Mbagala Nzasa Wilayani Temeke wakijaribu kuzisafirisha nyara hizo nje ya nchi.Kamanda Kova alisema watu waliokamatwa walikutwa wakijiandaa kupeleka nje ya nchi nyara hizo wakati hawana nyaraka zozote za umiliki wa meno hayo.Alisema nyara hizo za serikali zina uzito wa kilo 102.9 zenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 7, na kwamba zilikamatwa baada ya polisi kupata taarifa kutoka kwa raia wema.
Monday, November 2, 2009
Kitoto kichanga chaopolewa kutoka kwenye tundu la choo kikiwa hai
MTOTO mchanga wa siku moja ameopolewa akiwa hai akiwa ametupwa ndani ya shimo la choo huko maeneo ya Kimara King’ongo jijini. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye, amesema kuwa, mtoto huyo alitupwa juzi chooni majira ya saa 12 asubuhi, huko Kimara King'ongo na mtu asiyefahamika.Amesema choo hicho kipo nje ya nyumba ya Justina Lema na kichanga hicho alikutwa ameviringishwa matambara ndani ya choo hicho.Amesema kuwa mtoto huyo aliokolewa na wananchi wa eneo hilo baada mmiliki wa choo hicho kutoa taarifa kwa majirani kuwa anasikia sauti ya kichanga inatoka kwenye tundu hilo.Mtoto huyo ameokolewa akiwa hai na amehifadhiwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili na hali yake inaendelea vizuri.Kamanda huyo alisema juhudi za kumtafuta na kumsaka mtuhumiwa zinaendelea kwa kasi ili kumkamata ili aweze kufikishwa mahakamani
Binti wa Miaka 11 ajifungua Siku ya Harusi Yake

Subscribe to:
Posts (Atom)
VJN Super Motors
Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote