Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, November 27, 2009

Daznundaz kurudi tena?

Kama unalikumbuka ni kundi lililowahi kutamba sana miaka ya 90 ambalo lilikuwa likiundwa na wasanii nyota wa muziki wa kizazi kipya wawili Ferouz na Daz Baba ambao ndio walichangia kwa kiasi kikubwa kundi hilo kujipatia umaarufu wametangaza rasmi kumaliza tofauti zao. wakizungumza kwa pamoja na mtandao mmoja wa habari , wasanii hao walidai kuwa kwa sasa wako tayari kufanya kazi pamoja na hata kulirejesha upya kundi lao la Daznundaz. “Unajua tofauti zetu zilikuwa ndogo tu, ingawa vyombo vya habari vilichangia sana kuzikuza,hivi sasa tuko pamoja na mimi niko tayari kufanyakazi na mshkaji Daz Baba,” alieleza Ferouz, ambaye anaonekana kufulia kinoma kimuziki na kimaisha tofauti na alipokuwa na kundi la Daz nundaz. “Mimi na msanii mwenzangu Larumba ambaye tulikuwa pamoja tulianzisha kundi letu la Tanzaniano , lakini hili halituzuii kukaa pamoja na Ferouz na washkaji wetu wengine ili kulirejesha kundi letu la Daznundaz. Ferouz ni mtu wangu na niko tayari kufanya naye kazi,” alisema Daz Mwalimu . Kundi la Daznundaz lilisambaratika siku chache baada ya baadhi ya wasanii wake wakiongozwa na Ferouz kumtimua kundini msanii mwenzao Dazbaba kwa madai kuwa alikuwa akitumia dawa za kulevya ‘teja.’

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote