Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, November 27, 2009

Hongera Babu Sikare

Save Albino Benefit Concert ilioandaliwa na Babu Sikare anayekwenda kwa jina la Albino Fulani ambaye ni msanii, muigizaji na CEO wa Afrobino.Inc. ( http://www.afrobino.org/) iliyofanyika huko Columbus, Ohio, ilifana kupita kiasi ambapo watu wengi walijitokeza kutumbuizwa na wasanii mbalimbali kutoka Tanzania, Kenya na Zambia. Akiongea na mtandao mmoja wa habari, bwana Sikare alitoa shukurani za dhati kwa wote waliohudhuria na kutoa ushirikiano wa hali juu kufanikisha shughuli hiyo. Aliongeza kuwa imefika wakati kwa wasanii kutumia vipaji vyao kusaidia kwa namna moja ama nyingine watu wanaohitaji misaada katika jamii. Alitoa shukurani za dhati pia kwa kampuni ya Walgreens Pharmacy ya Marekani ambao walitoa bei poa ya mafuta ya kinga ya jua kwa watoto wenye ualbino yaliyonunuliwa. Mafuta hayo yatakwenda kusaidia watoto kuanzia miaka 5-10 na yatakabidhiwa kwa chama cha maalbino Tanzania hivi karibuni

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote