Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, November 23, 2009

Shoga aliyeleta Kizaazaa Italia Achomwa Moto na Kufa

Shoga wa kibrazili aliyesababisha maafisa wanne wa polisi nchini Italia kutiwa mbaroni na gavana wa mji wa Lazio kujiuzulu amefariki kwa kuchomwa moto ndani ya nyumba yake. Shoga raia wa Brazili mkazi wa Italia ambaye alihusika katika skendo la ngono la nchini Italia ambalo lilisababisha gavana wa jiji la Lazio kujiuzulu, amefariki kwa kuchomwa moto ndani ya nyumba yake katika mji wa Roma.Vyombo vya habari vya Italia, viliripoti kuwa chupa ya pombe kali aina ya whisky ilikutwa pembeni ya mwili wa shoga huyo aliyejulikana kwa jina la Brenda.Gavana wa Lazio, Piero Marrazzo, alijiuzulu nafasi yake mwezi uliopita baada ya video ya ngono akijivinjari na shoga huyo kuvuja kwenye vyombo vya habari.Mwanzoni mwa mwezi huu, Brenda aliwaita polisi na kutoa taarifa kuwa ameshambuliwa na kuporwa mali zake mtaani.Brenda na shoga mwingine wa kibrazili aliyejulikana kama Natalie walihusika kwenye skendo la ngono lililopelekea gavana Marrazzo ajiuzulu.Polisi wanne waliochukua video kwa siri wakati gavana huyo akijivinjari na mashoga hao, walijaribu kujipatia pesa toka kwa gavana huyo kwa kutishia kuiweka hadharani video hiyo lakini walikamatwa na kutiwa mbaroni.Gavana Marrazzo alijiuzulu huku akikiri kuwa na uhusiano na mashoga wanaofanya uhakaba.Mwanasheria wa gavana huyo amewataka polisi kumpa ulinzi shoga Natalie ili na yeye yasije yakamkuta kama yaliyomkuta rafiki yake.


No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote