Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, November 13, 2009

Mbwa wahitajika zoezi la kutafuta Miili ya waliopoteza maisha Same

BAADA ya zoezi la kukamilika kwa kuzikwa kwa miili 20 iliyopatikana kwa kufunikwa na mlima, Serikali imeombwa kupeleka mbwa wa kunusa ili kusaidia kutafuta maiti nyingine ambao hazijapatikana. Inadaiwa kuwa maiti nyingine zaidi ya tano bado hazijapatikana na zoezi hilo kuwa gumu kwa kuwa maiti hizo zilifunikwa na tope baada yam lima huo kuporomoka.Jumla ya nyumba saba zilifunikwa katika maporomoko hayo na watu wote waliokuwamo katika nyumba hizo usiku wa manane wa kuamkia juzi walikufa.Ombi la kuomba kikosi cha mbwa, lilitolewa jana na Halmashauri ya Wilaya ya Same kwa maelezo kwamba, juhudi pekee za wananchi hazitafanikiwa kupata miili iliyosalia bila kuopolewa. Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Monica Mbega, aliwataka wananchi kuwa waangalifu na kuchukua tahadhari kwa hali yoyote isiyokuwa ya kawaida katika eneo hilo na kuripoti maramoja.Katika tukio hilo walioopolewa kati yao kulikuwa na mama wajawazito wawili na miili ya vichanga hivyo vilitolewa tumboni mwa mama zao na kuzikwa tofauti, ambapo mama mmoja aliyefariki alishatimiza mimba ya miezi tisa.Maiti zilizotambuliwa na kuzikwa ni pamoja na Neema Shambi (70), Napenda Bakari (7), Namsemba Bakari (11), Sikudhani Elitabu (20), Nath John (12), Haika Charles (3) na Mariam Juma (4), Wemaeli Mhina (30), Ruth Mhina (6), Neema Bakari (8) na Christina Kiondo (32).Mingine ni Elitabu Shambi (30), Shambi Elineema (11), Ndimangwa Elineema (5), Amani Mhina (9), Kiondo Amani (37), Imani Kiondo (9) na Nikundiwe Kiondo (5), wote wakazi wa Goha.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote