Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, November 23, 2009

Sisi mabingwa watarajiwa Chalenji atamba Maximo

Kocha mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars, Marcio Maximo, amesema kwamba kikosi chake kitapambana kwa nguvu zote katika mashindano ya Chalenji kwa sababu timu yetu ni miongoni mwa mabingwa watarajiwa. Maximo alisema kati ya nchi 12 zinazoshiriki mashindano hao, ni nchi sita tu ndio zenye uwezo wa kuibuka mabingwa na kwamba wengine "ni wasindikizaji". Alizitaja nchi hizo kuwa ni pamoja na mabingwa watetezi, Uganda, Kilimanjaro Stars, Kenya, Rwanda, Zambia na Zimbabwe. Hata hivyo, Maximo ameonya kuwa Watanzania wasitarajie miujiza kwa sababu lolote linaweza kutokea katika soka. Maximo akiongea na vyombo vya habari juzi wakati timu yake ikiendelea na mazoezi kwa ajili ya michuano hiyo itakayoanza Jumamosi hii nchini Kenya, kwamba mashabiki na wadau watarajie matokeo mazuri lakini sio miujiza. Alisema kwamba matokeo mabaya katika mechi tatu za kirafiki za kimataifa walizocheza hivi karibuni, yameamsha morari kwa vijana wake ambao wameahidi kucheza kufa na kupona. "Kila mmoja anafahamu nini anatakiwa kukifanya, na nawajenga wajiamini kwamba wanaweza. Nafikiri, kama hatutamaliza mashindano tukiwa washindi wa tatu, basi tutafanya vizuri zaidi ya hapo," alisema Maximo.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote