Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, November 19, 2009

Dunia Imefika mwisho - Mchungaji Kortin Singida kwa kubaka

POLISI mkoani Singida linamshikilia Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) wa Usharika wa Igengu katika Dayosisi ya Kati, kwa tuhuma ya kumbaka msichana mwenye umri wa miaka 18 na kumtelekeza . Ilidaiwa msichana huyo (jina kapuni) alibakwa na mchungaji huyo na kusababishiwa maumivu makali katika sehemu zake za siri.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Celina Kaluba, alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Japhet Kidindima (37) mkazi wa wilayani Iramba mkoani humo.Kamanda Kaluba alisema kuwa tukio hilo lilitokea Jumatatu ya wiki hii, katika majira ya saa 9:45 alasiri, kwenye vichaka vilivyopo kati ya vijiji vya Igengu na Ibaga katika tarafa ya Kirumi, wilayani Iramba.Kamanda Kaluba alisema kuwa, mtuhumiwa huyo alifanikisha njama zake za ubakaji baada ya kumdanganya msichana huyo kuwa anataka kumtafutia kazi za ndani jijini Dar es Salaam.Kamanda alisema licha ya kumuahidi kumtafutia ajira, pia Mchungaji huyo alimuahidi msichana kuyo kumsafirisha hadi Dar es Salaam kwa ajili ya kwenda kufanya kazi hiyo.Alisema kuwa safari ya kwenda kijiji jirani cha Ibaga ilianza kwa miguu ambako ndipo ulipo usafiri wa basi, lakini walipofika katikati ya vijiji hivyo, Mchungaji Kidindima alimbaka msichana huyo kwenye vichaka.Alifafanua kuwa baada ya kumbaka, waliendelea na safari yao hadi kwenye kituo cha mabasi kilichopo kijiji cha Ibaga na hapo ndipo mtuhumiwa alifanikiwa kumtelekeza msichana huyo akiwa haelewi cha kufanya.Kamanda Kaluba alisema kuwa baadaye msichana huyo aliamua kuripoti tukio hilo katika kituo cha polisi kilichopo katika kijiji cha Ibaga kesho yake saa 7:30 mchana na jitihada za polisi kumsaka mtuhumiwa huyo zilianza.Alisema polisi walifanikiwa kumkamata Mchungaji Kidindima jana, majira ya saa tano asubuhi wakati akiwa masomoni kwenye chuo cha Biblia mjini Kiomboi.Hatua za awali zinachukuliwa ili mchungaji huyo aweze kufikishwa mahakamani kujibu tuhmu hizo za ubakaji na kutelekeza binti huyo vichakani.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote