Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, November 23, 2009

Aliyemuua Mkewe akiwa Usingizini aachiwa huru

Mwanaume mmoja wa nchini Uingereza ambaye alimyonga mkewe usingizini wakati alipoota ndoto anapigana na wezi, ameachiwa huru na mahakama. Brian Thomas, 59, aliota ndoto mwizi ameingia kwenye gari lao wakati alipokuwa amelala na mkewe usiku kwenye gari hilo, alimuua mkewe kwa kumkaba koo kwa nguvu akidhania anapigana na mwizi.Aliamka asubuhi na kugundua amemuua mke wake Christine Thomas na kuamua kuwapigia simu polisi ambapo alikamatwa na kupandishwa kizimbani kwa kosa la mauaji.Akitoa hukumu jaji wa kesi hiyo alisema kwamba Brian alikuwa mume mwaminifu na mwenye mapenzi ya kweli kwa mkewe na alikuwa hajijui wakati alipokuwa akifanya kitendo hicho.Mahakama iliambiwa kuwa hali aliyokuwa nayo Brian imewahi kuwatokea watu 50 tu dunia nzima.Brian alimnyonga mkewe usingizini mwezi julai mwaka jana wakati walipokuwa kwenye Mapumziko katika mji wa Aberporth, Wales.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote