Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, November 11, 2009

Msiba mzito Same

Watu ambao idadi yao haijafahamika inasemekana wamepoteza maisha katika tukio lililotokea usiku wa kuamkia leo katika jimbo linaloongozwa na Mheshimiwa Anne Kilango Malecela. Msiba huo umetokea baada ya mlima mmoja kumeguka na kufunika zaidi ya nyumba saba na inadaiwa watu wote waliokuwa wamelala ndani, wamepoteza maisha. Tukio hilo limetokea majira ya saa 7:00 usiku katika kata ya Miamba kitongoji cha Manka wilayani Same. Akizungumza na vyombo vya habari kwa njia ya simu leo asubuhi, Mbunge wa Same Mashariki, Mhe. Anne Kilango Malecela amesema chanzo cha maafa hayo ni mvua zilizonyesha mfululizo kwa siku tatu na kusababisha mlima kumeguka. "Mvua kubwa zimekuwa zikinyesha kwa siku tatu mfululizo, mbaya zaidi zinanyesha usiku tu, hali hiyo imesababisha udongo na miamba kumeguka na kufunika nyumba saba katika kitongoji cha Manka, huku watu wakiwa wamelala ndani, katika famila hizo hakuna aliyekwishaokolewa akiwa hai hadi sasa," amesema Mhe. Kilango. Kwa mujibu wa Mhe. Kilango hadi sasa miili kumi na moja imeshatolewa chini ya kifusi na juhudi zinaendelea. Hata hivyo amesema hali ya uokoaji nayo inakuwa ngumu kutokana na wapiga kura wake hao kuishi milimani ambako sio rahisi kufikika kirahisi na vyombo vya uokoaji. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Lucas Ng'oboko amethibitisha kutokea kwa maafa hayo lakini hakutoa taarifa zaidi kwa madai kuwa alikuwa njiani kuelekea eneo la tukio. "Hapa nilipo niko njiani kwenda eneo la tukio huko Same Mashariki, taarifa zaidi nitatoa baadaye baada ya kufika na kuona madhara yaliyotokea," amesema Kamanda Ng'oboko.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote