Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, November 26, 2009

Wafanyakazi Watano wa Kampuni moja wafariki dunia kwa mpigo

WAFANYAKAZI watano wa Kampuni ya ujenzi ya SICU ya jijini Dar es Salaam, wamefariki dunia na wengine 12 kujeruhiwa, baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kupinduka. Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Leonard Paul, alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea jana, majira ya saa moja usiku katika Kijiji cha Inokanoka, wilayani Ngorongoro na kulihusisha gari T 372 AFC Mitsubishi Canter. Kamanda Paul aliwataja waliokufa katika ajali hiyo kuwa ni Letuyo Lembeu (38), Ngidadiya Paluny (38), Oleyumbayiguti Pasani (36), John Mgawa (50) na Mesikongi Silelian (25), wote wakazi wa Ngorongoro. Aidha, waliojeruhiwa na kulazwa katika hospitali ya wilaya ni pamoja na Ezekiel Habali (27), Brayson Bake (26) na Azizi Hassan (27). Alieleza kuwa chanzo cha ajali hiyo kilitokana na ubovu wa barabara, hatua ambayo ilisababisha dereva wa gari hilo kushindwa kulimudu na kuacha njia kabla ya kupinduka. Polisi wanamshikilia dereva wa gari hilo, Huchen Weni (28), ambaye ni raia wa China kwa uchunguzi zaidi. Kamanda Paulo alifafanua kuwa gari hilo ni mali ya Kampuni ya ujenzi ya SICU ya jijini Dar es Salaam na lilikuwa linatoka Campu likiwa limebeba wafanyakazi 17 wa kampuni hiyo kuelekea eneo la Sopa na lilipofika kwenye kona liliacha njia na kupinduka.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote