Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, November 11, 2009

Akata nyeti za baba yake wa kambo na kuzichoma moto

Brigitte Harris ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 29, alikuwa akinyanyaswa kijinsia na kubakwa na baba yake wa kambo Eric Goodridge tangia alipokuwa na umri wa miaka mitatu.Kwa kuhofia ataendeleza tabia yake hiyo kwa mabinamu zake wadogo na akiwa na dhamira ya kulipa kisasi, alimpiga kwa kitu kizito kichwani baba yake huyo wa kambo aliyekuwa na umri wa miaka 55 na kupelekea apoteze fahamu.Brigitte alimshindilia taulo mdomoni na kisha kuukata uume wake kwa kutumia kisu kikali na kukinyofoa kabisa kipande kikubwa cha uume wake.Ili kuhakikisha madaktari hawataweza kukiunga tena kipande hicho cha uume wake alichokinyofoa, alikiweka kwenye jiko na kukichoma moto.Baada ya kuhakikisha kimeteketea kwa moto, alipiga simu hospitali kuita ambulansi lakini mpaka watu wa ambulansi walipofika, Goodridge alikuwa ameishafariki kwa kukosa pumzi.Brigitte mkazi wa New York, alishikiliwa na polisi tangia alipofanya mauaji hayo mwaka 2007.Akitoa hukumu ya kesi hiyo, jaji Arthur J Cooperman alimhukumu Brigitte kwenda jela kwa mauaji aliyofanya ingawa baadhi ya watetezi wake walikuwa na imani angeachiwa huru.Jaji Arthur aliagiza Brigitte atumikie kifungo kisichopungua miaka mitano na kisichozidi miaka 15.Brigitte amepanga kukata rufaa.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote