Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, November 24, 2009

Yanga yamtosa Ambani

Mabingwa watetezi Yanga hatimaye jana walitangaza rasmi kumtema mfungaji bora wa Ligi Kuu wa msimu uliopita, Boniface Ambani, na kuhitimisha uvumi uliotawala vyombo vya habari kwa muda mrefu kwamba mshambuliaji huyo kutoka Kenya hana nafasi tena kwenye kikosi cha kocha Mserbia Kostadin Papic. Mshambuliaji huyo ambaye alisajiliwa na Yanga msimu uliopita akitokea nchini India alikokuwa akicheza soka la kulipwa na kuisaidia Yanga kutwaa ubingwa wake wa pili mfululizo baada ya kuifungia mabao 18, hajafunga goli hata moja msimu huu hadi wakati timu zikienda mapumziko baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Afisa Habari wa klabu hiyo, Louis Sendeu alisema kuwa mchezaji huyo ameachwa kwa sababu ya kushuka kwa kiwango chake cha uchezaji. Mbali ya Ambani aliyebakiza muda wa miezi sita wa katika mkataba wake wa kuitumikia timu hiyo, wachezaji wengine walioachwa kwa sababu za kushuka kwa viwango vyao huku bado wakiwa na mkataba na Jangwani ni beki mrefu kutoka Kenya Joseph Shikokoti, beki wa kati Hamis Yusuph na Vincent Barnabas aliyeuzwa kwa mkopo kwenye timu ya African Lyon.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote