Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, November 24, 2009

Apata Mimba baada ya kufunga kizazi

Mama mmoja anayejulikana kwa jina la Debbie Amos mwenye umri wa miaka 43, mama wa watoto watatu, alifunga kizazi kwa kufanya upasuaji wa kuikata mirija ya kupitisha mayai na kisha kuikunja ili kumfanya asipate mimba tena.Miezi mitatu iliyopita, alishangaa kuona mabadiliko ya tumbo lake na alipofanyiwa uchunguzi aligundulika kuwa na mimba ya miezi sita.Wiki iliyopita ikiwa ni miaka 13 tangia alipofunga kizazi, Debbie alifanikiwa kujifungua salama mtoto wa kike aliyekuwa na uzito wa kilo 3.9."Sikuamini macho yangu, vipimo vilipoonyesha nina mimba, nilikaa chini kwa lisaa limoja nikiwa siamini, bado siamini mpaka sasa".Debbie na mumewe Melvyn mwenye umri wa miaka 57, walikuwa na matatizo ya kupata mtoto baada ya kufunga ndoa.Debbie alianza kutumia madawa ya kusaidia kupata mimba yanayoitwa Clomid wakati huo akiwa na umri wa miaka 19 na madawa hayo yalimsaidia kupata ujauzito wa mtoto wake wa kwanza ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 24.Aliendelea kutumia madawa hayo kwa miaka miwili zaidi na kufanikiwa kupata ujauzito wa mtoto wao wa pili wa kiume ambaye sasa ana umri wa miaka 19.Baada ya hapo waliamua kuwa watoto walionao wanatosha na Debbie aliacha kutumia madawa hayo lakini walishangazwa alipopata ujauzito wa mtoto wa tatu wa kike ambaye sasa ana umri wa miaka 16.Kwa kuhofia kupata watoto zaidi Debbie aliamua kufunga kizazi kwa operesheni ambayo ilifanyika kwenye hospitali kuu ya mji wa Colchester.Miaka 13 ikiwa imepita tangia alipofunga kizazi Debbie na mumewe walishangazwa kugundua kuwa wanatarajia mtoto wa nne."Mirija yangu yote miwili ya mayai ya uzazi ilikatwa na kukunjwa kwa hiyo ilikuwa ni vigumu sana kupata tena mimba", alisema Debbie."Na kwa umri wangu huu nilio nao ilikuwa vigumu zaidi kupata mimba tena".Madaktari walimwambia Debbie kuwa mirija yake ya mayai (fallopian tube) ilijiunda yenyewe tena baada ya kukatwa na hivyo kumfanya apate mimba tena.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote