Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, November 23, 2009

Mtoto wa ajabu azaliwa - LINDI

Mkazi mmoja wa Mtaa wa Rupiani katika Halmashauri ya Mji wa Lindi na ambaye hufahamika kwa jina la Salima Ally, 38, amejifungua mtoto wa ajabu na kuzua gumzo la aina yake kwa madokta na wauguzi wa Hospitali ya Mkoa wa Lindi. Mtoto huyo ambaye ni wa kike, amekuwa gumzo kwani licha ya kuzaliwa na afya njema na uzito wake wa kilo 3.2, imebainika kuwa hana macho wala pua. Aidha, mtoto huyo ana mdomo wenye mpasuko mkubwa kiasi cha kumfanya ashindwe kunyonya mwenyewe, huku kwenye paji la uso akiwa na uvimbe usio wa kawaida. Mtoto huyo alizaliwa jana, mishale ya saa 11:30 asubuhi katika hospitali hiyo ya mkoa wa Lindi iitwayo Sokoine. Akizungumza na mwandishi wa habari hii hospitalini hapo, Afisa Muuguzi wa zamu katika wodi hiyo ya wazazi namba nne aitwaye Bi. Zuhura Namkovera, amesema mtoto huyo alizaliwa salama lakini kinachosikitisha ni kwamba hadi sasa, maumbile yake ya ajabu yamemfanya aishi kwa shida mno. “Tangu azaliwe, mtoto huyu tumekuwa tukimnywesha maji, tena huwa anakunywa kwa shida sana kutokana na maumbile ya mdomo wake, ” amesema muuguzi huyo. Akieleza zaidi, Muuguzi huyo akasema kuwa huo ni uzazi wa sita wa mama huyo kwa mume aliyenaye. "Maendeleo ya afya ya mama (Bi. Salma) yanaendelea vizuri… na mtoto wake pia anaendelea vizuri, licha ya kwamba hajaanza kunyonya mwenyewe maziwa ya mama yake,” akasema Bi. Zuhura . Naye mganga aliyekuwa zamu katika hospitali hiyo, Dokta Jumanne Shija, amesema kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha hali hiyo, ikiwa ni pamoja na mama kuwahi kuathiriwa na magonjwa mbalimbali. “Ila mambo mengine yanakuwa ni maumbile tu… ni baada ya baadhi ya vichocheo vya mwili kushindwa kufanya kazi yake,” akasema Dk. Shija.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote