Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, November 16, 2009

FIFA yamfungia Maradona Miezi miwili

Kocha wa Argentina Diego Maradona amepigwa marufuku kujishughulisha na shughuli zozote zinazohusiana na masuala ya soka kwa kipindi cha miezi miwili. Diego Maradona amepigwa faini ya faranga 25,000 za Uswizi (Takribani Tsh. Milioni 30) na kutakiwa akae mbali na shughuli za soka kwa miezi miwili kutokana na maneno yake ya kashfa aliyoyatoa kwa waandishi wa habari waliokuwa wakimkosoa kufanya vibaya kwa timu ya taifa ya Argentina kwenye michuano ya awali ya kuwania nafasi ya kushiriki kombe la dunia mwakani nchini Afrika Kusini.Hata hivyo Argentina ilifanikiwa kupata nafasi ya kuja barani Afrika mwakani baada ya kushinda mechi yao ya mwisho katika kundi la Amerika kusini.Hukumu hiyo ya Fifa ilitolewa mjini Zurich Uswizi na Fifa ilisema kuwa adhabu hiyo ya Maradona inaanzia novemba 15 mwaka huu hadi januari 15 mwaka 2010.Kutokana na adhabu hiyo Maradona atazikosa sherehe za mwezi januari mwakani ambapo makundi ya kombe la dunia yatapangwa.Maradona aliwasili Zurich kusikiliza kesi yake hiyo akitokea nchini Hispania ambako Argentina ilibamizwa na Hispania mabao 2-1 siku ya jumamosi.Maradona aliondoka kwenye kikao hicho cha FIFA bila kuzungumza na vyombo vya habari lakini aliomba radhi wakati wa kusikilizwa kwa kesi yake kwa kitendo chake cha kuwatukana waandishi wa habari.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote