Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, November 26, 2009

Hali ya Mjamzito aliyekataliwa Hospitali ya Mwananyamala bado ni tata

HALI ya mwanamke mjamzito ambaye kiumbe chake kimefia tumboni tangu wiki iliyopita, bado ni tete, huku ndugu zake wakijitahidi kutafuta tiba ili kunusuru maisha yake. Akizungumza na Tanzania Daima nyumbani kwao Mwananyamala A, dada mkubwa wa mgonjwa huyo ambaye hakuwa tayari kutaja jina lake kwa kuogopa kuendelea kukosa ushirikiano kutoka Hospitali ya Mwananyamala, alisema hali ya ndugu yao si nzuri. “Kusema kweli ndugu yetu bado hali yake si nzuri, maana hata hii (leo) jana tumerudi tena Hospitali ya Mwananyamala lakini hakuna tiba tuliyopata,” alieleza. Aliongeza kuwa hata jana walipokwenda na kumtafuta daktari wa wasaidia, aliwaeleza kuwa wasubiri muda wa wiki mbili waliopangiwa awali. Alisema kutokana na majibu hayo, waliamua kurudi nyumbani na mgonjwa huyo huku wakijaribu kuwasiliana na ndugu wengine, ili kutafuta fedha kwa ajili ya kumpeleka katika hospitali binafsi. “Kwa sasa hatuna njia nyingine, kwa muda huu tunajaribu kukusanyana na kufanya kikao ili tumpeleke katika hospitali binafsi, kwani hatuwezi kukaa kwa wiki mbili, kwani hali yake ni mbaya,” alisisitiza.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote