Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, November 13, 2009

Tyson Matatani kwa kumpiga Mpiga Picha ngumi ya uso na kumpasua

Polisi nchini Marekani wamesema kuwa bingwa wa zamani wa ndondi za uzito wa juu, Mike Tyson na mpiga picha mmoja wamefunguliana mashtaka kila mmoja baada ya ugomvi uliozuka kwenye uwanja wa ndege wa Los Angeles International Airport.Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana, Mike Tyson alikuwa safarini kuelekea Las Vegas kwa kupitia uwanja wa ndege huo akiwa pamoja na binti yake mwenye umri wa miezi 10 na mkewe wakati tukio hilo lilipotokea.Taarifa zinasema kuwa Tyson na paparazzi huyo walirushiana ngumi lakini alikuwa ni Mike Tyson aliyempachika ngumi moja mpiga picha huyo iliyompeleka moja kwa moja chini na kumpasua sehemu ya juu ya uso wake.Mpiga picha huyo alipelekwa hospitali kupatiwa matibabu kwa majeraha aliyopata kufuatia kipigo alichokitafuta mwenyewe kwa kumghasi mbabe huyo wa zamani wa uzito wa juu.Alishonwa nyuzi tano katika sehemu yake ya juu ya uso wake iliyopasuliwa kwa ngumi nzito ya Tyson.Mike Tyson alikamatwa baada ya tukio hilo na kutupwa selo kwa muda kabla ya kuachiliwa kwa dhamana ya dola 20,000.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote