Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, November 13, 2009

Mtandao wa wezi wa Magari wakamatwa Dar

MTANDAO mkubwa wa wezi wa magari uliokuwa ukiongozwa na mwanamke mwenye asili ya Mnyarwanda umekamatwa.Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Suleiman Kova, amesema, mtandao huo ulinaswa na polisi wanaoendesha msako mkali kuwasaka wahalifu hao kote nchini.Amesema mtandao huo ulikuwa ukiongozwa na mwanamke Meritha Mwanahawa (20), ambaye katika kumbukumbu zake imeonesha kuwa ni bingwa wa kuwalaghai wanaume kimapenzi ambapo huenda kufanya nao mapenzi kisha kuwanywesha dawa za kulevya na kuwaibia funguo na kutoweka na magari yao.Amesema kuwa kumbukumbu za magari mengi yaliyoibwa zimeonyesha kuwa msichana huyo alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na baadhi ya madereva hao ambaod wealikiri wenyewe.Wengine walionaswa katika mtandao huo ni pamoja na Hamis Fumu (37), Arafat Juma (34), Samwel Mwamba (19), Yasmin Chuchu (20), Antipasi Kilawe (28) na Elias Moses (35).Kamanda Kova amesema kuwa jeshi lake bado linaendelea na msako mkali na litawafikisha mahakamani watuhumiwa baada ya upelelezi kukamilika.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote