Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, November 27, 2009

Je ni haki Kampuni ya Famili ya Kingunge (Smart Holdings) kupewa Tenda ya kukusanya Mapato Machinga Complex baada ya kuharibu Ubungo Stand?

Vyama vya wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga) kwa kushirikiana na Muungano wa Masoko ya Mkoa wa Dar es Salaam (Mumada), vimeandaa mkutano mkubwa, kujadili pamoja na mambo mengine, uhalali wa kampuni inayomilikiwa na familia ya Mbunge wa Kuteuliwa, Kingunge Ngombale-Mwiru. Familia hiyo imepewa zabuni ya kukusanya mapato katika jengo la Machinga Complex, huku ikiwa imefanya vibaya katika kazi hiyo katika Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT). Vyama vilivyoandaa mkutano huo utakaofanyika wiki ijayo kwa kushirikiana na Mumada, ni pamoja na Asbo, Tamada, Vibindo pamoja na Umoja wa Wafanyabiashara Walemavu Mkoa wa Dar es Salaam (Uwawada). Katibu wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano huo, David Nyendo, alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa tayari wameshaunda kamati ya watu sita, ambayo ina mwakilishi kutoka katika kila chama kwa ajili ya kuratibu mkutano huo. Nyendo alisema mkutano huo utafanyika Desemba 5, mwaka huu, katika ukumbi wa Al-Muntazir (zamani Korea) na kwamba, wanatarajia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi, kuwa mgeni rasmi. “Barua ameshapelekewa. Tulifika Ofisini kwake (Mkuu wa Mkoa), tukamkabidhi Msaidizi wake. Hivyo tunatarajia atakuwa mgeni rasmi katika mkutano wetu,” alisema Nyendo alipozungumza na na chombo kimoja cha habari. Alisema mkutano huo unatarajia kujadili kuhusu maendeleo ya Machinga Complex na mikakati ya kusukuma mambo, ambayo wamachinga wanahisi kuwa yana maslahi nao katika uendeshaji wa jengo hilo lililoko Ilala. Ajenda nyingine ni zabuni ya kukusanya mapato katika jengo hilo, pamoja na uhalali wa kampuni ya Smart Holdings iliyopewa zabuni hiyo ya kukusanya mapato katika jengo hilo. “Tutahoji pia, kwa nini Jiji wameharakia kutangaza zabuni kabla hata jengo halijaisha,” alisema Nyendo. Wakati mkutano huo ukisubiriwa kwa hamu kubwa, habari tulizozipata jana kutoka kwa baadhi ya viongozi wa vyama hivyo, zinaeleza kuwa huenda mkutano huo ukapitisha azimio la kutotoa ushirikiano kwa kampuni hiyo, ikiwa ni pamoja na kugomea kuilipa chochote kwa lengo la kushinikiza zabuni waliyopewa Smart Holdings itangazwe upya. “Kama mtu kaharibu Ubungo hadi Waziri Mkuu akaagiza ukaguzi ufanyike, iweje apewe sehemu nyingine akaharibu?” alihoji kiongozi mmoja wa Asbo, ambaye hata hivyo, hakutaka jina lake liandikwe magazetini kwa maelezo kuwa si msemaji wa chama. Licha ya kampuni hiyo ya mwanasiasa mkongwe nchini kufanya vibaya katika kazi ya ukusanyaji mapato ya serikali katika Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT), kiongozi huyo alidai kuwa ushindi wa zabuni yake umegubikwa na utata. Alidai utata huo unatokana na moja ya makampuni yaliyoomba zabuni hiyo, kampuni ya Amma Consult Limited, kuibuka mshindi katika kinyang’anyiro cha kuwania zabuni hiyo, lakini ikanyang’anywa ushindi huo na zabuni hiyo kutolewa kwa Smart Holdings Limited katika mazingira ya kutatanisha. Kampuni nyingine iliyowania zabuni hiyo, lakini ikashindwa, ni Zing Company. “Aliyenyang’anywa ushindi ‘alitenda’ zaidi ya Sh. bilioni 1.2 na alionyesha uwezo wake na namna atakavyoweza kufanya kazi hiyo, lakini aliyepewa zabuni alitenda fedha kidogo,” alidai bila kufafanua. Aliongeza: “Kampuni ya Amma Consult Limited ndiyo iliyokuwa imeshinda mwanzo, lakini katika hali ya kushangaza afisa mmoja wa kitengo cha manunuzi cha Halmashauri ya Jiji akainyang’anya ushindi.” Alidai katika kutekeleza njama hizo, Bodi ya Usimamizi na Uendeshaji wa jengo hilo haikushirikishwa katika hatua yoyote ya mchakato wa kumpata mzabuni licha ya Mwenyekiti wake, ambaye pia ni Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan Zungu (CCM) kuagiza suala hilo. Badala yake, bodi iliishia tu kualikwa kwenye ufunguzi wa kinyang’anyiro cha zabuni.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote