Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, November 19, 2009

Sina mpango wa kugombea urais 2010 - Dr. Slaa

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willbrod Slaa, amevunja ukimya na kueleza kuwa hafikirii kugombea urais katika uchaguzi mkuu wa mwakani.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Dk Slaa ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Karatu, alisema "Ikulu si mahali pazuri kukimbilia na urais si mchezo wa kitoto." Alisema wakati alipojiundoa katika upadre na kujitumbukiza katika ulimwengu wa kawaida, aliahidi kuwatumikia wananchi wa Karatu na si kutafuta njia ya kuingia Ikulu, ambako alisema kuna matatizo mengi yanayoweza kumfanya mtu kukosa usingizi. Unajua Ikulu si lele mama, kunahitaji mtu mvumilivu hasa wananchi wake wanapohangaika na ugumu wa maisha ya kila siku, jambo ambalo linaweza kumfanya ashindwe kupata usingizi, kwa sababu ya mawazo,alisema Dk Slaa. Alisema kama mtu anataka kugombea nafasi hiyo anapaswa kukumbuka maneno ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kuwa mtu anayekimbilia Ikulu anapaswa kuogopwa kama ukoma. Alisema mtu wa aina hiyo mara nyingi anakusukumwa na maslahi binafsi kuliko maendeleo ya watu. Dk Slaa alisema maendeleo yanapatikana bila ya hata kuingia ikulu na kwamba la msingi ni viongozi kujipanga katika kupigania maendeleo ya wananchi. Alisema mkakati wake ni kuhakikisha kuwa wananchi wa Karatu wananufaika na uongozi wake kwa kuwatafutia maendeleo na kuwaondolea kero kama ya maji na kadhalika. Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na uvumi kwa Dk Slaa ana mpango wa kuwania kiti cha urais kupitia tiketi ya Chadema. Kwa mujibu wa habari hizo, Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, hana mpango wa kuwania tena nafasi hiyo na badala yake anakwenda kuwania ubunge katika Jimbo la Hai mkoani Kilimanjaro.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote