Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, November 5, 2009

Mbatia aibuka na kusema "Takukuru, Wabunge wote ni WAFISADI"

Mwenyekiti wa Chama cha NCCR -Mageuzi, James Mbatia, amesema malumbano kati ya Bunge na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) yanatokana na ufisadi uliopo pande zote mbili. Mbatia alisema tafsiri ya malumbano baina ya Takukuru na Bunge, inaonyesha kuwa pande zote mbili zinatafutana nani fisadi zaidi ya mwingine. Alisema hali hiyo imetokana na nchi kuwa na mfumo mbovu wa Katiba kwa miaka mingi ambao hauendani na mazingira ya sasa. Mbatia alisema Takukuru imekuwa haina meno ya kupambana kikamilifu dhidi ya mafisadi na walarushwa kwa sababu, inasubiri kupewa maagizo kutoka Ofisi ya Rais. Pia, Mbatia alisema kutokana na tatizo hilo Takukuru imekuwa ikifanya kazi zake bila meno ya kung'ata mafisadi na walarushwa. Aliongeza kuwa malumbano hayo ni ishara inayoelekeza nchi kutafuta suluhu endelevu ambayo ni urekebishaji Katiba.Alisema kwa upande wa bunge, baadhi ya wabunge wamekuwa wakitumia kifungu namba 3 cha mwaka 1998 cha Bunge kujikinga. "Kwa kuwa sheria wameitunga wao lazima wakubali kuwa pindi wanapotakiwa kuhojiwa mahali popote wafanye hivyo, Endapo hawatatekeleza taratibu walizojiwekea wenyewe huo ni ufisadi,” alisema

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote