Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, November 2, 2009

Kitoto kichanga chaopolewa kutoka kwenye tundu la choo kikiwa hai

MTOTO mchanga wa siku moja ameopolewa akiwa hai akiwa ametupwa ndani ya shimo la choo huko maeneo ya Kimara King’ongo jijini. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye, amesema kuwa, mtoto huyo alitupwa juzi chooni majira ya saa 12 asubuhi, huko Kimara King'ongo na mtu asiyefahamika.Amesema choo hicho kipo nje ya nyumba ya Justina Lema na kichanga hicho alikutwa ameviringishwa matambara ndani ya choo hicho.Amesema kuwa mtoto huyo aliokolewa na wananchi wa eneo hilo baada mmiliki wa choo hicho kutoa taarifa kwa majirani kuwa anasikia sauti ya kichanga inatoka kwenye tundu hilo.Mtoto huyo ameokolewa akiwa hai na amehifadhiwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili na hali yake inaendelea vizuri.Kamanda huyo alisema juhudi za kumtafuta na kumsaka mtuhumiwa zinaendelea kwa kasi ili kumkamata ili aweze kufikishwa mahakamani

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote