Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, November 23, 2009

Wananchi Newala wazuia Msafara wa Waziri Mkuu

MSAFARA wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ulisimamishwa njiani baada ya wakazi wa kijiji cha Mkunya wilayani Newala, Mtwara, kuziba njia wakiwa na mabango wakitaka waziri huyo asimame asiendelee na safari zake awasikilize kwa dakika kadhaa. Tukio hilo lilitokea Jumamosi majira ya mchana wakati Pinda akielekea kwenye bonde la mto Ruvuma kukagua kituo cha maji cha Mkunya na kupokea taarifa ya kilimo cha umwagiliaji kwenye bonde la mto Ruvuma katika ziara yake.Mara baada ya kufika njiani hapo msafara huo ulikuta njia imefungwa na wananchi wakwia wamekaa kando ya barabara, na hatimaye Waziri Mkuu aliteremka kutoka kwenye gari yake na kuwasikiliza wananchi hao.Katika mazungumzo yao wakazi hao walisema wana kero ya kutopata maji safi na salama, kutolipwa malipo ya korosho na kutopatiwa pembejeo za ruzuku lakini uongozi wa wilaya umekuwa ukiwapuuza na kuficha taarifa badala ya kuwasaidia.Walisema kwamba tatizo la uhaba wa maji katika eneo lao limedumu kwa zaidi ya miaka 15 jambo ambalo linawafanya watumie muda mwingi kusaka maji badala ya kuutumia muda huo kwenye kilimo.Kuhusu mfumo wa stakabadhi za mazao ghalani, wakazi hao walisema hawautaki kwa sababu hawalipwi fedha zote za Sh. 700 kwa kila kilo kama walivyoahidiwa.Pia waliiomba Serikali iwasaidie kuwapatia pembejeo na mbolea za ruzuku kwani bei ni kubwa na wengi wanashindwa kuzimudu.Waziri Mkuu Mizengo Pinda, aliwaahidi wakazi hao kuwa kabla hajaondoka, atakuwa amepata ufumbuzi wa matatizo hayo na kukutana na wahusika mara moja.Kuhusu mfumo wa stakabadhi za mazao ghalani, Waziri Mkuu alisema hauna tatizo ila una kasoro ambazo itabidi ziangaliwe upya na kumtaka Mkuu wa Mkoa huo, Kanali (mstaafu) Anatory Tarimo, kujipanga upya na kusambaza elimu ya mfumo huo kwa wakulima.Kuhusu pembejeo za ruzuku, Pinda alisema atahakikisha anafuatilia suala hilo ili katika mwaka wa fedha ujao, mikoa ya Lindi na Mtwara iingizwe katika programu hiyo.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote