Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, November 25, 2009

Utata wa Makusanyo ya mapato Kituo cha Ubungo - Jiji yaiumbua familia ya Kingunge

Makusanyo ya mapato katika Kituo Kikuu cha Mabasi cha Ubungo (UBT), yameongezeka maradufu, ikiwa ni wiki chache tangu mkataba wa kampuni binafsi inayomilikiwa na familia ya Mbunge wa Kuteuliwa, Kingunge Ngombale-Mwiru, kumalizika na kazi hiyo kukabidhiwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ilianza rasmi kusanya mapato kituoni hapo Novemba Mosi, mwaka huu baada ya kampuni hiyo ya familia ya Kingunge ya Smart Holdings, iliyokuwa imepewa zabuni hiyo kwa zaidi ya miaka mitano kumaliza mkataba wake mwishoni mwa mwezi uliopita. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Bakari Kingobi, alisema jana kuwa tangu Halmashauri ianze kazi hiyo, imekuwa ikikusanya mapato ya wastani wa Shilingi milioni nne kwa siku. Kingobi aliyasema hayo jana alipokuwa akitoa taarifa katika kikao cha Madiwani wa Jiji la Dar es Salaam. Kwa hesabu hiyo, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, kwa mwezi itakuwa ikikusanya Sh. milioni 120. Awali, kampuni ya Smart Holdings ililalamikiwa kuwa ilikuwa ikikusanya mapato makubwa katika kituo hicho, lakini ikiishia kuilipa serikali fedha kidogo Sh. milioni 1.5 tu kwa siku. Katika makusanyo hayo, kampuni hiyo ilikuwa ikiilipa serikali sh. milioni 46.5 kwa mwezi. Kutokana na hali hiyo, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alimuagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, kufanya ukaguzi wa hesabu za mapato katika kituo hicho na katika Shirika la Masoko ya Kariakoo, jijini Dar es Salaam na kisha kuwasilisha ripoti ofisini kwake. Pinda alitoa agizo hilo wakati akizungumza katika kikao cha majumuisho, baada ya ziara yake ya siku tatu, jijini Dar es Salaam, Machi 15, mwaka huu. Katika agizo lake, Pinda alisema bila kujali mmiliki halali wa kampuni hiyo, ukaguzi wa hesabu hizo unapaswa kufanyika kwa maslahi ya umma, kabla ya kuchukua hatua kwa mujibu wa mapendekezo yatakayotolewa na CAG. Katika ziara hiyo, Pinda alishangazwa na kushtushwa na utendaji mbovu wa uongozi wa UBT, mkataba uliofikiwa kati ya kituo hicho na kampuni hiyo na namna ilivyopatikana. Pinda alifikia hali hiyo, baada ya kupewa taarifa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji, Kingobi, kuhusu hali ya utendaji wa uongozi wa UBT, ukusanyaji wa mapato, mkataba wa mkandarasi na maendeleo ya kituo hicho. Katika taarifa yake, Meneja wa Kituo hicho, Fadhili Izumbe, alisema kwa mujibu wa mkataba, mkandarasi huyo huipa Halmashauri ya Jiji, Sh. milioni 1.5 kwa siku, taarifa iliyomshangaza Pinda na kumfanya ahoji: “Hata kama anakusanya Shilingi bilioni moja anatoa Sh. milioni 1.5? Na kwa nini mkataba utamke shilingi badala ya asilimia?”. Kwa siku mabasi zaidi 400 husafirisha abiria, teksi 100 na watu zaidi ya 2,000 huingia UBT. Pia, kuna maduka ya vinywaji (baa na grosari), maduka ya kawaida, hoteli, ‘vioski’, gereji, ambavyo vyote hulipa ada za viwango mbalimbali. Siku moja baada ya ziara hiyo ya Pinda, mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Smart Holdings, Hassan Khan, alisema viongozi wa Halmashauri ya Jiji waliokuwapo kwenye ziara hiyo, hawajui lo lote na ndio maana walishindwa kumueleza Waziri Mkuu ukweli kuhusu mkataba huo. Khan alisema katika mkataba huo, walikubaliana na Halmashauri ya Jiji kuwa wangekuwa wakiilipa asilimia 75 na kushangazwa kusema asilimia hiyo ni sawa na Sh. milioni 1.5. Alisema katika mkataba huo, pia walikubaliana wawe wanalipa kiasi hicho cha fedha kwa kila siku bila kujali hali ya mapato itakayokuwa na bila kujali pia kuwa siku za mwishoni mwa juma (wikiendi) na wakati madaraja yanapokatika, kampuni yao hupata hasara. Utouh alikabidhi ripoti ya UBT mjini Dodoma, Julai mwaka huu, wakati wa Mkutano wa 16 wa Bunge. Akijibu maswali ya papo kwa papo mwishoni mwa mwezi uliopita bungeni, Pinda alisema ripoti hiyo inapitiwa na Katibu Mkuu wa Tamisemi na yule wa Ofisi ya Waziri Mkuu na kuahidi kuwa itatolewa hadharani baada ya maofisa hao wa serikali kumaliza kazi ya kuipitia. Hata hivyo, kabla Pinda hajatoa kauli hiyo, wiki kadhaa zilizopita, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi, alidokeza kuwa serikali ingechukua kituo cha Ubungo kupitia Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam mwisho wa mwezi uliopita.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote