Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, November 10, 2009

Kuweni makini na Mapenzi ya kwenye Mtandao

Mwanaume mmoja wa nchini Uingereza amebatizwa jina la 'Speminator' baada ya kuwapachika ujauzito wanawake 12 aliofahamiana nao kwenye mtandao wa Facebook wawili kati yao aliwapachika mimba ndani ya usiku mmoja. Wanawake nchini Uingereza wanaotumia mtandao wa tovuti ya Facebook wameshauriwa kutofanya urafiki na Dominic Baronet, raia wa Uingereza mwenye umri wa miaka 26 ambaye ni hatari sana katika kuwalaghai na kuwapachika ujauzito wanawake anaofahamiana nao kupitia mtandao wa Facebook.Katika kuthibitisha kuwa Dominic ni hatari sana kwa kuwapachika mimba wanawake, aliwapachika mimba wanawake wawili ndani ya usiku mmoja na kulifanya gazeti la News of The World la Uingereza limbatize jina la "Sperminator".Dominic hutumia siku chache kufanikiwa kuwalaghai wanawake anaofahamiana nao kwenye Facebook na kisha kufanya nao mapenzi.Wanawake watano tayari wameishajifungua watoto wake, wanawake watano wengine wanafikiria kuzitoa mimba zao na wanawake wawili wanatarajia kujifungua watoto wake hivi karibuni.Miongoni mwa wanawake waliokumbana na zahama la Dominic ni Kerry Martin, 24, ambaye aligundua kuwa Dominic ana wapenzi wengi baada ya kutembelea ukurasa wake kwenye Facebook na kukutana na ujumbe wa Baronet akijipongeza kumpachika ujauzito mwanamke mwingine aliyejulikana kama Stacy Jones mwenye umri wa miaka 24.Kerry alipounda urafiki na Stacy aligundua kuwa wote wawili walipata ujauzito siku moja ndani ya usiku mmoja isipokuwa nyakati tofauti."Dominic inabidi apigwe marufuku kwenye Facebook, anatumia tovuti ya Facebook kuwalaghai wanawake na kuwapachika mimba na kisha kuwatelekeza bila ya kujali matokeo yake", Stacy aliliambia gazeti la News of the World.Stacy ameutaka uongozi wa Facebook umfute Dominic kwenye mtandao huo na umpige marufuku kujiunga tena.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote