Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, November 11, 2009

Ahudhuria mazishi yake

Jamaa mmoja nchini Brazili ambaye alisemekana kuwa amefariki kwenye ajali mbaya ya magari, aliwashtua familia yake na waombelezaji wakati alipojitokeza makaburini wakati mazishi yake yakiendelea. Ademir Jorge Goncalves mwenye umri wa miaka 59 alitangazwa amefariki baada ya ndugu zake kuitambua maiti yake katika ajali mbaya sana ya magari katika jimbo la Parana nchini Brazili, taarifa ya polisi ilisema.Kama zilivyo taratibu za kitamaduni, mazishi yake yalifanyika siku iliyofuatia siku ambayo pia ilikuwa ni siku wabrazili hutembelea makaburi yao kuwakumbuka ndugu zao.Kitu ambacho familia yake haikujua ni kuwa, Goncalves alitumia usiku mzima kwenye maegesho ya malori akinywa pombe ya miwa inayoitwa "Cachaca" akiwa pamoja na marafiki zake.Goncalves hakusikia chochote kuhusiana na habari za kifo chake na alikuja kugundua asubuhi wakati huo waombelezaji wakiwa wameishalibeba jeneza kwenda kuzika na wakiwa wameishafika makaburini.Ilimbidi awahi makaburini kuwafahamisha familia yake kuwa yeye hajafa bado yupo hai, alisema msemaji wa polisi katika mji wa Santo Antonio da Platina."Maiti ya mwanaume aliyefariki katika ajali hiyo ilikuwa imeharibika vibaya sana lakini alikuwa amevaa nguo kama za Goncalves na hivyo kuifanya familia yake kuamini ndio yeye", aliendelea kusema msemaji huyo wa polisi."Watu wanaogopa kuangalia maiti kwa muda mrefu wakati wa kuzitambua maiti za ndugu zao na ndio sababu hali kama hii imetokea".Binamu wa Goncalves alisema kwamba baadhi ya ndugu wa familia yake waliitilia shaka maiti hiyo kama ni ya Goncalves lakini baada ya ndugu wengi kusisitiza ni maiti yake, taratibu za mazishi ziliendelea.Mazishi hayo hayakuendelea tena na ilibidi warudi nyumbani na kuwapa taarifa polisi ambapo maiti hiyo ilitambuliwa baadae kuwa ni ya mwanaume mwingine na ilizikwa jumatatu katika jimbo jingine.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote