Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, November 19, 2009

Baba wa kijana Aliyedai Amebakwa na Michael Jackson Ajiua

Baba wa kijana Jordy Chandler ambaye alilipwa dola milioni 20 baada ya kudai Michael Jackson amembaka, amejiua mwenyewe kwa kujipiga risasi ya kichwa. Evan Chandler mwenye umri wa miaka 65 ambaye ni baba wa kijana Jordy Chandler ambaye alidai amebakwa na Michael Jackson, amejiua mwenyewe kwa kujipiga risasi.Evan na mwanae walilipwa dola milioni 20 na marehemu Michael Jackson ili kuimaliza kesi hiyo nje ya mahakama.Evan ambaye alikuwa ni daktari wa meno, alikutwa amefariki kwenye nyumba yake iliyopo New Jersey akiwa na jeraha la risasi kichwani mwake.Polisi walitoa taarifa baadae wakisema kuwa wanaamini Evans alijiua mwenyewe kwakuwa alikutwa akiwa ameishikilia bunduki ambayo aliitumia kujiua.Mwaka 1993, Evans alimfungulia mashtaka Michael Jackson kwa niaba ya mwanae ambaye wakati huo alikuwa na umri wa miaka 13.Evans alimtuhumu Michael Jackson kumbaka mwanae, na ilimbidi Michael Jackson atoe dola milioni 20 kuimaliza kesi hiyo nje ya mahakama.Pamoja na kukubali kutoa kiasi hicho cha fedha, Michael Jackson aliendelea kukanusha kufanya kitendo chochote kibaya kwa mtoto huyo.Baada ya kukabidhiwa pesa hizo, Evan na mwanae walifarakana na kila mtu alienda kuanza maisha yake kivyake kivyake.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote