Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, November 30, 2009

Adai kuiona sura ya YESU kwenye Pasi

Mwanamke mmoja nchini Marekani anayejulikana kwa jina la Mary Jo Coady mkazi wa Massachusetts nchini Marekani, ambaye ndoa yake na mumewe ilivunjika hivi karibuni na kufuatiwa na mkosi wa kupunguziwa masaa ya kufanya kazi kazini kwake, ametangaza kuiona sura ya Yesu kwenye pasi ya umeme na amedai ana uhakika maisha yake yatakuwa mazuri baada ya kuiona sura Yesu.Mary alidai kuigundua picha ya Yesu kwa mara ya kwanza siku ya jumapili iliyopita wakati alipoingia kwenye chumba cha mtoto wake.Uchafu uliotokana na kuungua kwa nguo kwenye pasi ulionekana kama sura ya mtu mwenye nywele ndefu.Mary mwenye umri wa miaka 44 pamoja na watoto wake wawili, walikubaliana kuwa sura inayoonekana kwenye pasi ni ya Yesu na wamba Yesu anawasikiliza.Mary ambaye alilewa katika mazingira ya kikatoliki aliliambia gazeti la The Eagle-Tribune kuwa mkasa wake wa kuiona sura ya Yesu utakuwa changamato kwa watu wengine wakati huu krismasi ikikaribia.Mary alisema kuwa ana mpango wa kuificha pasi hiyo kwenye kabati na atanunua pasi nyingine.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote