Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, November 30, 2009

Mapenzi kizunguzungu - Afukua maiti ya Mkewe na kulala nayo kwa miaka 5 mfululizo

Mwanaume mmoja wa nchini Vietnam ambaye alikuwa na huzuni ya kuondokewa na mkewe, alifukua kaburi la mkewe na kuichukua maiti ya mkewe na kuanza kulala nayo kitanda kimoja kwa kipindi cha miaka mitano. Le Van aligubikwa na huzuni kubwa wakati mkewe alipofariki mwaka 2003 kiasi cha kwamba alianza kulala juu ya kaburi lake katika mji wa Quang Nam uliopo ukanda wa kati wa Vietnam.Gazeti la Vietnamnet liliripoti kuwa Van aliendelea kulala juu ya kaburi la mkewe usiku kwa kipindi cha miezi 20 mpaka alipoanza kuugua kutokana na hali ya hewa ya baridi.Ili kujikinga na baridi, Van aliamua kutengeneza handaki lililoenda kwenye jeneza lake na kuanza kulala pembeni ya maiti yake.Watoto wa Van waliligundua handaki hilo na waliamua kumzuia Van kulitembelea kaburi la mkewe.Mwezi novemba mwaka 2004, Van alilifukua kaburi la mkewe na kuichukua maiti ya mkewe hadi nyumbani kwake.Van alitumia udongo mfinyazi kuizunguka mifupa ya maiti ya mkewe na kisha aliivalisha maiti hiyo nguo za kike na kisha kuipaka vipodozi.Van mwenye umri wa miaka 55, baba wa watoto saba, alianza kulala pembeni ya maiti ya mkewe akiikumbatia kuanzia wakati huo hadi leo.Picha zinazomuonesha Van akiwa pembeni ya maiti ya mkewe zilichapishwa kwenye gazeti la Vietnamnet, ikiwemo picha moja ambayo iliionyesha mifupa ya mkono wa mkewe ikiwa imezungushiwa udongo.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote