Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, November 11, 2009

Golikipa wa timu ya Taifa ya Ujerumani ajiua

Golikipa namba moja wa timu ya taifa ya Ujerumani na timu ya Hannover inayoshiriki ligi kuu ya Ujerumani Bundesliga, Robert Enke amefariki dunia jana jumanne baada ya kugongwa na treni wakati aliposimama kwenye reli mbele ya treni lililokuwa kwenye spidi ya kilomita 160 kwa saa.Enke aliyekuwa na umri wa miaka 32 alifariki kwenye eneo la tukio ambalo haliko mbali na nyumba yake.Madereva wawili wa treni lililomgonga walisema kwamba walishangaa kumuona mtu akiwa amesimama kwenye reli mbele yao wakati treni likiwa spidi, walijaribu kufunga breki bila mafanikio.Rais wa timu ya Hannover, Martin Kind alielezea kusikitishwa kwake na habari za kufariki kwa golikipa wa timu yake ambaye alikuwa akitegemewa kulilinda lango la Ujerumani kwenye fainali za kombe la dunia nchini Afrika Kusini mwakani.Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Ujerumani, Joachim Loew na meneja wa timu ya taifa Oliver Bierhoff walisema "Tumeshtushwa sana, hatuna la kusema".Mtoto wa kike wa Enke aliyekuwa na umri wa miaka miwili alifariki miaka miwili iliyopita na mwezi mei mwaka huu Enke na mkewe walijitolea kumchukua na kumlea mtoto wa kike mwenye umri wa miezi miwili.Enke alipewa jezi namba moja ya Ujerumani baada ya kipa mkongwe wa Ujerumani Jens Lehmann kustaafu baada ya kombe la Euro 2008.Enke, alizaliwa katika mji wa Jena na wakati wa uhai wake alizichezea timu za Borussia Moenchengladbach ya Ujerumani, Benfica ya Ureno, Barcelona ya Hispania, Fenerbahce ya Uturuki na Tenerife ya Hispania.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote