Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, November 5, 2009

Watu 4 wakamatwa na Meno ya Tembo Dar

JESHI la polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata watu wanne wakiwa na meno ya Tembo vipande 33 kinyume na sheria za nchi. Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, ASP Suleimani Kova aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa, nyara hizo zilikamatwa maeneo ya Mbagala Nzasa Wilayani Temeke wakijaribu kuzisafirisha nyara hizo nje ya nchi.Kamanda Kova alisema watu waliokamatwa walikutwa wakijiandaa kupeleka nje ya nchi nyara hizo wakati hawana nyaraka zozote za umiliki wa meno hayo.Alisema nyara hizo za serikali zina uzito wa kilo 102.9 zenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 7, na kwamba zilikamatwa baada ya polisi kupata taarifa kutoka kwa raia wema.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote