Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Tuesday, November 24, 2009

Walimu 22 wafukuzwa kwa Ulevi Singida

Walimu 22 katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida, wamesimamishwa kazi kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo ulevi na utoro kazini. Hayo yalibainishwa mwishoni mwa wiki na ofisa Elimu wa Wilaya ya Iramba, Leonard Ngaharo, kwenye mkutano wa viongozi uliofanyika katika kijiji cha Mwanga, Tarafa ya Nduguti. Mkutano huo uliitishwa na Mbunge wa Iramba Mashariki, Mgana Msindai. Ngaharo alisema walimu hao wamesimamishwa kazi katika kipindi cha miezi miwili iliyopita ikiwa ni mkakati wa wilaya hiyo kuhakikisha taaluma inayotolewa kwenye shule zake za msingi, inakuwa na ubora unaostahili. Alisema walimu hao wamesimamishwa kazi kutokana na makosa ya kukiuka mikataba ikiwemo ulevi na utoro kazini. Aidha, Ofisa Elimu huyo alisema ofisi yake itawahamisha walimu wote waliokaa kwenye kituo kimoja kwa muda mrefu ili kuleta ufanisi na upatikanaji elimu bora kwenye shule zake za msingi. Ngaharo alilazimika kutoa ufafanuzi huo kufuatia ombi la kiongozi wa serikali za mitaa kumwomba Msindai asaidie kuwahamisha walimu wa shule ya msingi waliotumika kwa miaka mingi kwenye Kata ya Mwanga. Kwa upande wake, Mbunge huyo aliwataka viongozi wa dini kufanya kazi kwa bidii na kujenga uhusiano mwema kati yao na waumini wanaowaongoza, huku akiiasa jamii kuheshimu mema yote wanayoelekezwa. “Naomba sana waongozeni waumini wenu kwa njia za haki, msikate tamaa na endeleeni kuwahimiza wafanye kazi zaidi, ikiwemo utoaji wa michango ya miradi mbalimbali ya maendeleo…ya Kaisari mpe Kaisari na ya Mungu mpe Mungu,” alifafanua Msindai. Mbunge huyo alikuwa kwenye ziara katika jimbo lake hususani Kata za Mwanga na Ilunda, ambapo aliwahimiza wananchi kushiriki kwenye miradi ya maendeleo na kutumia vizuri mvua zinazonyesha sasa ili washiriki fursa ya kilimo kwanza.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote