UGONJWA wa mshtakiwa Farijara Hussein umekwamisha kuendelea kusikilizwa kwa kesi ya wizi wa Sh 3.8 bilioni za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) inayomkabili yeye pamoja na wenzake watano na sasa kesi hiyo imepangwa kusikilizwa mwakani ili kutoa nafasi ya mtuhumiwa huyo kupata matibabu. Kesi hiyo ilishindwa kuendelea kusikilizwa jana mbele ya jopo la mahakimu watatu lililokuwa likiongozwa na Hakimu Samuel Kalua mara baada ya Wakili wa Serikali, Oswald Tibabyekomya kudai kuwa wapo tayari kwa ajili ya kuendelea kuisikiliza na kwamba wana mashahidi wawili. Baada ya maelezo hayo, Wakili Majura Magafu anayemtetea mshtakiwa Farijara, aliiomba mahakama iahirishe kesi hiyo kwa sababu mteja wake huyo anaumwa na amepewa muda wa mampuziko wa siku tatu (ED) kuanzia juzi, jana na leo. Magafu aliendelea kudai mbali na mapumziko hayo pia alitakiwa aonane na mtaalamu wa hospitali ya Burhan, Profesa Aboud. Kufuatia hoja hiyo hakimu Kalua alikubaliana na maombi hayo na kuiahirisha kesi hiyo hadi Novemba 11, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na si kuendelea kusikilizwa ambapo alisema kuwa Desemba 21, mwaka huu kesi hiyo itatajwa tena na kuongeza kuwa kuanzia Februari Mosi hadi 5, 2010 kesi hiyo ndio itaendelea kusikilizwa mfululizo. Awali Oktoba 27 mwaka huu, mahakama ililazimika kusimama kusikiliza ushahidi katika kesi hiyo baada ya mshtakiwa huyo kuomba kwenda haja ndogo mara kwa mara kutokana na kusumbuliwa na tatizo la figo. Mshtakiwa huyo aliomba kwenda haja ndogo mara kwa mara na kusababisha hakimu kuamua kumruhusu aondoke. Akitoa ushahidi wake Msajili Msaidizi kutoka ofisi ya Msajili wa Majina ya Biashara na Kampuni (Brela), Rehema Kitambi alidai kuwa mshtakiwa Farijara na mtu mwingine aliyemtaja kwa jina la Kiza Selemani walighushi jina la biashara la Mibale Farm lililotumika kuchota fedha hizo za EPA. Alidai kuwa hati zenye jina la Mibale Farm hazitambui kwasababu hazijatolewa na Brela na hata saini inayoonekana katika baadhi ya hati hizo imeghushiwa na kufanana na ya kwake. Shahidi huyo alidai kuwa Septemba 2 mwaka 2005 Farijara na Kiza waliomba kusajili jina la biashara la Nibale Farm na kwamba Septemba 5 mwaka 2005 walipeleka maombi mengine ya kubadili jina hilo ili liwe Mibale Farm. Washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Rajabu Maranda, Ajay Somani, Imani Mwaposya, Ester Komu na Sophia Kalika. Washtakiwa hao wanadaiwa kuiibia BoT Sh 3.8 bilioni baada ya kudanganya kuwa kampuni ya Mibale Farm imepewa deni na kampuni ya Lakshmi Textile Mills ya nchini India.
Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Friday, October 30, 2009
FIFA & TFF kuzindua Program ya kuimarisha SOKA

MAGUFULI kugawa samaki Bure
.jpg)
Wachezaji SIMBA waahidiwa Milioni 30/=
.jpg)
Aidha, alisema wachezaji wenzake wapo kwenye morali kubwa na wanaamini wataibuka na pointi tatu katika mchezo huo wa ligi kuu Tanzania bara. Alipoulizwa msemaji wa timu hiyo, Cliford Ndimbo juu ya ahadi hiyo alisema hana uhakika na suala hilo kwa kuwa hajapewa taarifa rasmi na uongozi wa juu wa klabu hiyo.
Babu wa Miaka 112 aoa Binti wa Miaka 17
Babu mwenye umri wa miaka 112 wa nchini Somalia ambaye ana jumla ya watoto 18 amefunga ndoa na binti mwenye umri wa miaka 17 katika sherehe kubwa iliyohudhuriwa na mamia ya watu nchini Somalia. Mamia ya watu walifurika kwenye harusi ya babu mwenye umri wa miaka 112 wakati alipokuwa akifunga ndoa na mwanamke ambaye amemzidi jumla ya miaka 95.Ahmed Muhamed Dore ambaye tayari ana watoto 18 kutokana na wake zake watano alisema kuwa anahitaji watoto zaidi kutoka kwa mkewe mpya Safia Abdulleh, ambaye ana umri wa miaka 17."Leo Mwenyezi Mungu amenitimizia ndoto yangu", alisema Ahmed baada ya harusi iliyohudhuriwa na mamia ya watu kwenye mji wa Galguduud.Familia ya bi harusi ilisema kwamba binti yao ana furaha sana kuolewa na Ahmed.Ahmed alisema kuwa mke wake ambaye kwa umri wake ni sawa na umri wa kitukuu chake wa kike, wanatoka kijiji kimoja.Ahmed alidai kwamba alimsubiria kwa miaka mingi sana Safia afikie umri wa kuolewa ili atimize ndoto yake ya kumuoa."Sikumlazimisha aolewe na mimi, nilitumia ujuzi na uzoefu wangu wa kuwavutia wanawake ili anikubali nimuoe na hatimaye alikubali nimuoe", alijisifia Ahmed.Ndoa hiyo imeelezewa na wanahistoria wa Somalia kuwa haijawahi kutokea nchini humo watu wakafunga ndoa wakiwa na tofauti ya umri miaka 95, miaka mitano tu pungufu ya karne moja.
Kenya kufanya sensa ya mashoga
Serikali ya Kenya iko mbioni kufanya sensa ya kuwahesabu mashoga waliopo nchini humo katika jitihada zake za kuwaelimisha watu juu ya ugonjwa wa ukimwi.
Serikali ya Kenya inajiandaa kuwahesabu mashoga waliopo nchini humo ingawa kwa sheria za Kenya mashoga huadhibiwa kwenda jela miaka 14 wanapokamatwa.Nicholas Muraguri, mkuu wa taasisi ya kuzuia kuenea kwa ukimwi ya Nascop, akiongea na shirika la habari la BBC alisema kuwa kuna umuhimu mkubwa serikali ya Kenya kufanya takwimu ya mashoga nchini humo.Alisema kuwa mashoga wengi hawana elimu kuhusiana na ugonjwa wa ukimwi.Hata hivyo wachambuzi wa mambo wanahofia kuwa mashoga wengi watahofia kujitokeza kuhesabiwa kwa kuhofia kukamatwa na kutupwa jela.Muraguri alisema kwamba takwimu hiyo itahusisha pia mashoga kutajana wenyewe kwa wenyewe huku maafisa wengine wakiwapima kama wameambukizwa virusi vya ukimwi pamoja na kuwafundisha njia salama za mapenzi."Wakenya hawawezi kusema kuwa mashoga ni jamii iliyotengwa, ni miongoni mwa jamii zetu", alisema Muraguri."Kundi hili inabidi lifikiwe na lipewe mafunzo ya jinsi ya kujilinda wasiambukizwe", alisema.Sensa hiyo ya mashoga imewagawanya Wakenya wengi huku baadhi yao wakisema hawaamini kama itasaidia chochote katika kuzuia kuenea kwa ukimwi.Baadhi ya mashoga waliohojiwa na BBC walitanabaisha kuwa wako tayari kuhesabiwa iwapo sensa hiyo itafanyika kwa siri.
Serikali ya Kenya inajiandaa kuwahesabu mashoga waliopo nchini humo ingawa kwa sheria za Kenya mashoga huadhibiwa kwenda jela miaka 14 wanapokamatwa.Nicholas Muraguri, mkuu wa taasisi ya kuzuia kuenea kwa ukimwi ya Nascop, akiongea na shirika la habari la BBC alisema kuwa kuna umuhimu mkubwa serikali ya Kenya kufanya takwimu ya mashoga nchini humo.Alisema kuwa mashoga wengi hawana elimu kuhusiana na ugonjwa wa ukimwi.Hata hivyo wachambuzi wa mambo wanahofia kuwa mashoga wengi watahofia kujitokeza kuhesabiwa kwa kuhofia kukamatwa na kutupwa jela.Muraguri alisema kwamba takwimu hiyo itahusisha pia mashoga kutajana wenyewe kwa wenyewe huku maafisa wengine wakiwapima kama wameambukizwa virusi vya ukimwi pamoja na kuwafundisha njia salama za mapenzi."Wakenya hawawezi kusema kuwa mashoga ni jamii iliyotengwa, ni miongoni mwa jamii zetu", alisema Muraguri."Kundi hili inabidi lifikiwe na lipewe mafunzo ya jinsi ya kujilinda wasiambukizwe", alisema.Sensa hiyo ya mashoga imewagawanya Wakenya wengi huku baadhi yao wakisema hawaamini kama itasaidia chochote katika kuzuia kuenea kwa ukimwi.Baadhi ya mashoga waliohojiwa na BBC walitanabaisha kuwa wako tayari kuhesabiwa iwapo sensa hiyo itafanyika kwa siri.
Habari Njema Kwa Matasa

Thursday, October 29, 2009
Awekwa chini ya Ulinzi kwa kuongopa kaibiwa mtoto
MWANAMKE anayejulikana kwa jina la Maua Ally (29) amejikuta anashikiliwa na polisi baada ya kupiga mayowe ya uongo akilalamika kuwa mtoto wake aliyemzaa katika Hospitali ya Temeke ameibwa na watu wasiofahamika. Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Temeke, Liberatus Sabasi amesema, Jeshi la Polisi lilipokea taarifa kutoka kwa Muuguzi Mkuu wa Hospitali hiyo Nusura Simba (49), kuwa kuna mwanamke analalamika kuwa ameibiwa mtoto wake.Kamanda alisema kuwa kwa mujibu wa maelezo ya mwanamke huyo alidai kuwa, alifika katika hospitali hiyo akiwa anaumwa uchungu wa kujifungua na alipofika hapo alipokelewa na daktari kisha kupelekwa chumba cha kuzalisha [labour wodi], ambapo alifanikiwa kujifungua mtoto wa kiume.Mwanamke huyo alidai kuwa cha kushangaza baada ya kutoka chumba hicho hakumuona mtoto wake na ndipo alipoamua kutoa taarifa kwa uongozi wa hospitali hiyo.Baada ya jeshi la polisi kupokea taarifa hizo kutoka kwa uongozi wa hospitali hiyo, walifika hospitalini hapo na kumhoji mwanamke huyo chini ya ulinzi wa polisi na katika kumuoji kwa kutumia mbinu za kipolisi mwanamke huyo alikiri hakujifungua wala hakuwahi kuwa mjamzito na alifika hospitalini hapo kwa kuwa alikuwa na shida ya mtoto.Alidai kuwa aliamua kufanya hivyo na kutoa taarifa za uongo kwa sababu mume wake amekuwa akimshinikiza kubeba mamba na kutaka mtoto kwa muda mrefu na alimuongopea mume wake huyo alikuwa mjamzito.Ndipo alipoamua kufanya mbinu hiyo ili mume wake huyo ajue ni kweli alijifungua na mtoto wake aliibiwa na manesi na kuomba samahani kwa mapolisi hao na kwa uongozi wa hospitali hiyo kwa kitendo alichokifanya cha kudanganya.Kamanda Sabasi amesema kutokana na taarifa hizo, uchunguzi wa kitaalamu ulifanyika dhidi ya mwanamke huyo na walibaini kuwa mwanamke huyo hakujifungua na hakuwa na dalili hata ya kuwa na mimba. Kamanda Sabasi amesema kuwa, mtuhumiwa huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote baada ya upelelezi kukamilika kujibu shtaka hilo kwa kuuongopea umma.
Mechi ya Simba na Yanga Viingilio hivi hapa

Mchezo huo unaosubiriwa na mashabiki wengi unatarajia kufanyika Jumamosi katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo mwamuzi wa pambano hilo atakuwa Oden Mbaga.Katibu mkuu wa TFF, Fredrick Mwakalebela alisema jana kuwa tiketi kwa ajili ya mchezo huo zitaanza kuuzwa leo katika vituo mbalimbali jijini Dar es Salaam ili kuondoa msongamano siku ya pambano hilo na kusema siku hiyo tiketi hazitauzwa.Kuhus mpangilio wa viti, Mwakalebela alisema viti vya kijani mzunguko, kiingilio kitakuwa 5,000,viti vya kijani mzunguko 7,000, orange 10,000, orange VIP 20,000, VIP C, 30,000, VIP B 50,000 na VIP A 60,000.Mbali na viingilio hivyo, Mwakalebela aliwataka mashabiki wa timu hizo kuwa watulivu wakati wa mchezo huo na kuondoa dhana potofu ya ushirikina pamoja na kuwataka kuwa makini kila wanaponunua tiketi ili kukwepa udanganyifu na tiketi feki.Nao makatibu wa klabu hizo, Mwina Kaduguda wa Simba na Lawrence Mwalusako wameeleza wao hawana la kusema kuhusiana na matokeo ya mchezo huo, hivyo kuwaachia makocha wao pamoja na manahodha wa timu hizo kwani wao ndio wanao uwezo wa kuelezea jinsi walivyojipanga.Alisema ili kuondoa msongamano siku ya pambano tiketi hazitauzwa, hivyo kuwataka mashabiki na wapenzi wa mchezo huo kununua tiketi hizo mapema ili kuondoa vurugu."Tunawashauri mashabiki wanunue tiketi zao mapema kwani siku ya mchezo hatutaruhusu tiketi kuuzwa kwani chanzo cha vurugu ni ucheleweshaji wa tiketi na hivyo ili kukwepa matatizo kama hayo, leo tutaanza kuuza tiketi mpaka Ijumaa jioni ,"alisema Mwakalebela.
Odhiambo na Maftah ruska kuivaa Simba

Tibaigana alisema wachezaji hao wamefutiwa kifungo cha kukosa mechi tatu na faini ya shilingi 500,000 baada ya kikao cha kamati ya nidhamu ya TFF kuketi Jumatatu ya wiki hii.Kushindwa kuwasilishwa kwa aina ya matusi waliyotukanwa na wachezaji hao ni moja ya sababu za kuachiwa huru na kufutiwa faini ambayo ilitakiwa kulipwa na wachezaji hao.Mwenyekiti wa kamati hiyo Kamishna wa Polisi Mstaafu, Alfred Tibaigana alisema kamati yake imeshindwa kugundua kosa na kutoa maamuzi ya kuwapa uhuru wachezaji hao kwa kushindwa kugundua sababu halisi ya makosa waliyoshitakiwa.''Hukumu inaonyesha kuwa wachezaji hao walimtukana msaidizi wa mwamuzi wa kwanza mara baada ya mpira kumalizika na taarifa hizo zikaandikwa kwa taarifa ya kamisaa,''alisema Tibaigana.''Hukumu ambayo bado haina uhakika kwa kuwa walishindwa kuandika aina ya matusi ambayo yalitukanwa na wachezaji hao, na sisi kama kamati hukumu za namna hiyo huwa tunazihukumu kwa kumpa haki mshatakiwa kwa kuwa zinakuwa za shaka kwa kutokamilika.''Itakuwa bora yanapotokea matatizo kama hayo , basi waamuzi wanapoandika ripoti zao wanatakiwa kuandika aina ya matusi ambayo wanatukanwa kwa kuwa wao ni binadamu na tukio kama hilo halikuwa na ushahidi,'' alisema Tibaigana.Alisema wao kama kamati ya mashindano wamewaachia huru wachezaji hao tangu kufanyika kwa kikao hicho kilipokutana na kubaini kushindwa kwa waamuzi na kamisaa kuweka bayana matusi kutambua makosa kazi ambayo wamewaachia TFF kama itakatwa rufaa nyingine.Kutokana na uamuzi huo, Maftah na Odhiambo waliotiwa hatiani na kupewa adhabu na faini hiyo wakidaiwa kumtukana mwamuzi siku ya mchezo baina ya Yanga na Azam FC mchezo uliomaliza kwa suluhu ya bao 1-1, wameondolewa kifungoni.Hata hivyo, baada ya hukumu hiyo kutolewa msemaji wa Yanga, Louis Sendeu alisema, ''Kwa sasa tunasubiri siku tu kwani kikosi kazi kimekamilika kuona tunashinda mchezo huo.''
Wednesday, October 28, 2009
Mwakyembe agoma kuhojiwa na Takukuru

“Bunge linapokuwa kwenye mchakato wa kutaka Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru achukuliwe hatua, kisha taasisi hiyo ikaanza kuwahoji wabunge wanaosubiri utekelezaji wa maagizo waliyoyatoa, ni kinyume cha utawala wa sheria,” alisema. Kwa mujibu wa Mwakyembe, watendaji wa Takukuru walianza kuwahoji wabunge mbalimbali katika kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja, wakitaka taarifa kuhusu madai ya wabunge kupewa posho wanapotembelea taasisi za umma, licha ya kulipwa stahiki zao na ofisi ya Bunge. Dk. Mwakyembe alisema hatua iliyochukuliwa na Takukuru kuwahoji wabunge, inatia mashaka hasa kwa vile taasisi hiyo imewahi kuwalipa posho wabunge mara kadhaa. Kwa upande mwingine, Dk. Mwakyembe alisema watuhumiwa wa ufisadi wanatumia baadhi ya vyombo vya habari (akivitaja jina) kuwachafulia majina wananchi wanaotetea maslahi mapana ya umma. “Si jambo la ajabu nilivyoandikwa na gazeti la (analitaja jina), hili linamilikiwa na mafisadi, linatetea maslahi ya mafisadi kiasi cha kupoteza mvuto wake kwa wasomaji,” alisema mbunge huyo machachari.
Suala la kuhojiwa kwa wabunge kuhusiana na posho wanazodaiwa kuchua mara mbili, kwenye Bunge na kwa taasisi wanakofanya kazi, linaelezwa kuwa ni juhudi za kutaka kupunguza makali ya wabunge. Jana baadhi ya wabunge waliozungumza na gazeti hili kwa masharti ya kutotajwa majina yao, walisema wanaona mbinu hizi kama mapambano ya kitaasisi. Takukuru mwishoni mwa wiki walitoa taarifa kwa vyombo vya habari wakisema wabunge kama walivyo wananchi wengine wanawajibika kuitikia mwito wao wa kuhojiwa katika masuala mbalimbali yanaohusiana na rushwa.
Waaga Dunia wakijaribu kumuokoa mwenzao
WATU wawili: Pili Daud (29) na Amina Masud (44) wakazi wa Kawe Ukwamani, jijini Dar es Salaam, wamefariki dunia wakati wa harakati za kumuokoa Mariam Mwinyimvua (65) aliyekuwa amenaswa na umeme. Mariamu bado ni majeruhi huku wale waliotaka kumuokoa wakiwa wameaga dunia! Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye, alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya asubuhi, katika eneo hilo wakati Mariam Mwinyimvua (65) alipokuwa akitaka kuanika nguo katika kamba. Kwa mujibu wa Kamanda Kalunguyeye, kifo cha watu hao kilitokea baada ya Mariam Mwinyimvua kufua nguo zake na kuzianika kwenye waya wa umeme na kusababisha kunaswa ghafla. Kwa mujibu wa kamanda huyo, baada ya Mariam kunaswa ndipo Pili Daud alitokea kwa lengo la kumuokoa katika ajali hiyo na kwamba wakati akiwa kwenye harakati hizo naye alinaswa na umeme na kufariki papo hapo. Alisema baadaye alitokea Amina Masoud kwa lengo la kutoa msaada kwa wote wawili naye alinaswa pia na kufa papo hapo! “Walikufa wote wawili wakiwa katika harakati za kumuokoa ndugu yao aliyenaswa wakati akianika nguo,” alisema Kalunguyeye. Baada ya kutokea hali hiyo, Jeshi la Polisi, kwa kusaidiana na majirani, lilifanikiwa kumpa huduma ya kwanza Mwinyimvua na kisha kumkimbiza katika Hospitali ya Mwananyamala. Halikadhalika maiti za Pili na Amina zilipelekwa hospitalini hapo. Tanzania Daima Jumatano, ilipowasiliana na Kamanda Kalunguyeye baadaye kwa njia ya simu, alisema kuwa hali ya majeruhi huyo ni mbaya na wamemhamishia katika chumba cha wagonjwa mahututi.
Wazungu wezi kutoka ATM machine wapigwa kalenda
NEDKO Stanchen (34) na mkewe Stella Nedelcheva (28) raia wa nchini Bulgaria walioiba fedha zaidi ya shilingi Mil 70 kutoka kwenye mashine ya ATM ya Benki ya Baclays kesi yao imepigwa kalenda na kuahirishwa kwakuwa upelelezi wa shauri hilo kudaiwa kuw
Watuhumiwa hao walifikishwa leo mbele ya Hakimu Mkazi, Bingi Mashabara ambaye ameahirisha kesi hiyo kwa sababu hiyo na kupanga tarehe nyingine ya kusikiliza shauri hilo. Kesi hiyo ilikuja mahakamani hapo leo kwa ajili ya kutajwa.Washitakiwa hao wanadaiwa kuwa Julai mwaka huu waliiba katika mashine za kutolea fedha za ATM sh.milioni 14.5 mali ya Baclays.Kesi hiyo itakuja tena mahakamani hapo, Novemba 2, mwaka huu.
Watuhumiwa hao walifikishwa leo mbele ya Hakimu Mkazi, Bingi Mashabara ambaye ameahirisha kesi hiyo kwa sababu hiyo na kupanga tarehe nyingine ya kusikiliza shauri hilo. Kesi hiyo ilikuja mahakamani hapo leo kwa ajili ya kutajwa.Washitakiwa hao wanadaiwa kuwa Julai mwaka huu waliiba katika mashine za kutolea fedha za ATM sh.milioni 14.5 mali ya Baclays.Kesi hiyo itakuja tena mahakamani hapo, Novemba 2, mwaka huu.
Tuesday, October 27, 2009
Historia kuibeba simba Jumamosi

Mshtakiwa wa Kesi ya EPA hoi
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jana ilishindwa kusikiliza kesi ya wizi wa Sh 3.8 bilioni inayomkabili Farijala Hussein na wenzake baada ya mshtakiwa huyo kushindwa kusimama kizimbani kutokana na kusumbuliwa na tatizo la figo. Kesi hiyo ilipangwa kuendelea kusikilizwa mfululizo jana kwa mashahidi wa upande wa mashtaka, lakini Farijala ambaye alikuwepo mahakamani hapo alionekana amevimba uso na tumbo na hivyo kushindwa kusimama kizimbani. Wakili anayemtetea mshtakiwa huyo, Majura Magafu aliomba mahakama iahirishe kesi hiyo baada ya kudai kuwa mteja wake hataweza kukaa kizimbani kusikiliza kesi kutokana na kuumwa. Hata hivyo, wakili wa serikali, Frederick Manyanda alipinga hoja hizo na kudai kuwa si za msingi kwani upande wa utetezi ulipaswa kuithibitishia mahakama kwa kuonyesha vyeti.
Baada ya kusikiliza hoja za pande zote, kiongozi wa jopo la mahakimu wanaosikiliza kesi hiyo, Samuel Karua aliahirisha kesi hiyo hadi leo ili kuangalia hali ya mshtakiwa huyo. Katika hatua nyingine, mshtakiwa wa pili, Rajabu Maranda jana aliwasilisha ombi mahakamani hapo la kutaka aruhusiwe kusafiri nje ya Dar es Salaam ili aende kwenye shughuli za kisiasa. Washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Ajay Somani, Imani Mwakosya, Esther Komu na Sophia Kalika. Washtakiwa hao wanadaiwa kuwa waliiba zaidi ya Sh3 bilioni kutoka kwenye Akaunti ya malipo ya Madeni ya Nje (EPA) iliyokuwa Benki Kuu (BoT) baada ya kudanganya kuwa kampuni ya Mibare Farm imepewa deni na kampuni ya Textile Mills Ltd ya nchini India. Wakati huohuo, mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jana iliridhia maombi ya mfanyabiashara Jayant Kumar, maarufu kama Jeetu Patel, anayekabiliwa na kesi ya wizi wa Sh3.3 bilioni ya kutaka kesi hiyo isitishwe mahakamani hapo ili jalada liende Mahakama Kuu kwenye kesi aliyoifungua ya kikatiba. Akitoa uamuzi huo huku akinukuu kesi mbalimbali na vifungu vingine vya sheria, Hakimu Mkuu Mkazi Richard Kabate alisema upande wa mashtaka umeshindwa kutoa tafsiri sahihi kuhusu mwenendo wa kesi. Awali upande wa mashtaka ulipinga jalada hilo kupelekwa Mahakama Kuu baada ya kudai kwamba hoja za upande wa utetezi hazina msingi wowote kwani maneno yanayolalamikiwa ni ya mitaani na wala hayajaathiri mwenendo wa kesi hiyo.
Hakimu Kabate alisema kwa mujibu wa sheria Mahakama ya Kisutu haina uwezo wa kuyatolea maamuzi malalamiko yaliyotolewa na Jeetu. Katika malalamiko yake Jeetu anadai kuwa mwenendo wa kesi yao umeingiliwa kutokana na matamshi aliyoyatoa mwenyekiti mtendaji wa IPP, Reginald Mengi kwamba wao ni mafisadi papa. Alidai kuwa katika matamshi hayo ambayo yalitolewa kupitia kipindi maalumu kilichorushwa na kituo cha televisheni cha ITV, Mengi aliingilia uhuru wa mahakama kwa kuwahukumu wakati kesi yao bado inaendelea mahakamani.
Alidai kuwa kutokana na matamshi hayo jamii iliwaona wao wana hatia dhidi ya tuhuma zinazowakabili. Tayari mahakama ya Kisutu imeridhia kusitishwa kwa kesi nyingine mbili zinazomkabili Jeetu na wenzake ili majalada ya kesi hizo yapelekwe Mahakama Kuu kwenye kesi ya kikatiba aliyoifungua. Kesi hiyo itatajwa Novemba 6 mwaka huu. Jeetu, Devendra Patel na Amit Nandy wanadaiwa kuiibia BoT Sh 3.3 bilioni baada ya kudanganya kuwa kampuni yao ya Navy Cut Tobacco (T) Ltd imepewa deni hilo na kampuni ya Matsishuta ya nchini Japan.
Baada ya kusikiliza hoja za pande zote, kiongozi wa jopo la mahakimu wanaosikiliza kesi hiyo, Samuel Karua aliahirisha kesi hiyo hadi leo ili kuangalia hali ya mshtakiwa huyo. Katika hatua nyingine, mshtakiwa wa pili, Rajabu Maranda jana aliwasilisha ombi mahakamani hapo la kutaka aruhusiwe kusafiri nje ya Dar es Salaam ili aende kwenye shughuli za kisiasa. Washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Ajay Somani, Imani Mwakosya, Esther Komu na Sophia Kalika. Washtakiwa hao wanadaiwa kuwa waliiba zaidi ya Sh3 bilioni kutoka kwenye Akaunti ya malipo ya Madeni ya Nje (EPA) iliyokuwa Benki Kuu (BoT) baada ya kudanganya kuwa kampuni ya Mibare Farm imepewa deni na kampuni ya Textile Mills Ltd ya nchini India. Wakati huohuo, mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jana iliridhia maombi ya mfanyabiashara Jayant Kumar, maarufu kama Jeetu Patel, anayekabiliwa na kesi ya wizi wa Sh3.3 bilioni ya kutaka kesi hiyo isitishwe mahakamani hapo ili jalada liende Mahakama Kuu kwenye kesi aliyoifungua ya kikatiba. Akitoa uamuzi huo huku akinukuu kesi mbalimbali na vifungu vingine vya sheria, Hakimu Mkuu Mkazi Richard Kabate alisema upande wa mashtaka umeshindwa kutoa tafsiri sahihi kuhusu mwenendo wa kesi. Awali upande wa mashtaka ulipinga jalada hilo kupelekwa Mahakama Kuu baada ya kudai kwamba hoja za upande wa utetezi hazina msingi wowote kwani maneno yanayolalamikiwa ni ya mitaani na wala hayajaathiri mwenendo wa kesi hiyo.
Hakimu Kabate alisema kwa mujibu wa sheria Mahakama ya Kisutu haina uwezo wa kuyatolea maamuzi malalamiko yaliyotolewa na Jeetu. Katika malalamiko yake Jeetu anadai kuwa mwenendo wa kesi yao umeingiliwa kutokana na matamshi aliyoyatoa mwenyekiti mtendaji wa IPP, Reginald Mengi kwamba wao ni mafisadi papa. Alidai kuwa katika matamshi hayo ambayo yalitolewa kupitia kipindi maalumu kilichorushwa na kituo cha televisheni cha ITV, Mengi aliingilia uhuru wa mahakama kwa kuwahukumu wakati kesi yao bado inaendelea mahakamani.
Alidai kuwa kutokana na matamshi hayo jamii iliwaona wao wana hatia dhidi ya tuhuma zinazowakabili. Tayari mahakama ya Kisutu imeridhia kusitishwa kwa kesi nyingine mbili zinazomkabili Jeetu na wenzake ili majalada ya kesi hizo yapelekwe Mahakama Kuu kwenye kesi ya kikatiba aliyoifungua. Kesi hiyo itatajwa Novemba 6 mwaka huu. Jeetu, Devendra Patel na Amit Nandy wanadaiwa kuiibia BoT Sh 3.3 bilioni baada ya kudanganya kuwa kampuni yao ya Navy Cut Tobacco (T) Ltd imepewa deni hilo na kampuni ya Matsishuta ya nchini Japan.
ADHT karibuni nyumbani karibuni Tanzania

Baunsa mdogo kuliko wote duniani huyu hapa

Monday, October 26, 2009
Kitu gani chamrudisha IRENE UWOYA ?

Mgombea wa CCM afariki dunia akisubiri kutangazwa mshindi
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kilolo, kimepata pigo baada ya mwanachama wake aliyepita bila kupingwa katika nafasi ya Mwenyekiti, Ashery Kigava wa Kitongoji cha Amani katika Kijiji cha Lukani, kufariki dunia wakati akisubiri kutangazwa kuwa mshindi.
Akitoa taarifa ya kifo hicho, mbele ya Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Profesa Peter Msolla wakati wa mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Lukani, Diwani wa Kata ya Ukumbi, Chesco Ngimba alisema kifo cha mwenyekiti huyo mteule kilitokea juzi. Kwa upande wake, Profesa Msolla mbali ya kutoa rambirambi kwa wafiwa, alisema CCM imepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha kiongozi huyo mratajiwa na kuongeza kuwa, ni pingo ndani ya chama na kitongoji hicho.
Akitoa taarifa ya kifo hicho, mbele ya Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Profesa Peter Msolla wakati wa mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Lukani, Diwani wa Kata ya Ukumbi, Chesco Ngimba alisema kifo cha mwenyekiti huyo mteule kilitokea juzi. Kwa upande wake, Profesa Msolla mbali ya kutoa rambirambi kwa wafiwa, alisema CCM imepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha kiongozi huyo mratajiwa na kuongeza kuwa, ni pingo ndani ya chama na kitongoji hicho.
Wanachama wa DECI Arusha wafungua kesi ya Madai
WANACHAMA 300 wa Kampuni ya Development Entrepreneurship Community Initiative (DECI) mkoani Arusha, wamefungua kesi ya madai katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, kudai fidia ya sh bilioni 2. Kesi hiyo inatarajiwa kuanza kutajwa rasmi leo mahakamani hapo kwa mahakama kupanga rasmi tarehe ya kuanza kusikilizwa. Wanachama hao wanaowakilisha wenzao 4,700 katika kesi hiyo, wanataka viongozi wakuu wa kampuni hiyo kuwalipa fedha zao walizopanda na riba baada ya kuvunja mkataba baina yao. Akizungumza kwa niaba ya wananchama wenzake, msemaji wa wana DECI hao, Leonard Kilasi, alisema wameamua kufungua kesi hiyo baada ya kujiridhisha kuwa viongozi wa kampuni hiyo hawana mpango wa kurejesha fedha zao. “Mpaka sasa hatufahamu hatma ya fedha zetu, hivyo tumeamua kufungua kesi ili mahakama iweze kutenda haki na sisi tupate fedha zetu tulizopanda kabla ya kampuni hiyo kufutwa,” alisema Kilasi. Aidha, Kilasi alisema wadaiwa wa kwanza katika kesi hiyo ni wakurugenzi wa DECI makao makuu, na mwakilishi wao mkoani hapa, Salome Ilungu. Hata hivyo, wakati wana DECI hao wakikusudia kufungua kesi, tayari wakurugenzi wa taasisi hiyo inayojishughulisha na kazi ya kupanda na kuvuna pesa, wameshafunguliwa kesi na serikali wakidaiwa kuendesha mchezo huo wa upatu kinyume cha sheria.
Mapacha walioungana wakataa kutenganishwa

Mapacha wa nchini India, Ganga na Jamuna Mondal wenye umri wa miaka 39 maarufu duniani kama "Spider Sisters" wameungana katika namna ambayo ni nadra sana kutokea duniani kwani wameungana kuanzia kiunoni lakini kila mmoja ana mguu wake mmoja huku miguu yao ya pili imeungana pamoja na kufanya mguu mmoja wa tatu wenye vidole tisa.Awali madaktari walionya kuwa kujaribu kuwatenganisha kutahatarisha maisha yao lakini daktari mtaalamu wa mapacha walioungana wa nchini Marekani, Dr James Stein aliwafanyia uchunguzi mapacha hao na amedai kuwa mapacha hao wanaweza kutenganishwa bila kuhatarisha maisha yao.Lakini mapacha hao wamekataa kutenganishwa na kusema "Tutaishi kama jinsi ambavyo Mungu ametuumba".Kila pacha mmoja ana kichwa chake na mikono yake miwili.
Je tutafika? Malawi Yajiandaa Kuhalalisha Uhakaba

Hatimaye Mtoto amzaa mtoto mwenzie

Mtoto Shiloh Pepin maarufu kama 'Nguva Mtoto' Afariki Dunia

Alipozaliwa katika hali hiyo madaktari walidai atafariki ndani ya siku chache lakini ameweza kuishi miaka 10 duniani.Shiloh Pepin maarufu kama "Nguva Mtoto" alizaliwa miguu yake ikiwa imeunganika na kukusanyika sehemu moja kuanzia kiunoni mpaka chini kama nguva alivyo.Madaktari hawakuweza kuitenganisha miguu yake kutokana na kwamba ilikuwa imekusanyika pamoja na kuzungukwa na mishipa mikubwa ya damu hivyo kujaribu kuitenganisha miguu hiyo kungehatarisha maisha yake.Shiloh alizaliwa akiwa na ugonjwa unaoitwa "mermaid syndrome" ambao pia unajulikana kama "sirenomelia" na kutokana na maelezo ya madaktari hakuna aliyetegemea angeishi miaka 10.Shiloh Pepin "Nguva Mtoto" alizaliwa katika mji wa Kennebunkport, Maine nchini Marekani mwezi wa nane mwaka 1999.Alizaliwa akiwa hana utumbo mdogo, tumbo la uzazi wala uke na alikuwa na figo moja tu na ovari moja tu. Miguu yake iliungana pamoja kuanzia kiunoni mpaka chini.Shiloh alikuwa maarufu duniani kupitia televisheni mbali mbali duniani zilizofanya mahojiano naye, video zake nyingi zipo kwenye mitandao duniani.Shiloh alitokea kupendwa na watu wengi sana na aliwapa changamoto watu wengi kwa kuendelea na maisha yake kwa furaha kama walivyo watoto wengine ingawa alikuwa hawezi hakutembea akitembea kwa kujiburuza chini.Shiloh aliwahishwa hospitali mwanzoni mwa mwezi huu baada ya kusumbuliwa na mafua na baadae kugundulika ana pneumonia.Shiloh alilazwa hospitali kuanzia oktoba 10 mwaka huu akipewa dripu za antibiotics na akipumua kwa kutumia mashine.
Wachapwa Bakora Kwa Kuangalia Video za Ngono Kwenye Simu

Je haki imetendeka? Ahukumiwa kifungo cha miezi 8 kwa kosa la Mauaji na kuachiwa huku baada ya kutumikia miezi 3

Mlowezi Tom Cholmondeley alihukumiwa kwenda jela miezi minane baada ya kesi yake ya mauaji kubadilishwa kuwa kesi ya kuua bila kukusudia.Mlowezi huyo tajiri alimuua kwa kumpiga risasi raia wa Kenya, Robert Njoya aliyeingia kwenye shamba lake lililopo kwenye mkoa wa Rift Valley ili kuwinda wanyama pori.Mlowezi huyo aliachiwa huru ijumaa kabla ya hata ya miezi minane aliyohukumiwa kuisha kwa kile kilichoelezwa kuwa alionyesha tabia nzuri.Wakati alipokuhumiwa kutumikia kifungo cha miezi minane jela mwezi wa tano mwaka huu, mlowezi huyo alikuwa ameishakaa jela miaka mitatu akisubiria hukumu yake.Jaji wa mahakama kuu ya Kenya, Muga Apondi ndiye aliyetoa hukumu hiyo ya miezi minane jela na kusababisha hasira za wananchi mbali mbali wa Kenya waliokuwa wakilalamika kuwa sheria imepindishwa ili kuwabeba matajiri.Jaji Apondi akiielezea hukumu aliyoitoa alisema kuwa mlowezi huyo hakuua kwa kukusudia kwani baada ya kumpiga risasi Robert Njoya, alijaribu kutoa huduma ya kwanza na alimpeleka hospitali.Mwaka mmoja kabla ya kumuua Robert Njoya mlowezi huyo huyo alimuua raia mwingine wa Kenya lakini kesi yake ilifutwa katika hali ya utatanishi.
Ashikiliwa kwa kumlawiti binti yake
MWANAUME mmoja aitwae Daniel Makundi (40) anashikiliwa na Polisi mkoani Tanga kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wake. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Simon Sirro, alisema tukio hilo lilitokea juzi, majira ya 7 za usiku katika Kata ya Nguvumali mkoani humo.Kamanda huyo alisema kuwa mtoto huyo alipohojiwa na jeshi hilo alieleza kuwa ni mara kwa mara mzazi wake huyo alikuwa anamfanyia kitendo hicho.Na kusema hiyo ni mara yake ya sita kufanyiwa kitendo hicho na ndipo ilipogundulika.Kamanda huyo amesema kuwa katika uchunguzi uliofanyika na madaktari ilibainiuka kuwa mtoto huyo alishawahi kufanyiwa kitendo hicho kabla ya hapo.Hivyo mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani mwanzoni mwa wiki ijayo ili kujibu shtaka linalomkabili.
Thursday, October 22, 2009
Mbwa huyu amponza Boss wake

Mauaji ya Albino yanaendelea- Mtoto albino auwawa kwa kukatwa shingo
MWANAFUNZI wa darasa la pili katika Shule ya Msingi Nyawilimilwa, wilayani Geita, Mwanzamwenye ulemavu wa ngozi, Gasper Elikana (10) ameuawa kwa kukatwa shingo na mguu wake kunyofolewa. Mbali na kumuua albino huyo saa 2:30 usiku juzi, wauaji hao walimjeruhi vibaya kwa mapanga, baba yake mzazi, Elikana Ngelela (44). Kufuatia tukio hilo, Jeshi la Polisi limetangaza zawadi ya sh 1,000,000 kwa yeyote atayetoa taarifa za kukamatwa kwa wahusika, kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, Bw. Elias Kalinga alipozungumza na Majira jana jioni baada ya kufika eneo la tukio. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Abbas Kandoro alisema kuwa alipokea taarifa za tukio hilo kwa masikitiko makubwa na kwamba kitendo hicho lazima kikemewa na kila Mtanzania anayejali maisha ya binadamuwenzake. Bw. Kandoro alisema utajiri haupatikani kwa kukata viungo vya albino bali ni watu kufanya kazi kwa bidii ili wajiletee maendeleo. Alisema kuwa serikali inatoa wito kwa jamii kutoa ulinzi kwa walemavu wa ngozi mkoani Mwanza na si kuiachia serikali pekee katika mapambano dhidi ya watu wanaojihusisha na vitendo hivyo vya kinyama. Bw. Kandoro alisema ameagiza timu maalumu kutoka mkoani Mwanza, ikiongozwa na Bw. Kalinga kwenda wilayani Geita kufanya uchunguzi kuungana na Kikosi Kazi kinachoongozwa na Mkuu wa Wilaya yaGeita, Bw. Philemon Shelutete. Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Geita, Dkt.Cassian Kabuche alisema kuwa majeruhi ambaye amelazwa wodi namba nane hospitali hapo hali yake si ya kuridhisha kutokana na majeraha aliyopata kichwani. "Alifikishwa hapa jana (juzi) usiku akiwa hajitambui kiasi kwamba iwapo hali ingeliendelea hivyo hadi leo (jana), tungempeleka katika Hospitali ya Rufaa Bugando jijini Mwanza, lakini kutokana na juhudi zilizozifanya hali yake angalau inatia moyo kidogo," Alisema Dkt.Kabuche.Habari zilizopatikana kijijini hapo, zinasema wauaji hao wakiwa na mapanga, walifika nyumbani kwa Bw. Ngelela na kuanza kumshambulia kwa mapanga na kisha kumuua mwanaye. Mkazi wa kijiji hicho, Bw. Makami Nkilijiwa, alisema majirani walisikia kelele za kuomba msaada kutoka kwa mama wa mtoto huyo, nawalipofika walikuta wauaji wamekwishatoweka na mguu wa kulia wa mtoto huyo, huku mwili wake ukiwa umekatwa shindo huku baba yake akiwa ajitambui. Baada ya kuona hali hiyo, wakazi wa kijiji hicho walimchukua majeruhi na mwili wa marehemu hadi Hospitali ya Wilaya ya Geita ambako maiti imehifadhiwa na majeruhi akiendelea na matibabu.
Haya Mambo bado yapo? Mtoto afa kwa kukeketwa!!
POLISI mkoani Manyara wanamshikilia Bw. Danieli Shauri (37) kwa kosa la kumkeketa binti yake, Debora Daniel (4) na kumsababishia kifo.Mtoto huyo alikeketwa Oktoba 11, mwaka huu na kuendelea kuvuja damu sehemu za siri hadi Oktoba 18 alipofariki dunia.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Parmena Sumary alisema kuwa tukio hilo lilitokea siku hiyo saa 10.00 jioni katika Kijiji cha Imbilili wilayani Babati.Kamanda Sumary alisema kabla ya kifo chake, mtoto huyo alikuwa akiishi na mtuhumiwa baada ya mama yake mzazi, Bi. Chatherine Daniel (29) kupata kichaa na kumtelekeza akiwa mdogo.Kutokana na hali hiyo mtoto huyo alikosa afya na kupata na homa za mara kwa mara kwa sababu ya kukosa maziwa ya mama, hali iliyosababisha wazazi wa mtuhumiwa kushauri akeketwe ili kuondokana na matatizo hayo.Kamanda alisema kuwa mtuhumiwa alitekeleza ushauri potofu wa wazazi wake, lakini alishangazwa na hali ya mtoto huyo kuendelea kuwa mbaya hadi alipofariki dunia kwa kupoteza damu nyingi.Baada ya kifo hicho kutokea, mtuhumiwa alitaka kuuzika mwili wa mtoto huyo bila ya watu kujua lakini wasamaria alitoa taarifa kwa Mtendaji wa Kijiji hicho, Patizumu Jeseph ambaye alifika nyumbani kwa mtuhumiwa na kukuta maandalizi ya mazishi na kuwaamuru kusimamisha shughuli hiyo hadi hatua za kisheria zitakapofuatwa.Baada ya amroi hiyo mwili huo ulichukuliwa hadi Hospitali ya Wilaya ya Babati kwa uchunguzi zaidi na ndipo iligundulika kuwa marehemu alipatwa na mauti hayo baada ya kukeketwa na kuvuja damu nyingi.Kwa mujibu wa kamanda huyo, ngariba aliyehusika kumkeketa mtoto huyo, Mama Mangiza, alitoroka baada ya hali ya mtoto inakuwa mbaya na polisi wanaendelea kumsaka kujibu shtaka hilo.
Mpigie Kura Elizabeth

Wednesday, October 21, 2009
Tulikupenda sana ila Mungu alikupenda zaidi - Buriani Masanja
Huu ni Ukatili kupitiliza ukomeshwe

First Lady Apewa TUZO ya Mama wa Upendo

Ndoa ya Monaliza Chinda yafikia Kileleni

Zain yaja na Huduma Mpya ya Pamoja Plus (+)

Akifanya uzinduzi huo jana asubuhi kwenye ukumbi wa Kibo katika Hoteli ya Kilimanjaro (Kempinski) hapa Dar es Salaam mbele ya Wanahabari, Mkurugenzi Mtendaji wa Zain Tanzania Bwana Khaled Muhtadi amesema kwa sasa wateja wake watapata huduma nafuu kwa kupewa punguzo la hadi asilimia hamsini (50%) kwa simu za Zain pamoja na mitandao mingine watakazopiga. Ameeleza kuwa mteja atakayejiunga na huduma hiyo (Pamoja Plus), atapata nafasi ya kusajili namba za watu kumi (10) wa mtandao wa Zain atakazopata, kisha ataongeza tena namba moja kutoka mtandao mwingine wowote aupendao ambayo nayo itafaidi punguzo hilo huku akiweza kubadilibadili namba hizo hadi mara tatu kwa mwezi apendavyo. Aidha Mkurugenzi huyo Mtendaji wa Zain nchini amesema zile simu za Zain zitakazopigwa na ambazo haziko katika chaguo la namba alizozisajili katika Pamoja Plus nazo zitapata punguzo la asilimia ishirini (20%) na pia zile za mitandao mingine ambazo nazo hazijasajiliwa zitapata punguzo la asilimia kumi na saba (17%).
Kumbe mambo ya Limbwata hadi Majuu yapo !!!!!!!Cristiano Ronaldo apigwa JUJU

Tuesday, October 20, 2009
Maajabu ya Kweli jitahidi na wakwako awe kama huyu

Mtoto wa Ajabu awashangaza Wanasayansi Duniani

Wanasayansi nchini Urusi wameshindwa kujua ni nini kinapelekea mtoto anayeitwa Ali mwenye umri wa miezi tisa, mwili wake uwe unatoa maandishi tofauti tofauti ya kiarabu mara kwa mara.Televisheni ya Vesti news ya nchini Urusi ilionyesha video ya mtoto huyo na picha ambazo wazazi wake wamekuwa wakimpiga kila maandishi mapya yanapotokea.Kwa mujibu wa wazazi wake wanaoishi kwenye mji wa Dagestan, siku mbili baada ya Ali kuzaliwa herufi za kiarabu zilianza kujitokeza kwenye miguu yake na baada ya siku kadhaa zilianza kutengeneza maneno kamili.Maandishi tofauti tofauti ya kiarabu hutokea zaidi kila siku ya jumatatu na ijumaa kwenye sehemu mbalimbali za mwili wake.Awali kulikuwa na alama za maandishi yaliyofifia kwenye kidevu chake na baadae maandishi hayo yalijitokeza wazi yakisomeka "Allah", alisema mama wa mtoto huyo Madina Yakubova.Miongoni mwa maneno ambayo yamesomeka wazi ni yale yanayosema "Waonyesheni watu dalili za kuwepo kwangu".Kwa kushangaza zaidi kwenye mguu mmoja wa Ali yalijitokeza maandishi yaliyosemeka "Allah (Mungu) ndiye muumba wa vitu vyote".Ali alipozaliwa aligundulika kuwa na matatizo makubwa ya moyo wake na ugonjwa unaoathiri zaidi ubongo unaoitwa "cerebral paralysis" lakini alipopimwa tena baada ya maandishi hayo ya kiarabu yalipoanza kujitokeza aligundulika hana matatizo yoyote na afya njema.Madaktari nchini Urusi hawajui ni nini kinaendelea kwenye mwili wa mtoto huyo na wamekiri hawajawahi kwamba hawana jibu la kutoa kwa taaluma za kisayansi.
Mtoto amnyang'anya Baba yake Mke!!!!!!!!!!!!!!

Kijana mwenye umri wa miaka 18 wa nchini Uingereza ametoroka na mama yake wa kambo mwenye umri wa miaka 34 baada ya kumchanganya kimapenzi na kupelekea avunje ndoa yake.Benjamin Smith alisababisha ndoa ya baba yake, Andrew Smith na mama yake wa kambo Dawn Smith ivunjike ikiwa ni miezi michache baada ya kukutana naye kwa mara ya kwanza tangia alipomtelekeza alipokuwa mtoto miaka 17 iliyopita.Benjamin Smith alikutana na baba yake mwaka jana na alihamia kwenye nyumba yake kuanza maisha mapya akiishi na baba yake.Lakini muungano huo wa baba na mwana uligeuka kuwa chachu kwa baba wa kijana huyo.Mke wake alianza kufanya mapenzi na kijana huyo na haikuchukua muda mrefu ndoa yao ilivunjika.Kijana huyo na mama yake wa kambo walitoroka na kuhamia mji mwingine jirani wa Lincoln kuanza maisha mapya pamoja.Kutokana na kwamba Benjamin alikuwa na mojawapo ya funguo za nyumba ya baba yake, alirudi nyumbani kwa baba yake kisiri na kumuibia pesa sawa na paundi 150.Benjamin alikamatwa na polisi na kufikishwa kizimbani ambako alikiri kosa lake na kuhukumiwa kufanya kazi bila malipo kwa masaa 60 pamoja na kumrudishia baba yake pesa alizomuibia.Si baba, mwana wala mama wa kambo ambaye alikuwa tayari kuzungumzia mkasa huu ambao umewavutia watu wengi nchini Uingereza.
Monday, October 19, 2009
Simba Yaigeuza asusa JKT Ruvu 4 -1

Vita Ya Ufisadi yageuka Shubiri
VITA ya ufisadi iliyotangazwa na baadhi ya wabunge waliojipambanua kuwa ni wapambanaji wa ufisadi na kuungwa mkono na baadhi ya watu hivi sasa inaonekana kuwa shubiri kutokana na baadhi ya maamuzi yaliyofanywa kwa hofu ya ufisadi kuonekana kuigharimu nchi kiasi cha kuhatarisha ustawi wa kiuchumi na kijaami.
Uhasama baina ya wabunge na mawaziri wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ulioonekana katika Bunge lililopita kiasi cha kuilazimisha Halmashauri Kuu ya chama hicho kuunda kamati maalum ya kutafuta suluhu ni miongoni mwa mambo yaliyochangiwa kwa kiasi kikubwa na vita hiyo ambayo hivi sasa imeacha majeraha makubwa nchini.
Uchunguzi wa Tanzania Daima Jumapili pamoja na mahojiano iliyofanya na baadhi ya viongozi mbalimbali imeonyesha baadhi ya maamuzi nyeti yanashindwa kupata baraka za viongozi wa kisiasa ambao hivi sasa wamekuwa wakitaka kushindana na kukomoa pasi na kuangalia athari za maamuzi yao.
Kukomoa huko ndiko kunakomtikisa Rais Jakaya Kikwete pamoja na kamati aliyoiunda chini ya Rais mstaafu, Alli Hassan Mwinyi, ambayo imeshaanza kuonyesha kutokuwa na uwezo uliotarajiwa kutatua suala hilo linaloonekana kuizidi kimo CCM.
Chuki miongoni mwa wabunge na mawaziri wa CCM sasa imeonekana si kukitafuna chama bali hata mgawo wa umeme uliopo ambao baadhi ya watendaji shirika la ugavi wa umeme nchini (TANESCO) walishatoa mapendekezo kadhaa serikalini ili kuinusuru nchi kuingia katika janga hilo.
Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Dk. Idris Rashid, ni mmoja wa watendaji waliosimama kidete kuelezea mipango yao ya kuboresha uzalishaji wa umeme ikiwemo kununua mitambo mipya, kununua ya Dowans na mingine ambayo ilikumbana na vikwazo vikali.
Baada ya Dk. Idris kupata upinzani huo alitangaza kuwa TANESCO imejitoa kununua mitambo ya Dowans huku akionya kuwa shirika hilo lisije likalaumiwa kwa mgawo ambao ungejitokeza Oktoba na Novemba mwaka huu.
Onyo hilo la Dk. Idris lipokewa kwa shutuma nzito na baadhi ya wanasiasa wakiongozwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ambayo ilidai bora nchi iingie gizani kuliko kununua mitambo hiyo.
Mgawo wa umeme ulioanza wiki iliyopita wa saa 14 kwa siku ndiyo umewafanya baadhi ya wananchi, wanasiasa, wafanyabiashara kukumbuka onyo la Dk. Idris na kuwalaumu viongozi walioshiriki kwa namna moja au nyingine kukwamisha mipango ya TANESCO.
Wakati mgawo wa umeme ukionekana kushika kasi Kamati ya Nishati na Madini, chini ya Mbunge wa Bumbuli, William Shelukindo (CCM), itangaza kufanya uchunguzi ili kuona kama mgawo huo umesababishwa na watendaji wa TANESCO ili kutimiza mipango yao hasa ya kununua mitambo ya Dowans.
Kamati hiyo ilizungumza na watendaji wa TANESCO na baadaye ilisalimu amri kuwa mgawo huo ulitokana na kuharibika kwa mashine kadhaa pamoja na upungufu wa maji kama ambavyo shirika hilo lilivyotangaza.
Baadhi ya wafanyabiashara wenye viwanda wameingiwa na hofu ya kuendelea kufanyabiashara hasa kutokana na mgawo huo ambao umeathiri kwa kiwango kikubwa uzalishaji.
Shirikisho la Wenye Viwanda Nchini (CTI) ni miongoni mwa wadau waliojitokeza kutaka nchi isiendelee kuwa gizani kwa kuendekeza maamuzi yenye athari ilhali kuna mitambo yenye uwezo wa kuzalisha umeme lakini inashindwa kutumika.
Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) ni miongoni mwa taasisi za serikali zinazoathirika na mgawo huo kwa kuwa imekuwa ikipoteza mapato mbalimbali iliyokuwa ikiyapata kutokana na uzalishaji mali.
Wachambuzi wa masuala ya kiuchumi wameweka bayana kuwa nchi ipo hatari kuporomoka zaidi kiuchumi kama serikali haitochukua hatua za haraka kutafuta vyanzo vya kudumu vya kuzalisha nishati ya umeme ambayo hutegemewa na viwanda mbalimbali.
Wakati wachambuzi hao wakitoa tahadhari hiyo, Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Zitto Kabwe, ambaye siku za nyuma alijitokeza hadharani kulitaka Bunge na serikali kufikiria upya juu ya mitambo ya Dowans na ikiwezekana wainunue ili nchi isiingie gizani ameibuka tena kuitaka serikali itaifishe mitambo hiyo.
Zitto alisema uamuzi wa kuitaifisha mitambo hiyo ni mgumu lakini kwa hali ilivyo hivi sasa ni lazima viongozi wakubali kufanya umuzi huo hata kama watasakamwa na wahisani kwa kukiuka sheria.
Hoja hiyo ya Zitto kwa kiasi kikubwa imeonekana kuungwa mkono na kada mbalimbali za wananchi huku serikali kupitia kwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, akikataa kufanya hivyo kwa madai ni kukiuka sheria za nchi.
Kauli hiyo ya Ngeleja imeonekana kupingwa na baadhi ya watu wakiwemo wanasheria ambao wameweka bayana kuwa serikali imekuwa ikikiuka sheria mbalimbali ambapo wakati mwingine si kwa manufaa ya walio wengi hivyo ni vema kufikiria upya wazo la Zitto.
Tindu Lissu ni mmoja wa wanasheria aliyeweka wazi kuwa serikali haiwezi kuwa na kesi ya kujibu kama ikifikia hatua hiyo kwa kuwa sheria ya kimataifa ya uwekezaji pamoja na namna mitambo hiyo ilivyoingia hapa nchi imegubikwa na mizengwe.
Mwanasheria ameweka bayana kuwa hofu hiyo ya serikali haipaswi kupewa nafasi katika kipindi hiki ambacho nchi ipo hatarini kuporomoka kiuchumi kutokana na kushuka kwa uzalishaji viwandani.
Mgawo wa umeme umeonekana kuibua upya sakata la vita ya ufisadi ambalo lilishika kasi baada ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa kutokana na kuhusishwa katika kashfa ya kuipa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharula kampuni ya Richmond ambayo ilibainika kutokuwa na uwezo.
Sakata la Richmond ndilo kwa kiasi kikubwa lililozaa ufa na makundi yenye kuhasimiana vikali ndani na nje ya Bunge kiasi cha kuhatarisha mustakabali wa CCM ambao katika siku za hivi karibuni umekumbwa na kashfa mbalimbali.
Wachambuzi wa masuala ya siasa wanaona serikali itakuwa na wakati mgumu wa kuamua kipi cha kufanya kumaliza tatizo la mgawo wa umeme ambalo kwa namna moja au nyingine lilisababishwa na utendaji usio makini pamoja na tamaa za watu waliopewa jukumu la kuongoza nchi.
Moja kati ya sababu inayowafanya wachambuzi hao kuiona serikali kuwa iko njia ni ukweli kuwa wabunge walio katika mstari wa mbele kupinga baadhi ya mambo ni kutoka CCM ambacho ndicho chama kilichoshikilia dola.
Wachambuzi hao pia hawakusita kueleza wakati mgumu itakaokumbana nao Kamati ya Mzee Mwinyi iliyopewa jukumu la kutatua uhusiano mbovu baina ya wabunge na mawaziri ulioshamiri hivi sasa.
Ugumu wa Kamati ya Mzee Mwinyi unadaiwa utachagizwa zaidi na joto la uchaguzi mkuu ambapo kila mbunge anataka kuonekana anawajibika kwa wananchi wake hivyo kuwawia vigumu viongozi wa serikali. (Habari toka Mtanzania Daima)
Uhasama baina ya wabunge na mawaziri wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ulioonekana katika Bunge lililopita kiasi cha kuilazimisha Halmashauri Kuu ya chama hicho kuunda kamati maalum ya kutafuta suluhu ni miongoni mwa mambo yaliyochangiwa kwa kiasi kikubwa na vita hiyo ambayo hivi sasa imeacha majeraha makubwa nchini.
Uchunguzi wa Tanzania Daima Jumapili pamoja na mahojiano iliyofanya na baadhi ya viongozi mbalimbali imeonyesha baadhi ya maamuzi nyeti yanashindwa kupata baraka za viongozi wa kisiasa ambao hivi sasa wamekuwa wakitaka kushindana na kukomoa pasi na kuangalia athari za maamuzi yao.
Kukomoa huko ndiko kunakomtikisa Rais Jakaya Kikwete pamoja na kamati aliyoiunda chini ya Rais mstaafu, Alli Hassan Mwinyi, ambayo imeshaanza kuonyesha kutokuwa na uwezo uliotarajiwa kutatua suala hilo linaloonekana kuizidi kimo CCM.
Chuki miongoni mwa wabunge na mawaziri wa CCM sasa imeonekana si kukitafuna chama bali hata mgawo wa umeme uliopo ambao baadhi ya watendaji shirika la ugavi wa umeme nchini (TANESCO) walishatoa mapendekezo kadhaa serikalini ili kuinusuru nchi kuingia katika janga hilo.
Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Dk. Idris Rashid, ni mmoja wa watendaji waliosimama kidete kuelezea mipango yao ya kuboresha uzalishaji wa umeme ikiwemo kununua mitambo mipya, kununua ya Dowans na mingine ambayo ilikumbana na vikwazo vikali.
Baada ya Dk. Idris kupata upinzani huo alitangaza kuwa TANESCO imejitoa kununua mitambo ya Dowans huku akionya kuwa shirika hilo lisije likalaumiwa kwa mgawo ambao ungejitokeza Oktoba na Novemba mwaka huu.
Onyo hilo la Dk. Idris lipokewa kwa shutuma nzito na baadhi ya wanasiasa wakiongozwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ambayo ilidai bora nchi iingie gizani kuliko kununua mitambo hiyo.
Mgawo wa umeme ulioanza wiki iliyopita wa saa 14 kwa siku ndiyo umewafanya baadhi ya wananchi, wanasiasa, wafanyabiashara kukumbuka onyo la Dk. Idris na kuwalaumu viongozi walioshiriki kwa namna moja au nyingine kukwamisha mipango ya TANESCO.
Wakati mgawo wa umeme ukionekana kushika kasi Kamati ya Nishati na Madini, chini ya Mbunge wa Bumbuli, William Shelukindo (CCM), itangaza kufanya uchunguzi ili kuona kama mgawo huo umesababishwa na watendaji wa TANESCO ili kutimiza mipango yao hasa ya kununua mitambo ya Dowans.
Kamati hiyo ilizungumza na watendaji wa TANESCO na baadaye ilisalimu amri kuwa mgawo huo ulitokana na kuharibika kwa mashine kadhaa pamoja na upungufu wa maji kama ambavyo shirika hilo lilivyotangaza.
Baadhi ya wafanyabiashara wenye viwanda wameingiwa na hofu ya kuendelea kufanyabiashara hasa kutokana na mgawo huo ambao umeathiri kwa kiwango kikubwa uzalishaji.
Shirikisho la Wenye Viwanda Nchini (CTI) ni miongoni mwa wadau waliojitokeza kutaka nchi isiendelee kuwa gizani kwa kuendekeza maamuzi yenye athari ilhali kuna mitambo yenye uwezo wa kuzalisha umeme lakini inashindwa kutumika.
Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) ni miongoni mwa taasisi za serikali zinazoathirika na mgawo huo kwa kuwa imekuwa ikipoteza mapato mbalimbali iliyokuwa ikiyapata kutokana na uzalishaji mali.
Wachambuzi wa masuala ya kiuchumi wameweka bayana kuwa nchi ipo hatari kuporomoka zaidi kiuchumi kama serikali haitochukua hatua za haraka kutafuta vyanzo vya kudumu vya kuzalisha nishati ya umeme ambayo hutegemewa na viwanda mbalimbali.
Wakati wachambuzi hao wakitoa tahadhari hiyo, Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Zitto Kabwe, ambaye siku za nyuma alijitokeza hadharani kulitaka Bunge na serikali kufikiria upya juu ya mitambo ya Dowans na ikiwezekana wainunue ili nchi isiingie gizani ameibuka tena kuitaka serikali itaifishe mitambo hiyo.
Zitto alisema uamuzi wa kuitaifisha mitambo hiyo ni mgumu lakini kwa hali ilivyo hivi sasa ni lazima viongozi wakubali kufanya umuzi huo hata kama watasakamwa na wahisani kwa kukiuka sheria.
Hoja hiyo ya Zitto kwa kiasi kikubwa imeonekana kuungwa mkono na kada mbalimbali za wananchi huku serikali kupitia kwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, akikataa kufanya hivyo kwa madai ni kukiuka sheria za nchi.
Kauli hiyo ya Ngeleja imeonekana kupingwa na baadhi ya watu wakiwemo wanasheria ambao wameweka bayana kuwa serikali imekuwa ikikiuka sheria mbalimbali ambapo wakati mwingine si kwa manufaa ya walio wengi hivyo ni vema kufikiria upya wazo la Zitto.
Tindu Lissu ni mmoja wa wanasheria aliyeweka wazi kuwa serikali haiwezi kuwa na kesi ya kujibu kama ikifikia hatua hiyo kwa kuwa sheria ya kimataifa ya uwekezaji pamoja na namna mitambo hiyo ilivyoingia hapa nchi imegubikwa na mizengwe.
Mwanasheria ameweka bayana kuwa hofu hiyo ya serikali haipaswi kupewa nafasi katika kipindi hiki ambacho nchi ipo hatarini kuporomoka kiuchumi kutokana na kushuka kwa uzalishaji viwandani.
Mgawo wa umeme umeonekana kuibua upya sakata la vita ya ufisadi ambalo lilishika kasi baada ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa kutokana na kuhusishwa katika kashfa ya kuipa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharula kampuni ya Richmond ambayo ilibainika kutokuwa na uwezo.
Sakata la Richmond ndilo kwa kiasi kikubwa lililozaa ufa na makundi yenye kuhasimiana vikali ndani na nje ya Bunge kiasi cha kuhatarisha mustakabali wa CCM ambao katika siku za hivi karibuni umekumbwa na kashfa mbalimbali.
Wachambuzi wa masuala ya siasa wanaona serikali itakuwa na wakati mgumu wa kuamua kipi cha kufanya kumaliza tatizo la mgawo wa umeme ambalo kwa namna moja au nyingine lilisababishwa na utendaji usio makini pamoja na tamaa za watu waliopewa jukumu la kuongoza nchi.
Moja kati ya sababu inayowafanya wachambuzi hao kuiona serikali kuwa iko njia ni ukweli kuwa wabunge walio katika mstari wa mbele kupinga baadhi ya mambo ni kutoka CCM ambacho ndicho chama kilichoshikilia dola.
Wachambuzi hao pia hawakusita kueleza wakati mgumu itakaokumbana nao Kamati ya Mzee Mwinyi iliyopewa jukumu la kutatua uhusiano mbovu baina ya wabunge na mawaziri ulioshamiri hivi sasa.
Ugumu wa Kamati ya Mzee Mwinyi unadaiwa utachagizwa zaidi na joto la uchaguzi mkuu ambapo kila mbunge anataka kuonekana anawajibika kwa wananchi wake hivyo kuwawia vigumu viongozi wa serikali. (Habari toka Mtanzania Daima)
Thursday, October 15, 2009
Mzee wa Mavocal aondoka na Milioni 25

Ungekuwa wewe ungefanyaje?
Amekua muda mrefu akihisi mke wake anamuibia kwa kutembea nje yandoa. Akaamua aandae safari feki na kurudi ghafla bila mkewe kutarajia. Akarudi na Taxi usiku wa manane na aliamua dreva Taxi aweshahidi, akamlipa 100,000 ili waende wote kufumania. Akanyanyua Bastola, wakanyatia ndani mpaka chumba chakulala, akaingia yeye na dereva taxi kwa kupanda kwa kamba,akawasha taa na dreva akafunua blanketi alilojifunikia mke wake....wapo wawili!Mke wa jamaa yu kitandani na mwanaume mwingine!!!Jamaa akaweka bastola kichwani kwa yule mwanaume mgoni wake, ghafla mke wake akapaza sauti, “Usimuue!Huyu bwana ametusaidia sana! Nlikudanganya niliposema nimerithi fedha. Ni yeye alinunua lile LandCruiser VX niliyokununulia, alilipia hii nyumba tunayomiliki sasa, alinipa zile pesa tulikuwa tunadaiwa na benki na analipia tiketi zetu zotetunavyoendaga maonyesho. Ndiye pia anayelipia ada za watoto wetu, hata hiyo suti uliyovaa na nyingine. Pia analipa kodi zetu za kilamwezi!”Huku akiyumbayumba kwa kutoamini, MME AKASHUSHA BASTOLACHINI, akamtazama dereva, akamuuliza, UNGEFANYA NINI UNGEKUWA NI WEWE? Dreva Taxi akamwambia; “Mfunike bwana, mfunike na hilo blanketi kabla hajasikia baridi”
Tuesday, October 13, 2009
Mwanamuziki wa Kundi la Boyzone Stephen Gately amefariki Dunia akiwa katika mapumziko huko Majorca

Chanzo cha habari kimesema Stephen mwenye umri wa miaka 33 alienda kulala kama kawaida lakini hakuweza kuamka asubuhi. Mwanamuziki mmojawapo wa Band Ronan Keating amesema kundi limepata pigo kubwa kutokana na kifo hiki. Stephen kakutwa umauti akiwa na partner wake wa miaka mingi ambaye walifungua ndoa ya watu wenye jinsia moja 2006 anayejulikana kama Andrew Cowles. Wanamuziki 4 waliosalia katika kundi la Boyzone wamesafiri asubuhi ya leo kuelekea"Majorca .
Monday, October 12, 2009
Jaji wa Marekani Aliyewalawiti Wafungwa Kufungwa Maisha akipatikana na Hatia

Jaji Herman Thomas, jaji ambaye alikuwa akiheshimika sana kiasi cha kwamba alikuwa akitabiriwa kuwa jaji mkuu wa kwanza mweusi wa Alabama Kusini, huenda akahukumiwa kwenda jela maisha baada ya kupandishwa kizimbani kwa tuhuma za kuwalawiti wafungwa wanaume ili awapunguzie adhabu zao.Jaji Thomas anakabiliwa na tuhuma za makosa 78 ya kukiuka misingi ya kutoa haki, kulawiti wafungwa, kuwateka wafungwa na kuwashambulia waliokataa kulawitiwa.Jaji huyo mwenye umri wa miaka 48, alijitetea kwamba hakufanya kitendo hicho na kwamba alikuwa akikutana na wafungwa ili kuwapa miongozo bora.Wakili wa jaji huyo alidai kwamba mteja wake amebabimbikiwa kesi hiyo na wafungwa ili kumchafulia jina lake kwa kazi nzuri ya ujaji aliyoifanya kwa miaka 20.Jaji Thomas na wakili wake walidai kwamba kesi aliyofunguliwa ni njama za wanasiasa ambao hawapendi mafanikio yake.Lakini mahakama iliambiwa kwamba Jaji Thomas alianza kufuatiliwa mienendo yake baada ya kuibadilisha hukumu ya binamu yake mwaka 2006 ingawa hukumu ya kesi hiyo ilikuwa imetolewa na jaji mwingine.Mahakama iliambiwa pia kwamba jaji Thomas alizichukua kesi walizopewa majaji wengine bila ya kufuata taratibu husika.Baadhi ya wafungwa wanaume walielezea jinsi walivyotolewa jela na kupelekwa kukutana na Thomas kwenye gari lake au ofisini kwake.Awali kulikuwa na taarifa za wafungwa kuvuliwa nguo zao za ndani na kisha kuchapwa bakora halafu ndipo zilipojitokeza taarifa za kulawitiwa kwa wafungwa na wafungwa wengine kulazimishwa wajipigishe punyeto mbele yake.Wafungwa wote waliolawitiwa na jaji huyo walikuwa ni wafungwa weusi hakukuwa na mfungwa mzungu kati yao.Alama za bakora kwenye matako ya baadhi ya wafungwa na pia alama ya majimaji ya mbegu za kiume za mfungwa aliyelazimishwa apige punyeto kwenye zulia la ofisi ya jaji huyo ni miongoni mwa vielelezo vya ushahidi dhidi ya jaji huyo.Wafungwa waliotoa ushahidi waliweza kuelezea vizuri kabisa jinsi ilivyo ofisi ya jaji huyo ambayo haina madirisha.Thomas alijiuzulu nafasi yake mwaka 2007 baada ya tuhuma za wafungwa kuchapwa bakora kwenye makalio yao kusambaa.Waendesha mashtaka walisema kwamba kuna wafungwa 15 wapya na wa zamani ambao wako tayari kutoa ushahidi wa kulawitiwa na jaji huyo.Ushahidi huo utachukua wiki kadhaa na jaji Thomas huenda akahukumiwa kifungo cha maisha iwapo atapatikana na hatia.
Subscribe to:
Posts (Atom)
VJN Super Motors
Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote