Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Thursday, October 29, 2009

Awekwa chini ya Ulinzi kwa kuongopa kaibiwa mtoto

MWANAMKE anayejulikana kwa jina la Maua Ally (29) amejikuta anashikiliwa na polisi baada ya kupiga mayowe ya uongo akilalamika kuwa mtoto wake aliyemzaa katika Hospitali ya Temeke ameibwa na watu wasiofahamika. Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Temeke, Liberatus Sabasi amesema, Jeshi la Polisi lilipokea taarifa kutoka kwa Muuguzi Mkuu wa Hospitali hiyo Nusura Simba (49), kuwa kuna mwanamke analalamika kuwa ameibiwa mtoto wake.Kamanda alisema kuwa kwa mujibu wa maelezo ya mwanamke huyo alidai kuwa, alifika katika hospitali hiyo akiwa anaumwa uchungu wa kujifungua na alipofika hapo alipokelewa na daktari kisha kupelekwa chumba cha kuzalisha [labour wodi], ambapo alifanikiwa kujifungua mtoto wa kiume.Mwanamke huyo alidai kuwa cha kushangaza baada ya kutoka chumba hicho hakumuona mtoto wake na ndipo alipoamua kutoa taarifa kwa uongozi wa hospitali hiyo.Baada ya jeshi la polisi kupokea taarifa hizo kutoka kwa uongozi wa hospitali hiyo, walifika hospitalini hapo na kumhoji mwanamke huyo chini ya ulinzi wa polisi na katika kumuoji kwa kutumia mbinu za kipolisi mwanamke huyo alikiri hakujifungua wala hakuwahi kuwa mjamzito na alifika hospitalini hapo kwa kuwa alikuwa na shida ya mtoto.Alidai kuwa aliamua kufanya hivyo na kutoa taarifa za uongo kwa sababu mume wake amekuwa akimshinikiza kubeba mamba na kutaka mtoto kwa muda mrefu na alimuongopea mume wake huyo alikuwa mjamzito.Ndipo alipoamua kufanya mbinu hiyo ili mume wake huyo ajue ni kweli alijifungua na mtoto wake aliibiwa na manesi na kuomba samahani kwa mapolisi hao na kwa uongozi wa hospitali hiyo kwa kitendo alichokifanya cha kudanganya.Kamanda Sabasi amesema kutokana na taarifa hizo, uchunguzi wa kitaalamu ulifanyika dhidi ya mwanamke huyo na walibaini kuwa mwanamke huyo hakujifungua na hakuwa na dalili hata ya kuwa na mimba. Kamanda Sabasi amesema kuwa, mtuhumiwa huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote baada ya upelelezi kukamilika kujibu shtaka hilo kwa kuuongopea umma.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote