CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kilolo, kimepata pigo baada ya mwanachama wake aliyepita bila kupingwa katika nafasi ya Mwenyekiti, Ashery Kigava wa Kitongoji cha Amani katika Kijiji cha Lukani, kufariki dunia wakati akisubiri kutangazwa kuwa mshindi.
Akitoa taarifa ya kifo hicho, mbele ya Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Profesa Peter Msolla wakati wa mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Lukani, Diwani wa Kata ya Ukumbi, Chesco Ngimba alisema kifo cha mwenyekiti huyo mteule kilitokea juzi. Kwa upande wake, Profesa Msolla mbali ya kutoa rambirambi kwa wafiwa, alisema CCM imepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha kiongozi huyo mratajiwa na kuongeza kuwa, ni pingo ndani ya chama na kitongoji hicho.
Akitoa taarifa ya kifo hicho, mbele ya Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Profesa Peter Msolla wakati wa mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Lukani, Diwani wa Kata ya Ukumbi, Chesco Ngimba alisema kifo cha mwenyekiti huyo mteule kilitokea juzi. Kwa upande wake, Profesa Msolla mbali ya kutoa rambirambi kwa wafiwa, alisema CCM imepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha kiongozi huyo mratajiwa na kuongeza kuwa, ni pingo ndani ya chama na kitongoji hicho.
No comments:
Post a Comment