Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, October 26, 2009

Mgombea wa CCM afariki dunia akisubiri kutangazwa mshindi

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kilolo, kimepata pigo baada ya mwanachama wake aliyepita bila kupingwa katika nafasi ya Mwenyekiti, Ashery Kigava wa Kitongoji cha Amani katika Kijiji cha Lukani, kufariki dunia wakati akisubiri kutangazwa kuwa mshindi.
Akitoa taarifa ya kifo hicho, mbele ya Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Profesa Peter Msolla wakati wa mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Lukani, Diwani wa Kata ya Ukumbi, Chesco Ngimba alisema kifo cha mwenyekiti huyo mteule kilitokea juzi. Kwa upande wake, Profesa Msolla mbali ya kutoa rambirambi kwa wafiwa, alisema CCM imepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha kiongozi huyo mratajiwa na kuongeza kuwa, ni pingo ndani ya chama na kitongoji hicho.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote