Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, October 30, 2009

Kenya kufanya sensa ya mashoga

Serikali ya Kenya iko mbioni kufanya sensa ya kuwahesabu mashoga waliopo nchini humo katika jitihada zake za kuwaelimisha watu juu ya ugonjwa wa ukimwi.
Serikali ya Kenya inajiandaa kuwahesabu mashoga waliopo nchini humo ingawa kwa sheria za Kenya mashoga huadhibiwa kwenda jela miaka 14 wanapokamatwa.Nicholas Muraguri, mkuu wa taasisi ya kuzuia kuenea kwa ukimwi ya Nascop, akiongea na shirika la habari la BBC alisema kuwa kuna umuhimu mkubwa serikali ya Kenya kufanya takwimu ya mashoga nchini humo.Alisema kuwa mashoga wengi hawana elimu kuhusiana na ugonjwa wa ukimwi.Hata hivyo wachambuzi wa mambo wanahofia kuwa mashoga wengi watahofia kujitokeza kuhesabiwa kwa kuhofia kukamatwa na kutupwa jela.Muraguri alisema kwamba takwimu hiyo itahusisha pia mashoga kutajana wenyewe kwa wenyewe huku maafisa wengine wakiwapima kama wameambukizwa virusi vya ukimwi pamoja na kuwafundisha njia salama za mapenzi."Wakenya hawawezi kusema kuwa mashoga ni jamii iliyotengwa, ni miongoni mwa jamii zetu", alisema Muraguri."Kundi hili inabidi lifikiwe na lipewe mafunzo ya jinsi ya kujilinda wasiambukizwe", alisema.Sensa hiyo ya mashoga imewagawanya Wakenya wengi huku baadhi yao wakisema hawaamini kama itasaidia chochote katika kuzuia kuenea kwa ukimwi.Baadhi ya mashoga waliohojiwa na BBC walitanabaisha kuwa wako tayari kuhesabiwa iwapo sensa hiyo itafanyika kwa siri.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote