Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, October 12, 2009

Nani atakuwa Star wa Bongo mwaka huu?

Mdhamini mkuu wa shindano la Bongo Star Search, Kampuni ya Vodacom, juzi imetangaza zawadi ya washindi watakaoibuka katika kinyanganyiro hicho.Akitangaza zawadi hizo Meneja wa Udhamini wa Vodacom Emillian Rwejuna alisema kuwa fainali za shindano hilo zitafayika katika ukumbi wa Diamond Jubilee mnamo tarehe 13 mwezi huu.Katika fainali hizo mshindi wa kwanza ataibuka na zawadi nono ya shilingi Milioni 25, mshindi wa pili atajinyakulia shilingi Milioni 5, mshindi wa tatu atajinyakulia shilingi Milioni 3 ambazo ni fedha taslimu pamoja na zawadi ya shilingi laki tano kutoka kwa Shear Illusion ambao ni moja ya wadhamini.Mshindi wa nne ataondoka na shilingi milioni moja na nusu na mshindi wa tano ataondoka na shilingi milioni moja.Kwa upande wa burudani, safu ya burudani itaongozwa na Shaa, Feisal Ismail, baby Madaha, Abubakar Mzuri na wasanii wengine kibao aliseama Ritta.Washindi waliofanikiwa kuingia katika tano bora ambao watagombania nafasi ya kuwa supa staa mpya wa Bongo ni Paschal Cassian wa Mwanza, Beatrice William wa mwanza, Peter Maechi toka mkoa wa Kigoma, Jackson George anayewakilisha mkoa wa Tanga na Kelvin Mbati toka Mkoa wa Dar es Salaam.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote