Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Friday, October 30, 2009

Babu wa Miaka 112 aoa Binti wa Miaka 17

Babu mwenye umri wa miaka 112 wa nchini Somalia ambaye ana jumla ya watoto 18 amefunga ndoa na binti mwenye umri wa miaka 17 katika sherehe kubwa iliyohudhuriwa na mamia ya watu nchini Somalia. Mamia ya watu walifurika kwenye harusi ya babu mwenye umri wa miaka 112 wakati alipokuwa akifunga ndoa na mwanamke ambaye amemzidi jumla ya miaka 95.Ahmed Muhamed Dore ambaye tayari ana watoto 18 kutokana na wake zake watano alisema kuwa anahitaji watoto zaidi kutoka kwa mkewe mpya Safia Abdulleh, ambaye ana umri wa miaka 17."Leo Mwenyezi Mungu amenitimizia ndoto yangu", alisema Ahmed baada ya harusi iliyohudhuriwa na mamia ya watu kwenye mji wa Galguduud.Familia ya bi harusi ilisema kwamba binti yao ana furaha sana kuolewa na Ahmed.Ahmed alisema kuwa mke wake ambaye kwa umri wake ni sawa na umri wa kitukuu chake wa kike, wanatoka kijiji kimoja.Ahmed alidai kwamba alimsubiria kwa miaka mingi sana Safia afikie umri wa kuolewa ili atimize ndoto yake ya kumuoa."Sikumlazimisha aolewe na mimi, nilitumia ujuzi na uzoefu wangu wa kuwavutia wanawake ili anikubali nimuoe na hatimaye alikubali nimuoe", alijisifia Ahmed.Ndoa hiyo imeelezewa na wanahistoria wa Somalia kuwa haijawahi kutokea nchini humo watu wakafunga ndoa wakiwa na tofauti ya umri miaka 95, miaka mitano tu pungufu ya karne moja.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote