Wakati kesho watani wa jadi nchini Simba na Yanga zikiingia uwanjani kupambana katika mchezo wa ligi kuu ya soka ya Tanzania bara, uongozi wa timu ya Simba umewaahidi wachezaji kuwapa Sh. Milioni 30 kama watashinda mchezo huo. Hatua hiyo ni kujibu mapigo kwa Yanga, ambapo gazeti moja la kila wiki lilidai kuwa wachezaji wa timu hiyo wameahidiwa kiasi cha sh. milioni moja kwa kila bao litakalofungwa dhidi ya Simba. Habari za ndani kutoka katika kambi ya timu hiyo iliyopo Zanzibar, wachezaji hao wameahidiwa fedha hizo na kundi la wanachama wa klabu maarufu kama Friends of Simba endapo watashinda mchezo huo. Ni kweli tumeambiwa kuna milioni 30 ambazo tutapewa kama tutafanikiwa kuwafunga Yanga katika mchezo wetu wa Jumamosi, alisema mmoja wa wachezaji waliopo kwenye kambi ya timu hiyo ambaye akupenda jina lake litajwe gazetini. Alisema tangu kuanza kwa kambi ya timu hiyo mjini Zanzibar wiki iliyopita wachezaji wamekuwa katika mazoezi makali kwa ajili ya kujiandaa na mchezo huo.
Aidha, alisema wachezaji wenzake wapo kwenye morali kubwa na wanaamini wataibuka na pointi tatu katika mchezo huo wa ligi kuu Tanzania bara. Alipoulizwa msemaji wa timu hiyo, Cliford Ndimbo juu ya ahadi hiyo alisema hana uhakika na suala hilo kwa kuwa hajapewa taarifa rasmi na uongozi wa juu wa klabu hiyo.
Aidha, alisema wachezaji wenzake wapo kwenye morali kubwa na wanaamini wataibuka na pointi tatu katika mchezo huo wa ligi kuu Tanzania bara. Alipoulizwa msemaji wa timu hiyo, Cliford Ndimbo juu ya ahadi hiyo alisema hana uhakika na suala hilo kwa kuwa hajapewa taarifa rasmi na uongozi wa juu wa klabu hiyo.
No comments:
Post a Comment