Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Wednesday, October 21, 2009

Kumbe mambo ya Limbwata hadi Majuu yapo !!!!!!!Cristiano Ronaldo apigwa JUJU

Mganga mmoja wa nchini Hispania ametamba kumpiga juju nyota wa Real Madrid asifurukute ndani ya Real Madrid na aandamwe na majeraha mpaka msimu utakapoisha. Uongozi wa club ya Real Madrid umepokea barua toka kwa mganga Jose Ruz, mwenye umri wa miaka 58 mkazi wa mji wa Malaga, ambaye ni maarufu kwa jina la "Pepe" akiwataarifu kuwa amemroga nyota huyo wa Ureno asifurukute kabisa uwanjani wakati akiichezea klabu ya Real Madrid. Pepe amedai kwamba Ronaldo ataandamwa na majeraha msimu mzima na kiwango chake cha soka kitashuka. Pepe alisisitiza kwamba hana nia mbaya na Real Madrid isipokuwa anatimiza wajibu wake kama mganga baada ya kutakiwa na mteja wake ampige juju Ronaldo."Nafanya kazi yangu kwa mujibu wa matakwa ya mteja wangu ambaye pia mtu maarufu na anajuana vyema na Ronaldo".Mganga huyo alidai kwamba mmoja wa wapenzi wa zamani wa Cristiano Ronaldo ndiye aliyemtaka ampige juju Ronaldo kutokana muda aliompotezea baada ya kuwa naye na kisha kumtosa.."Ronaldo atajeruhiwa vibaya sana uwanjani, siwaahidi lini ataumia, lakini subirini muone", alitamba Pepe.Cristiano Ronaldo ndiye mchezaji ghali kuliko wote duniani baada ya kuhama kutoka Manchester United ya Uingereza kuhamia Real Madrid ya Hispania kwa uhamisho uliovunja rekodi ya dunia wa paundi milioni 80.

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote