Uwepo wa Site hii Unategemea sana Ushirikiano wangu na wako, na ni njia mojawapo ya kuonyesha mshikamano na Jamii inayotuzunguka , PLS Usisite kunitumia Habari au kitu chochote chenye Uhakika ambacho hisia zako zitakupeleka kuwa kitaleta Mabadiliko na mafunzo katika jamii, Kumbuka kuwa msaada si Fedha wala Lulu bali chochote kinachoweza kuleta mabadiliko katika Maisha ya mtu mwingine. Kwa lolote usisite kuwasiliana nami kupitia chingasite@gmail.com au tumainijhn@yahoo.co.uk au simu No. 0712221744 na 0787221744. Karibuni Wote
Powered By Blogger

Monday, October 19, 2009

Simba Yaigeuza asusa JKT Ruvu 4 -1

AUNGURUMAPO Simba mcheza nani?, ndiyo hali inayoendelea kwa sasa katika Ligi Kuu ya Vodacom baada ya vinara hao kuichakaza JKT Ruvu kwa mabao 4-1 kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam jana. Maafande hao wa JKT wanaosifika kwa kutandaza soka ya kuvutia walishindwa kuhimili vishindo vya mnyama huyo aliyepania kutwaa ubingwa msimu huu na kujikuta wakiruhusu mabao mawili katika dakika mbili. Mshambuliaji Uhuru Selemani aliifungia Simba bao la kwanza katika dakika ya 29, kwa kumalizia mpira uliotemwa na kipa Shaaban Dihile aliyekuwa akijaribu kuzuia shuti. Dakika moja baadaye beki wa kimataifa wa Kenya, Joseph Owino alifunga bao la pili kwa vinara hao akimalizia pasi ya Mussa Mgosi kwa kupiga shuti lililokwenda moja kwa moja wavuni. Kabla ya kiungo Ramadhani Chombo, 'Redondo' kufunga bao la tatu na Mgosi (78) kushindilia msumali wa mwisho kwa maafande hao. Hadi sasa Simba inashikilia rekodi ya kuwa timu pekee Duniani ambayo haijafungwa na wala haijatoa sare yoyote baada ya vinara wa Hispania, Barcelona kuharibu rekodi yao mwishoni mwa wiki walipolazimishwa sare na Valencia. Baada ya mabao hayo JKT walijirekebisha na kupata bao katika dakika ya 43 kupitia kwa Damac Makwaya aliyepiga mpira wa adhabu uliomshinda kipa Juma Kaseja aliyeudharau akifikiri unatoka na kufanya matokeo kuwa 2-1hadi mapumziko. Kipindi cha pili kilianza kwa kasi hadi dakika ya 50 ambapo kiungo wa Simba, Ramadhani 'Redondo' alifunga bao la tatu kwa kichwa akiunganisha krosi ya Salum Kanoni. Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, aliyeteuliwa kwenye kikosi cha wachezaji bora wa CHAN, Mgosi alipachika bao la nne kwa vijana hao wa Msimbazi akimalizia pasi ya Okwi. Kwa matokeo hayo Simba inaongoza ligi ikiwa na pointi 24 baada ya michezo nane ikifutiwa na Mtibwa Sugar (15) inayolingana pointi na Azam na Yanga lakini kuna tofauti ya mabao ya kufunga. (Habari toka Mwananchi)

No comments:

VJN Super Motors

Wauzaji Mahiri wa Spare za Pikipiki na Magari yote toka Europe na Japan, Tupo Mtaa wa Msikitini Musoma Mjini, Pia tunaweza kutoa hudumu kwa watu wa Dar es salaam, Wasiliana nasi kwa Sanduku la Barua 557 Musoma, Simu No. 0282620610 , Barua pepe : vincent_nye@yahoo.co.uk. Karibuni wote